Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA: aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kutimiza masharti ya ajira kwa Watumishi ikiwemo kuwapandisha madaraja na stahiki zingine?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali; naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza;

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa zoezi hili la upandishaji wa madaraja kwa maeneo mengine ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Mwanza inaonekana kwa mara ya mwisho ni tangu mwaka 2020/2021, na idadi ya watumishi walio kasimiwa kupandisha madaraja hailingani na waliopandishwa mpaka sasa;

Mheshimiwa Mwenyekiti, na suala la pili, kwa kuwa Serikali inatambua umuhimu wa likizo kwa watumishi hasa kada ya Walimu;

Je, Wizara ina mpango ngani kuhakikisha kwamba Wizara ya Fedha sasa haitapunguza ile ceiling ya fedha za likizo zilizopo na badala yake waongeze zaidi?

Nashukuru Mheshimiwa Mwenyekiti.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na jambo la watumishi kupandishwa madaraja nimeeleza katika jibu langu la swali la msingi; kwamba Serikali imeendelea kupandisha madaraja ikiwemo utaratibu wa mserereko, ambao ndio maarufu sasa hivi ambao unaingiza kundi kubwa la wafanyakazi katika kipindi kimoja ili kuweza kuwapandisha katika madaraja stahiki. Pamoja na hilo pia nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali haina mpango wa kupunguza fedha za wafanyakazi katika masuala yanayohusu likizo kama alivyoeleza katika swali lake la pili. Nashukuru sana.