Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Bwawa la Mandela Kwenjugo na Kamkole Mabanda?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; hivi sasa ipo mitambo ya Serikali kupitia DDCA inayochimba Bwawa la Kwenkambala na kwa Mahizi. Kwa nini Serikali isiibakishe mitambo hii ndani ya Wilaya ya Handeni itakapokamilisha Kwenkambala na kwa Mahizi ili iendelee kuchimba mabwawa hayo mawili ambayo unayazungumzia Mheshimiwa Naibu Waziri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili mradi wa HTM mkandarasi tayari amekwishapewa msamaha wa kodi na alikwishakamilisha usanifu. Ni lini mkandarasi huyu atakuwa site kuanza ujenzi mara moja kwa mradi huu mkubwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa Mbunge wa Handeni Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mitambo kubaki Handeni hakuna tatizo tutahakikisha inabaki mpaka imalize kazi. Kuhusu mradi wa HTM lini utaanza tayari, mkandarasi anapaswa kuwa site; kwa hiyo baada ya hapa Mheshimiwa Mbunge tuonane ili tufatilie kwa pamoja kuhakikisha mkandarasi anakuwepo site.