Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupanda Hifadhini mazao yanayofuatwa na wanyama waharibifu kutoka Hifadhi za Rungwa, Muhesi na Kizigo?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Itigi baada ya kuliwa mazao yao na hawa wanayama wanategemea kile kidogo ambacho Serikali imekiweka kwenye sheria ikiwemo kifuta machozi na kifuta jasho;

Je, ni lini sasa watamalizia kulipa wananchi ambao wameliwa mazao yao miaka miwili iliyopita?

Mheshimiwa Spika, swali la pili Serikali imegawa pori kubwa la akiba la Rungwa, Muhesi na Kizigo kuwa mapori yanayojitegemea. Rungwa peke yake, Muhesi peke yake na Kizigo peke yake. Muhesi imepakana sana karibu na vijiji vingi vya Itigi;

Je, ni lini sasa wataongeza askari wa wanyamapori ili angalau waweze kuwadhibiti hawa wanyama wanapotoka kule kuingia kwenye makazi ya watu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni mwezi wa tatu tumemaliza kulipa kifuta jasho na kifuta machozi katika Wilaya ya Manyoni hususan katika maeneo ya Vijiji vya Njiri, Rungwa, Sanjaranda na Itigi Mjini ambao walipata madhara makubwa ya wanyamapori wakali na waharibifu. Hivyo nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba kwa sasa hivi tumeshafanya tathmini kwa wale ambao wamebaki tutawalipa katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la askari, tumeshaomba tayari kuongezewa tena kwa mwaka huu askari waajiriwa ambao tayari tumeshapata kibali tunaamini kwenye maeneo ambayo yana changamoto za wanyama wakali na waharibifi tutaendelea kuongeza nguvu na vituo kujengwa ili angalau tupunguze athari hii ya wanyama wakali na waharibifu.