Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, lini Miradi ya Umwagiliaji katika Vijiji vya Msange na Mnghamo – Singida Kaskazini itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi kwanza nitoe shukrani na pongezi kwa majibu mazuri na ambayo yanaenda kutoa matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini ambao wanasubiri skimu hizi kwa hamu kubwa.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; katika Skimu ya Msange wananchi wanatumia mfumo wa mafuta, yaani diesel, kwa ajili ya kuendesha kilimo cha umwagiliaji na tayari wananchi wameshatuma maombi kwa ajili ya kubadilishiwa mfumo kwenda…

SPIKA: Swali.

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, je, Serikali iko tayari sasa kuwasaidia wananchi kubadilisha mfumo kutoka kwenye generator ili waepuke mafuta mengi na sasa watumie umeme?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna Bwawa la Mgori pamoja na Kisisya ambayo yamejaa tope na mifumo ya umwagiliaji imeharibika;

Je, Serikali iko tayari sasa kwenda kuyafufua mabwawa haya ili yaweze kuwasadia wananchi kuongeza kipato katika kilimo? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhani, Mbunge wa Singida Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Kilimo itakaa pamoja na Wizara ya Nishati ili kuhakikisha wanafanikisha jambo hili kuondoa wananchi kutoka kwenye generator kwenda kwenye umeme. Kwa hiyo, hilo tutakaa pamoja ili kulifanikisha hilo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Bwawa la Mgori na Kisisya ambayo yamejaa tope na yanahitaji kufufuliwa, nimhakikishie tu, kwamba nimezungumza na Waziri wa Kilimo na Wizara ya Kilimo itawatuma wataalam wake waende kufanya tathmini ili waweze kutafuta fedha kwa ajili ya kazi hiyo, ahsante sana.