Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa kurahisisha matumizi ya Kibenki kwa njia ya Simu kwa kutumia bando za simu badala ya salio la simu la kawaida?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naipongeza Serikali kwa majibu mazuri, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kuna double standard baadhi ya makampuni yameondoa utaratibu wa kutumia salio la kawaida unapoingia kwenye menu za kibenki na makampuni mengine bado yanataka utumie salio la kawaida badala ya bando ulilonalo kwenye simu. Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha makampuni yote yanatoa huduma hii kwa usawa kwa kuondoa utaratibu wa kutumia salio la kawaida ili Watanzania wote waweze kunufaika na kurahisisha matumizi yao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Pamoja na Serikali kusitisha gharama ya ongezeko la bando tokea Oktoba mwaka jana, kwa sasa hivi tatizo kubwa tulilokuwa nalo ni bando za kwenye simu zetu tunazoweka kuisha kwa kasi ya haraka sana. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha inaweka utaratibu maalum kwa ajili ya ku-regulate matumizi ya kasi za bando kwenye simu kama ilivyo limit kupanda gharama za matumizi ya bando kwenye simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Judith Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la kibiashara ni kama ambavyo nimejibu kwenye swali langu la msingi. Ni makubaliano kati ya mtoa huduma na benki na pale ambapo watoa huduma wanabadilisha wengine wanakuwa hawatozi ni masuala ya kiushindani ambapo sisi kama Serikali kazi yetu ni kuweka mazingira wezeshi ili ushindani uweze kutokea.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo unapotumia USSD, USSD maana yake si suala la kutuma meseji na kupokea, ni suala ambalo linakuwa linatoa options zingine ambazo mtumiaji anaweza kuona, na kuna hatua nyingi ambazo zinafanyika. Kwa hiyo, suala la kutumia bando ili uweze kukata huduma ya USSD inakuwa ni ngumu ni sawasawa na pale unapojiunga na bando halafu ukajaribu kupiga simu nje ya nchi. Hilo ni jambo haliwezekani, labda kama itawezekana tutakaa na watoa huduma ili tuangalie kama kuna uwezekano wa kuwepo na bando la USSD ili liweze kuhudumia huduma maalum.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili suala la kasi katika matumizi ya bando, kasi ni matumizi ya mtumiaji husika. Kama ana vitu vingi vya ku-download na kuna vitu vingi vya ku- upload matokeo yake ni kwamba kasi ya bando ambalo atakuwa amejiunga litaisha mapema. Kwa hiyo, naendelea kushauri kwamba watumiaji wa bando waweze kuangalia matumizi halisi katika simu zao na pale ambapo wanakuwa hawatumii basi waweze kuzima data ili data isiweze kuisha, ahsante.