Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza:- Je, lini Wananchi wa Kata ya Moshono katika barabara ya mzunguko ya Kona ya Kiserian watalipwa fidia?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwanza sikubaliani na majibu ya Serikali kwenye swali langu la msingi kwa sababu ukizingatia kwamba sheria ni mwaka 2007, leo ni mwaka 2023 miaka 16 sasa bado Serikali inasema inatafuta fedha na huku wameweka vigingi kwenye maeneo ya wananchi lakini ingekuwa ni mwananchi ndiyo ameingilia kwenye hilo eneo Serikali ingeenda kumwondoa kwa nguvu. Baada ya maelezo hayo naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, ni lini sasa Serikali itawalipa fidia wananchi hawa? Swali la pili, kama Serikali haina uwezo wa kulipa fidia, kwa nini isiwaruhusu wananchi hawa wakaendeleza maendeleo hayo mpaka watakapokuwa tayari kuwalipa fidia?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kulipa wale wote ambao waliathirika na ujenzi huu wa Arusha Bypass kwa maana hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wananchi wa Arusha waendelee kuwa na subira wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wananchi waruhusiwe kujenga maeneo haya. Nchi yetu inaongozwa kwa mujibu wa sheria na taratibu na sheria ya kuhifadhi barabara ambayo ilianza tangu mwaka 1932 enzi za ukoloni na ikarudiwa mwaka 1967 na tukatunga sheria mpya mwaka 2007 ambayo inataka hifadhi ya barabara kutoka kati kati ya barabara mpaka upande wa pili iwe mita 30 na kutoka kati kati tena upande mwingine iwe mita 30 kwa maana ya kwamba jumla ni mita 60.

Mheshimiwa Spika, kwa maana hiyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge na Watanzania wote kwamba sheria hii lazima tuilinde na ikizingatiwa kwamba Arusha ni mjini tunahitaji pia kuendeleza miundombinu mizuri pale Arusha ili jiji hili la kitalii na kwa maana hiyo tuna hakika tukifanya vizuri katika suala la miundombinu hata watalii pia wataongezeka zaidi.