Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuruhusu Mabasi ya Abiria yanayopita Wilayani Sikonge kuendelea na safari badala ya kuyalazimisha kulala?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kwa kuwa eneo la kutoka Sikonge kwenda Inyonga lenye kilometa 161 halina mawasiliano. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kunakuwepo na usalama kwenye eneo hilo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Mheshimiwa Waziri katika majibu yake amesema kwamba wamiliki wa mabasi wanaweza kuomba kuondoka, kuanza safari zao pale Dar es Salaam muda wa saa tisa usiku au saa kumi. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kutoa tamko hapa Bungeni kwamba mabasi hayo yanaweza kuanza safari muda wa saa tisa au saa kumi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Taska Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mkakati ambao tunao katika kuhakikisha eneo hilo linakuwa salama. Kwanza nikupongeze wewe binafsi kwa kuweza kutupatia changamoto ya kufikiria kuanza usafirishaji wa mabasi ya abiria usiku.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kutekeleza maagizo Mheshimiwa Spika na maombi ya Waheshimiwa Wabunge tumeshaanza kulifanyia kazi suala hilo.

Mheshimiwa Spika, tumekaa na Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi ambao ndiyo wadau wakubwa kuangalia jinsi ya kuweza kufanya na tumeamua kulipa majukumu Baraza la Usalama Barabarani la Taifa ambalo limesheheni wajumbe ama wadau kutoka taasisi muhimu ikiwemo Jeshi la Polisi, LATRA, TANROADS na kadhalika ili wataalam hawa waweze kutushauri namna bora ambayo itaweza kusaidia kuruhusu magari haya kuweza kutembea usiku ikiwemo hili eneo ambalo umeliruhusu.

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa mambo ambayo tunategemea kutoka kwa wataalamu hawa ni jinsi ya kuweza kudhibiti changamoto zilizopelekea maamuzi ya Serikali mwaka 1990 kuzuia ambayo ilikuwa ni mambo mawili makubwa.

Mheshimiwa Spika, moja; ilikuwa ni kutokana na changamoto ya ujambazi na utekaji kipindi hicho; pili; ilikuwa ni ajali ambazo zilikuwa zikitokea usiku na kuharibu maisha ya Watanzania wengi.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi; tunataka kuhakikisha kwamba wakati ambapo tunalitafakari jambo hili tutakaporuhusu tuweze kuhakikisha kwamba mabasi haya yanaruhusiwa kusafiri lakini wananchi wetu wanaendelea kubakia salama. Hivyo Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba jitihada hizi za kuhakikisha kwamba eneo hilo na maeneo mengine nchi nzima yanakuwa salama kuruhusu usafiri wa usiku yanaendelea.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni kuhusu tamko; kama ambavyo nimezungumza kwamba tunaomba nitoe tamko kwamba wale ambao wanaona kuna haja ya kuanza safari zao mapema basi walete maombi na tamko ni kwamba tutaridhia maombi hayo kwa wale ambao watakuwa na haja ya kuanza safari hizo wakati tunaendelea na jitihada hizo za kutafutia ufumbuzi wa kudumu suala hili.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri maombi anakuwa analeta nani, mmiliki wa chombo cha usafiri au unaleta mkoa husika au nani analeta hayo maombi?

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, maombi yawasilishwe na wenye vyombo vya usafiri ama wamiliki wa mabasi hayo ambayo yanahitaji kusafiri kwa nyakati hizo.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuruhusu Mabasi ya Abiria yanayopita Wilayani Sikonge kuendelea na safari badala ya kuyalazimisha kulala?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Mabasi ya abiria yanayosafiri kutoka Mkoa wa Dar es Salaam kwenda Mkoa wa Kagera na Nchi jirani ya Uganda kupita Wilaya ya Misenyi hulazimika abiria kulala katika Mji wa Kahama na wananchi kupata adha kubwa usiku kucha.

Mheshimiwa Spika, katika Pori la Biharamulo kuna vituo vya polisi vingi kila baada ya kilometa chache ambayo ni pongezi kubwa kwa Serikali.

Je, ni lini sasa mabasi yanayotoka katika Mkoa wa Dar es Salaam kwenda Mkoa wa Kagera na Nchi ya Uganda kuruhusiwa kusafiri mpaka kufika bila wananchi kulala njiani na kupata adha kubwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kyombo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake linafanana na swali ambalo la msingi ambalo Mheshimiwa Taska Mbogo ameuliza. Hivyo niombe majibu ambayo nimeyajibu kwenye swali la msingi yaendelee kubakia hivyo hivyo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuruhusu Mabasi ya Abiria yanayopita Wilayani Sikonge kuendelea na safari badala ya kuyalazimisha kulala?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi. Sheria zilizopo sasa Tanzania mabasi na malori yanatembea mchana na malori ndiyo yanayotembea usiku lakini duniani kote mabasi yanatembea muda wote, malori yanatembea mchana mwisho saa 12:00. Je, ni lini na sisi Tanzania tutakwenda na utaratibu ambao uko duniani ili twende na wenzetu katika maendeleo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya Massare kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, lengo ni kuhakikisha kwamba shughuli za uchumi zinaendelea kufanyika nyakati zote. Tunaamini kabisa kwamba mabasi na malori na magari yote yakiweza kutembea masaa 24 yatachangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, hivyo siyo suala la kusema yupi ni bora kuliko mwingine lakini changamoto ambayo nimeizungumza ni kwamba lazima tutakapofanya hivyo tuzingatie usalama wa wananchi wa nchi yetu na tumegundua kwamba mabasi na malori ndiyo ambayo ni visababishi vikubwa vya ajali. Nitatoa mfano wa ajali zilizotokea hivi karibuni ajali ambayo imetokea pale Tanga hivi karibuni ambayo iliua takribani Watanzania 20 ilikuwa ni kati ya lori na basi tena nyakati za usiku. Ajali iliyotokezea hapa Kongwa halikadhalika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba concern ya Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine kuona kwamba huduma hizi zinaweza kuimarishwa na kutoa nafasi kwa wananchi wetu kuweza kutoa mchango wao katika uchumi wa nchi yetu kwa ufanisi zaidi tumezipokea na tutazifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza mikakati hiyo imeshaanza na tuvute subira pale ambapo wataalam wetu watatushauri utaratibu bora zaidi wa kufanya basi tuweze kuruhusu mabasi hayo yaweze kutembea muda wote.