Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, lini Serikali itapitia upya masharti ya fomu za bima ya afya ili kuondoa upotevu wa fedha za Vituo vya Afya kwa kushindwa kujaza fomu hizo?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza, nashukuru kwa majibu yaliyotolewa.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Katika Hospitali yetu ya Mkoa wa Iringa imefungwa mashine ya CT-scan na inatoa huduma kwa wagonjwa wote isipokuwa wagonjwa wa bima ya afya kwa sababu NHIF wameshindwa kutoa kibali cha wagonjwa kupata huduma hizo. Swali langu ni kwa nini hawataki kutoa kibali?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; gari ya chanjo ya Manispaa ya Iringa ni ya mwaka 1998, imekwenda zaidi ya kilometa 380,000 na zaidi na hatuna gari, gari imechakaa kabisa. Ni lini tutapata gari hiyo ili wananchi waendelee kupata huduma za chanjo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kusema kwamba Rais wetu alipopokea nchi kwenye Tanzania nzima ni hospitali mbili tu za mikoa zilikuwa na CT-scan na kwa sasa hospitali zote za mikoa zimepelekewa CT-scan na zimebaki nne za ziada maana yake Rais wetu amefanya kazi kubwa mno. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tusingefurahi mtu yeyote awakoseshe Watanzania hiyo huduma ambayo Rais wao amepeleka. Kwa hiyo, niseme tu kwa niaba ya Waziri wa Afya nimuagize DG wa Bima kwamba mpaka kesho saa mbili watu wa Iringa ambao wanastahili kupata huduma na waliotimiza vigezo waanze kupata huduma.

Mheshimiwa Spika, swali lako la pili ni kwamba gari; tumezungumzia hapa tukasema zimenunuliwa Ambulance zaidi ya 727 maana yake hata Iringa itaenda kupata gari na tutaenda kuwekeza kwenye eneo hilo ambalo unasema ambalo ni muhimu sana la chanjo.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, lini Serikali itapitia upya masharti ya fomu za bima ya afya ili kuondoa upotevu wa fedha za Vituo vya Afya kwa kushindwa kujaza fomu hizo?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, ni lini bima ya afya watasajili vituo vipya vya afya kikiwemo cha Ng’uluhe, Ruaha Mbuyuni, Ilula pamoja na Nyalungu ili waweze kuanza kupata huduma watu kupitia mfuko wa bima ya afya?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ninachoweza kukwambia ni kwamba ninakuomba tukae chini leta vituo vyako ambavyo havijasajiliwa tutizame vigezo, vikikidhi vigezo zianze kusajiliwa na huduma itolewe.