Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, la kwanza. Kilwa Kisiwani kwa sababu ni kisiwa utaratibu wake ni wa kipekee. Je, na yenyewe nayo imo katika mpango huu na awamu hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Kata za Nanjirinji, Narikalage pamoja na vijiji vyake vya Nainokwe, Liwiti pamoja na Narikilage yenyewe inapitiwa na msitu wa hifadhi na kulikuwa na mgogoro kati ya REA na TFS: Je, mgogoro huo umekwisha na Serikali sasa iko tayari kusambaza umeme katika kata hizo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikianza na swali la kwanza, tunafahamu kwamba kuna vijiji katika Jimbo la Kilwa Kusini ambavyo vipo katika visiwa na upo mradi unaitwa RBF (Result Based Financing) awamu ya pili ambao utafikisha umeme katika visiwa hivyo pamoja na visiwa vingine Tanzania Bara 36 katika awamu hii. Kwa hiyo, pamoja na visiwa hivyo viwili, viko visiwa vya maeneo mengine vya maeneo mengine ambavyo pia vitafikishiwa umeme katika miradi hii ambapo tunatafuta sasa wakandarasi wa kupeleka mradi wa umeme katika maeneo hayo. Kwa upane wa Kilwa amepatikana Mkandarasi anaitwa Greenl Leaf ambaye anakamilisha taratibu za kupeleka umeme katika maeneo hayo ya visiwa.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili, ni kweli tulikuwa na changamoto ya mawasiliano katika ya Wizara ya Nishati na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitisha miundombinu ya umeme katika mapori ya TFS, lakini tatizo hilo sasa limekuwa solved, na sasa tunazungumza lugha moja. Kwa hiyo, sasa kunapokuwa na mradi unaohitaji kupita katika maeneo hayo, vibali vinatolewa na mradi unaweza kupitishwa kwa wakati.

Kwa hiyo, kwa sasa tatizo hilo limetafutiwa ufumbuzi na halina tatizo.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Pamoja na utekelezaji wa REA III unaoendelea Wilaya ya Nkasi lakini umeme unakatika kupita kawaida: Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutatua changamoto hii ambayo wananchi wangu wanapata hasara kubwa hasa wanaosindika Samaki?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wenzetu wa Nkasi wanapata umeme kutoka nje ya nchi, lakini mradi wa Gridi Imara unapeleka Gridi ya Taifa katika Mkoa wa Katavi ambao utafika pia katika Mkoa wa Rukwa na maeneo hayo. Kwa hiyo, ndani ya miezi kama 18 tatizo hili litakwisha kwa sababu tutakuwa tumefikisha umeme wa gridi kwenye maeneo hayo ambao ni umeme wa uhakika na ambao tunaweza tukau- control sisi wenyewe katika maeneo hayo.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini sasa mtaweza kufunga transformer mliyokuwa mmeahidi tangu Desemba ili kupunguza adha ya kukatikatika umeme kwenye Jimbo la Temeke? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, transformer iliyotakiwa kuwekwa katika eneo la Temeke ipo katika mchakato wa manunuzi kwa sababu tayari pesa ilishatengwa na uamuzi ulishafanyika, hivyo katika miezi miwili au mitatu inayokuja tunaamini taratibu za manunuzi zitakuwa zimekamilika na transformer itafungwa kwa ajili ya kuongeza uwezo wa umeme katika maeneo hayo kuweza kuwahudumia wananchi wote.

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 4

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni lini Serikali itapeleka umeme katika vitongoji 192 katika Wilaya ya Buhigwe? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kavejuru, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa REA III Round II ambao unaendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali tuliyokuwa nayo unaendelea kupeleka umeme katika vitongoji mbalimbali ambavyo vimo ndani ya vijiji. Pia, upo mradi wetu wa densification (ujazilizi awamu ya pili) ambao pia unaendelea kupeleka umeme kidogo kidogo katika maeneo ya baadhi ya vitongoji. Kwa awamu hii tuna vitongoji kama 2,630.

Mheshimiwa Spika, ili kumaliza tatizo hili la umeme katika vitongoji, Serikali ipo katika taratibu za kutafuta fedha takribani shilingi 6,500,000,000,000 kuhakikisha kwamba inapeleka umeme kwa mkupuo mmoja katika vitongoji vyote, takribani kama 36,000 tulivyokunavyo Tanzania Bara ambavyo havijafikiwa na umeme. Tunaamini mradi huu utakamilika na katika miaka mitatu au minne au mitano ijayo vitongoji vyote vitakuwa vimepata umeme.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 5

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mafinga tunaishukuru Serikali kwa kutufikishia umeme katika kila kijiji, hata hivyo vitongoji vingi havina umeme: Je, ni lini vitongoji vitaanza kupata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika swali lililotangulia la Mheshimiwa Kavejuru, Serikali ipo katika mpango mkakati mkubwa sana wa kutafuta fedha kwa ajili ya kupeleka umeme kwenye vitongoji vyote takribani 36,000 ambavyo vimebaki Tanzania Bara ambavyo havijapatiwa umeme kwa mradi utakaogharimu karibia Shilingi 6,500,000,000,000/=. Kwa hiyo, taratibu zitakapokamilika kila eneo linalohitaji umeme litafikishiwa miundombinu ya umeme katika vitongoji vyetu.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 6

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri matatizo ya mkandarasi wa REA aliyepewa tender ya kusambaza umeme kwenye Mkoa wa Songwe unayafahamu. Mpaka sasa hivi katika ya vijiji 127 amepeleka umeme kwenye vijiji 48 tu: Sasa hamwoni wakati umefika wa kuvunja naye mkataba kunusuru Mkoa wa Songwe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Songwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna baadhi ya maeneo ambapo Wakandarasi wetu hawajafanya vizuri. Tunachokifanya kikubwa ni kuhakikisha tunawasimamia kwa karibu kuhakikisha kwamba kazi zao zinakamilika kwa wakati. Katika eneo la Songwe, tumekuwa tukilifuatilia kwa karibu na Mheshimiwa Mwenisongole na tunamhakikishia kwamba ndani ya muda stahiki mradi huo utakamilika.

Mheshimiwa Spika, katika wale Wakandarasi ambao wako nyuma sana na hatuna namna, tutavunja mikataba yao, lakini wale ambao wanaweza kufanya kazi na kuikamilisha kwa wakati, tutasimamia vizuri ili tuweze kuikamilisha kwa wakati kwa sababu kuvunja mkataba pia siyo option nzuri ya kukamilisha mradi kwa wakati.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 7

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Serikali ilituahidi kutuletea mkandarasi kwa ajili ya kukamilisha vitongoji 47 vilivyoko ndani ya Jimbo la Hai: Ni lini mkandarasi huyo ataanza kazi ya kukamilisha kwenye vitongoji hivi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli taratibu za kumpata mkandarasi wa kwenda kukamilisha umeme katika maeneo ya Hai na maeneo mengine ya Kilimanjaro ambayo yalikuwa yameshamaliza level ya vijiji yanaendelea na tunaamini katika miezi miwili ijayo Mkandarasi atakuwa amepatikana, na ataenda kuingia site sasa kuweza kupeleka umeme katika maeneo hayo ambayo yalikuwa hayajafikiwa na umeme.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Vijiji vingi katika Kata za Narurango, King’ori, Majengo bado havijapata Umeme wa REA na Mkandarasi anavyofanya kazi yake wala haeleweki, analeta nguzo, anaondoka…

SPIKA: Swali!

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Umeme wa REA utafika kwenye hizo kata ili vijiji vyote vipate umeme kulingana na ahadi ya Serikali kwamba mwisho wa mwaka huu vingepata umeme? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tumetoa ahadi ya Serikali, tutahakikisha kwamba wakandarasi wote wanaotekeleza mradi wa REA III Round II kufikia Desemba mwaka huu kazi hizo zitakuwa zimekamilika katika maeneo ambayo yanapelekewa umeme kwenye kata, vijiji na vitongoji ili wananchi waweze kunufaika na hiyo huduma ya umeme ambayo iko katika huo mradi mkubwa wa mwisho wa kupeleka umeme katika vitongoji na vijiji.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Supplementary Question 9

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri kuna tume mliunda ya kupitia vijiji vile vyenye sura ya miji hivi: Lini tume hii itamaliza kazi ili wananchi wajue wako wapi kwenye kuunganishiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa OleleKaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tume iliundwa na ilipita kwenye baadhi ya maeneo kukusanya maoni na tulielekeza ihakikishe inamuona kila Mbunge. Majibu yalipokuja Wizarani tulivyojaribu ku-crosscheck na Waheshimiwa Wabunge tuligundua kuna Wabunge kwa bahati mbaya hawakufikiwa na hawakuonwa na timu hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tumeiagiza irudie upya zoezi hili kwenye yale maeneo ambayo ilikuwa haikufika na katika miezi miwili inayokuja tunaamini itakuwa imemfikia kila Mbunge na kupata maoni yake kwenye maeneo ambayo yanatakiwa kufanyiwa jitihada za kuhakikisha maeneo yenye uso wa mjini lakini ni vijijini yanapatiwa umeme kwa gharama ile nafuu. Kwa hiyo, majibu yatakapofikia mwisho tutaleta taarifa sahihi.