Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiopingika kwamba Majimbo ya Vijijini yana maeneo makubwa sana ya kiutawala lakini yana mahitaji makubwa ya elimu ya VETA.

Je, Serikali haioni sababu ya kuowandolea adha wananchi wa vijijini kutafuta elimu hii kwa umbali mrefu?

Mheshimiwa Spika, kutokana na hoja za swali nililouliza hapo juu, Serikali ni lini itajenga chuo cha VETA angalau kimoja kwenye Jimbo la Lulindi.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Mchungahela kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, lengo la ujenzi wa vyuo hivi katika ngazi za Wilaya ni kusogeza huduma hizi karibu kule Wilaya. Tunafahamu kweli zipo Wilaya ambazo zina maeneo makubwa ya kiutawala, lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati tunajenga vyuo hivi, tunaweka vilevile na huduma ya mabweni. Lengo la huduma za mabweni ni kuhakikisha wanafunzi wote ambao wanatoka mbali kuweza kukaa pale pale chuoni na kuweza kupata huduma hii kwa karibu zaidi. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi, bado tunaweza tukawahudumia wale ambao wametoka mbali kwa sababu watakuwa wanakaa pale pale chuoni.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, anazungumzia suala la ujenzi kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya swali la msingi, kwamba kwa sasa tunakamilisha kwanza ujenzi wa vyuo hivi katika wilaya hizi, halafu tutaangalia sasa yale majimbo yenye changamoto ikiwemo labda na jimbo lake pamoja na Jimbo la Nanyamba kule nako kuna malalamiko makubwa sana. Hii itategemea sasa vile vile na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, ahsante nakushukuru. Serikali mwaka 2021 iliahidi kujenga Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara Kata ya Kisawasawa. Sasa hivi tunapewa taarifa kwamba chuo hakitajengwa katika Halmashauri hiyo kwa sababu kuna Chuo cha Ufundi cha FDC. Chuo kinaenda kujengwa katika Halmasahuri ya Mlimba: -

Mheshimiwa Spika, nataka kujua: Je, kuwepo kwa Chuo cha Ufundi cha FDC ni sababu ya kukosa vyuo vya VETA? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Asenga, Mbunge wa Ifakara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu ya swali la msingi, vyuo hivi tunajenga katika ngazi ya Wilaya, havijengwi katika ngazi ya Halmashari. Ni jukumu la Wilaya kuangalia kwamba vinakwenda kujengwa wapi? Kwa zile Wilaya ambazo zina Halmashauri zaidi ya moja, ni lazima wakae chini Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi ili waweze kuamua wapi chuo hiki kinakwenda kujengwa? Kwa hiyo, sisi jukumu letu ni kwenda kujenga Chuo cha VETA lakini majukumu au wajibu wa kuchagua eneo gani la kwenda kujenga linabakia katika Wilaya husika.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa VETA Wilaya 63 na Wilaya ya Nyang’hwale tayari upembuzi yakinifu umeshafanyika; je, katika Wilaya 63 na Nyang’hwale ikiwemo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’hwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwamba vyuo hivi vinaenda kujengwa kwenye Wilaya na kama tayari tumeshafanya upembuzi yakinifu, tafsiri yake ni kwamba tumeshakuja kufanya Geotechnical Survey, Topographical Survey pamoja na Environmental and Social Impact Assessment. Kama shughuli zozote zimeshafanyika kwenye eneo lako, is likely kwamba chuo hicho kinakuja kujengwa kwenye eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ujenzi wa Chuo cha VETA Chemba umekamilika, nataka kujua ni lini sasa kitafunguliwa ili kidahili wanafunzi? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli ujenzi wa vyuo 25 vile vya Wilaya awamu ya kwanza pamoja na vinne vya Mikoa, tayari ujenzi umekamilika. Jukumu letu tulilonalo sasa hivi ni utafutaji wa vifaa na kuajiri walimu kwa ajili ya kwenda kufundisha kwenye maeneo hayo. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, mwaka ujao wa fedha kuanzia mwezi Julai tutaanza kutoa kozi za muda mfupi lakini kuanzia Mwezi wa Kumi tutafanya usahili sasa kwa ajili ya kozi za muda mrefu sambamba na upelekaji wa vifaa vya kufundishia kwenye maeneo hayo kwa sababu samani tayari tumeshapeleka.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale iliahidiwa kujengewa Chuo cha VETA kwenye bajeti hii inayotekelezwa sasa. Mpaka leo hii imebakia miezi miwili bajeti inakwenda kwisha: Je, lini tutapewa fedha hizi tuweze kujenga chuo hicho?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari tumeshapeleka fedha za awali kwa ajili ya mobilization na zile kazi za mwanzo; na kazi nyingine za Geotechnical Survey, Topographical pamoja na ESIA (Environmental and Social Impact Assessment) tayari zimeshafanyika. Kwa hiyo, hivi sasa tunachokamilisha ni kupata matokeo ya tafiti hizi tulizokwenda kufanya. Baada ya matokeo hayo, tayari tutapeleka fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa maeneo yote yale 63 tuliyoyataja.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 6

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Halmashauri yangu ya Nanyumbu imepokea fedha za ujenzi wa Chuo cha VETA, lakini cha kushangaza fedha hizi zimekabidhiwa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ambayo ipo kilometa 90 kutoka wilayani kwangu: Kwa nini fedha hizi zimepelekwa Masasi wakati Nanyumbu yupo mdhibiti ubora ambaye angesimamia fedha hizi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Yahya Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli fedha tumepeleka katika FDC ya Masasi na hatukupeleka kwenye Wilaya ya Nanyumbu moja kwa moja kwa sababu FDC Masasi ndipo ambapo fedha tutazipitishia pale. Tumeona ni muhimu kupitishia hizo pesa pale baada ya kufanya study ile ya ujenzi awamu ya kwanza; Vyuo vyote vya FDC wamesimamia vizuri zaidi vile vyuo vya VETA kuliko zile ofisi zetu za wadhibiti ubora. Kwa hiyo, tumepitisha kule kwa sababu ya kupata usimamizi makini kwa chuo chetu kile na matumizi ya fedha yaweze kuwa sahihi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 7

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kama alivyozungumza kwenye majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri kwa suala la FDC na VETA, kwamba lengo ni kupeleka katika kila Wilaya.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri haona sasa wakati umefika wa ku-engage TAMISEMI katika mlolongo huu wa kwenda kusimamia ili hivi vyuo kuwa endelevu? Serikali haioni wakati umefika wa kumshirikisha TAMISEMI katika usimamizi wa hivi vyuo vya ufundi? Nashukuru.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ametoa ushauri wa kwamba tushirikiane, lakini tumekuwa tukishirikiana kwenye eneo hili la utoaji wa elimu kuanzia shule hizi za msingi, sekondari mpaka vyuo. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi kwamba ushirikiano upo, lakini kwa vile ametoa ushauri, ushauri huo tumeuchukua tunaenda kuufanyia kazi. Kwa maana ya ushirikiano, bado tunaendelea kushirikiana na TAMISEMI kwa sababu vyuo hivi viko kwenye Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chuo cha VETA katika kila Jimbo ili kuwakomboa vijana na tatizo la ajira?

Supplementary Question 8

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Swali langu kwa Mheshimiwa Waziri ni moja tu kwamba: Kwa kuwa mnakwenda kujenga sasa vyuo kwa wilaya zote, ina maana ya mahitaji ya walimu wa ufundi yanakwenda kuongezeka: Mna mpango gani maalum kama Wizara wa kuzalisha walimu wa kwenda kufundisha elimu ya ufundi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nyongo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli ujenzi wa vyuo hivi; vile 25 na hivi 63 na hivi vya mikoa unakwenda kuongeza uhitaji wa walimu kwenye eneo hili. Naomba nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, kwanza tuna chuo chetu ambacho kinafundisha walimu wa masuala haya atakayekwenda kufundisha maeneo haya ya vyuo vya ufundi pale Morogoro. Vile vile, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Nyongo, tunakwenda kufanya maboresho ya mitaala pamoja na sera yetu ya elimu. Tutakwenda ku-convert vyuo vyetu vile vya ualimu tulivyokunavyo zaidi ya 35 ili tuingize component au kada ya ufundi mle ndani ili tuweze kupata hiyo supply ya walimu kwenye maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie vile vile Mheshimiwa Nyongo kwamba, Mheshimiwa Rais tayari alishatoa kibali cha kuajiri watumishi au walimu zaidi ya 571, ambao tunaendelea na mchakato na mpaka kufika sasa walimu 171 tayari tumeshaajiri kwa ajili kuanza kutoa mafunzo kwenye vyuo 25 ambavyo ujenzi wake umekamilika.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.