Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niishukuru Serikali kwa majibu mazuri pamoja na kwamba wananchi walitegemea iwe ni hospitali lakini kwa sababu kwa kuwa Halmashauri imeshakuwa na hospitali haiwezekani kupata hospitali nyingine ya Wilaya.

Je, ni lini fedha hizi ambazo zimetengwa zitakwenda kwa ajili ya utekelezaji kwa sababu mwaka wenyewe ndiyo unaelekea mwisho maana Juni ndiyo mwisho.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba Mheshimiwa Waziri aweze kuongozana nami kipindi hiki ambacho Bunge linaendelea aweze kwenda kuona kituo chenyewe cha afya ambacho tunakizungumzia kwa sababu kina hali mbaya sana. Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Sera ya Afya kwa sasa Halmashauri moja inakuwa na hospitali moja na ndiyo maana Serikali ilileta fedha imejenga Hospitali ya Halmashauri, kwa hiyo, hiki lazima kiendelee kama kituo cha afya. Fedha hizi zitapelekwa ndani ya mwaka wa fedha huu wa 2022/2023 Serikali inatafuta fedha ili kupeleka fedha kwa ajili ya mpango huo wa kukamilisha kituo hicho.

Mheshimiwa Spika, niko tayari kuongozana nae na ningeomba uridhie tuongozane baada ya kuahirisha Bunge hili ili tukapate muda wa kutosha, tufanye ziara hiyo na kufanya majukumu hayo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 2

MHE. DKT CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, aliyekuwa Waziri wa TAMISEMI alituahidi mwaka jana kwamba angetupatia kituo cha afya kwenye Kata ile ya Kirua Vunjo Kusini kwenye Kijiji cha Kohesa. Sijui mtaanza lini kujenga hospitali hiyo kwa sababu tulipata mbadala wa kupata Hospitali ya Wilaya.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi ya Serikali itatekelezwa, ni suala la muda tu kwa hiyo Serikali inatafuta fedha ili kwenda kutekeleza ahadi hiyo kupeleka Kituo cha Afya katika Kata aliyoitaja, ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL S. BARAN: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwa kuwa, Kituo cha Afya cha Gallapo kinahudumia Tarafa nzima ya Babati ikiwemo Kata za Endakiso, Mamire, Qash na Gallapo. Je, ni lini Serikali itajenga nyumba ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Sillo Baran, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nilifanya ziara Babati Vijijini, tulishirikiana sana na Mheshimiwa Mbunge tulifika Kituo cha Afya cha Gallapo, ni kweli kinahitaji muindombinu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali imeweka mpango wa kutafuta fedha kupeleka Gallapo ili kianze ujenzi wa majengo ya Mama na Mtoto na majengo ambayo yanapungua, ahsante sana.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Kata ya Kimala ipo pembezoni sana mwa Wilaya ya Kilolo na hakuna Kituo cha Afya, katika ile Kata barabara hazipitiki wananchi wanaenda katika Kituo cha Afya cha Dabaga.

Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuwajengea Kituo cha Afya katika Kata hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata hii ya Kimala ambayo iko pembezoni tulishaelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kufanya tathmini na kuwasilisha Kata za kipaumbele za kimkakati kwa ajili ya ujenzi wa vituo cha afya. Kwa hiyo, nitoe rai kwa Mkurugenzi kufanya hayo maelekezo ya Serikali na kutuletea, ikiwa ni kipaumbele cha Halmashauri hiyo basi Serikali itaona namna ya kutafuta fedha kushirikiana na mapato ya ndani lakini pia fedha za Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi. Ahsante. (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 5

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kata ya Endago ya Wilaya ya Hanang ina wakazi zaidi ya 5,600 lakini haijawahi kuwa na Kituo cha Afya wala Zahanati. Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya afya katika Kata hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Kata hii ina idadi kubwa ya wananchi zaidi ya 5,000 lakini haina zahanati. Nimhakikishie kwamba tunaweka mpango wa kutafuta fedha kwenda kujenga zahanati katika eneo lile, ikibidi tunaweza tukaona uwezekano wa kujenga Kituo cha Afya baada ya tathmini kuona inakidhi vigezo. Ahsante.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 6

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kituo cha Afya Mtina kilichopo katika Jimbo la Tunduru Kusini kilitegewa shilingi milioni 250 katika bajeti hii ambayo ipo 2022/2023. Je, ni lini Serikali itapeleka pesa hii kwa ajili ya kuboresha huduma ya Mama na Watoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba kwa sababu ipo kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha, naamini kwamba ifikapo Juni 30, fedha zitakuwa zimepelekwa kwa ajili ya ukamilishaji wa miundombinu hiyo. Ahsante.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 7

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wilaya ya Kilindi ina Tarafa Nne, Tarafa Tatu zina vituo vya afya. Je, ni lini Serikali itajenga kituo afya Tarafa ya Kimbe, Kijiji cha Ndegerwa? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omari Kigua Mbunge wa Jimbo la Kilindi kama ifiatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tarafa hii ya Kimbe ambayo haina kituo cha afya tayari ilishawekwa kwenye mpango wa Tarafa za kimkakati, sasa fedha tu inatafutwa ikishapatikana itakwenda kujenga kituo cha afya kwa ajili ya kusogeza huduma kwa wananchi. Ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Supplementary Question 8

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kituo cha Afya cha Negezi na Mwang’alanga ni moja kati ya vituo vya afya ambavyo vimeanza kufanya kazi katika kipindi hiki lakini bado vina mapungufu ya wodi za kawaida za wagonjwa, mapungufu ya mochwari na walk ways. Ni lini Serikali itakwenda kukamilisha vituo hivi vianze kufanya kazi ipasavyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Jimbo la Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Negezi na hivyo vingine ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja ni miongoni mwa vituo ambavyo Serikali imeweka mpango wa kuhakikisha vinakamilishwa kwanza kabla ya kuanza vituo vingine vipya, ndiyo maana katika mwaka uliopita wa fedha na mwaka huu hatujajenga vituo vingi sana vya afya vipya kwa sababu lengo ni kukamilisha kwanza vituo ambavyo vimeanza kwa sehemu ili vitoe huduma kwa upana wake na baadae tuende kwenye vituo vingine.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ipo kwenye kipaumbele. Ahsante. (Makofi)