Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- (a) Je, Serikali itakubali kujenga Hospitali ya Wilaya ya Busokelo hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wametoa eneo tayari na wako tayari kushirikiana na Serikali? (b) Je, kama Serikali inakubali, ni lini kazi hiyo itaanza?

Supplementary Question 1

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza nimpongeze kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia suala la afya kwa Jimbo langu la Busokelo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, je, ni lini hasa hospitali hii itaanza kujengwa ikizingatia kuwa wananchi wa Jimbo la Busokelo pamoja na Mbunge wao tupo tayari kushirikiana na Serikali kujenga hospitali hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na kwamba hizi shilingi bilioni mbili ambazo zimetamkwa kwenye jibu la msingi yalikuwa ni maombi maalum, je, Mheshimiwa Naibu Waziri unaweza ukawathibitishia wananchi wa Jimbo la Busokelo kwamba hizi fedha sasa na maombi yao yamekubaliwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya lini hospitali hii itajengwa, nimesema hapa.
Kwanza mimi naomba niwapongeze hawa Wabunge wote unaowaona humu. Wabunge unaowaona humu jana wamefanya tukio kubwa sana la kupitisha Bajeti ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Bajeti ile sasa inatupa uwezo wa kwenda kutekeleza matatizo ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikwambie sisi Mawaziri tutakuwa serious kuhakikisha kuwa hawa Wabunge kutokana na kelele na juhudi kubwa wanayoifanya tunawahudimia kwa nguvu zetu zote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimueleze Mheshimiwa Mwakibete kwamba kwa sababu pesa imetengwa; na nilikuambia kwamba bajeti ya Serikali hapa imeshapitishwa, na kwamba inafanyiwa kazi; kama swali lako linavyosema fedha hii imetengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya yako. Jukumu letu kubwa sisi sasa ni kuweza kusimamia ili wananchi wako wapate huduma na hatimaye wa- appreciate kwamba wamepata Mbunge kijana wa kuwatumikia. Kwa hiyo ondoa hofu katika hilo.

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- (a) Je, Serikali itakubali kujenga Hospitali ya Wilaya ya Busokelo hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wametoa eneo tayari na wako tayari kushirikiana na Serikali? (b) Je, kama Serikali inakubali, ni lini kazi hiyo itaanza?

Supplementary Question 2

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa vile swali la msingi la Busokelo linafanana na la Wilaya yangu mpya ya Itilima. Kwa vile Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ishatenga eneo la hekari 40 na tayari mipango yote inaendelea. Je, Serikali iko tayari kusaidia baadaye watakapokamilisha mpango huo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, wameshatenga eneo ekari 40, Serikali inasemaje katika hili? Serikali inachokisema ni kwamba mkimaliza mipango yenu wekeni katika Mpango wa Bajeti ya 2017/2018 kama kipaumbele cha ujenzi wa hospitali. Na ninaomba nikwambie itakapofika katika mchakato huu wa bajeti, kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa sababu sera yetu kubwa ni kujenga hospitali kila Halmashauri badala hata ya kujenga Hospitali kila Wilaya. Kwa hiyo kwa huu mpango mkiuanza sisi kazi yetu ni kusukuma tu.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba uondoe hofu, ni kwamba wekeni katika mpango, nia yetu ndani ya miaka mitano watu waone kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuleta mabadiliko katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- (a) Je, Serikali itakubali kujenga Hospitali ya Wilaya ya Busokelo hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wametoa eneo tayari na wako tayari kushirikiana na Serikali? (b) Je, kama Serikali inakubali, ni lini kazi hiyo itaanza?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya kiafya yanayoikabili Wilaya ya Busokelo yanafanana na Wilaya ya Karagwe, haina Hospitali ya Wilaya, inayo Hospitali Teule ya Nyakahanga inayotoa huduma za tiba kwa Wilaya mbili, Karagwe na Kyerwa. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ili kuboresha huduma za afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Karagwe hawana hospitali, lakini naomba niwapongeze kwamba wanafanya juhudi kubwa na ndiyo maana pale tumempeleka kijana mmoja anaitwa Dkt. Sobo, daktari mzuri sana wa upasuaji kama DMO. Ni kweli changamoto hizi, ninapata taarifa kutoka kule kila siku kwamba hakuna Hospitali ya Wilaya. Maeneo haya ni miongoni mwa maeneo tuyoyawekea kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tunajua kwamba kule mnatengeneza kikosi kazi cha kuweza kuhudumia maeneo yale, naomba katika bajeti ya mwaka unaokuja sasa wekeni kipaumbele chenu ili tuhakikishe sasa Karagwe badala ya kutumia hospitali ya DDH, tutumie Hospitali zetu za Wilaya kwa kuhakikisha kwamba tunaweka nguvu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba, ikiwezekana kama kuna kituo cha afya ambacho mnatumia pale kipewe nguvu ili baadaye kipandishwe kuwa hata Hospitali ya Wilaya kwa kuanzia linaweza likawa jambo jema. Lakini naomba nikwambie kwamba, Serikali itaunga mkono juhudi zote za wana-Karagwe na watu wa Mkoa wa Kagera.

Name

Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- (a) Je, Serikali itakubali kujenga Hospitali ya Wilaya ya Busokelo hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wametoa eneo tayari na wako tayari kushirikiana na Serikali? (b) Je, kama Serikali inakubali, ni lini kazi hiyo itaanza?

Supplementary Question 4

MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa matatizo ya Busokelo yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini, na kwa kuwa, wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini tumeanzisha kwa nguvu zetu wenyewe ujenzi wa Hospitali ya Wilaya toka mwaka 2007, na mapato ya Halmashauri ni kidogo, Halmashauri imekuwa ikijenga kidogo kidogo kwa kushirikiana na wananchi wake, lakini ukamilishaji wa hospitali hii umekuwa ni mgumu.
Je, Serikali iko tayari sasa kuipa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini ombi maalum la fedha ilizoomba kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali hii?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Azza nakumbuka mwaka 2015 alitaka kushika shilingi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, kuhusiana na suala zima la mambo ya maendeleo katika Mkoa wa Shinyanga. Na nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba mwaka huu ulikuwa na kilio kikubwa sana cha suala zima la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Shinyanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba, Serikali imesikia kilio hiki, tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo. Lengo kubwa ni kwamba, juhudi unazozifanya kwa wana-Shinyanga, kama Mbunge wao wa Viti Maalum, naomba niseme tutakuunga mkono.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninakumbuka kuna lile ombi maalum Serikali imesikia hili. Jambo kubwa ni kwamba, tushikamane kwa pamoja tukusanye mapato, Serikali iwe na nguvu, miradi tuliyoipanga na maombi tuliyoyapeleka yote yaweze kufanikiwa.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Azza ondoa hofu, Serikali yako, na mimi mweyewe niseme na Waziri wangu mwenye dhamana, tuko tayari kuhakikisha kwamba Wanashinyanga wanapata huduma bora ya afya katika eneo lao.