Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini mfumo wa utawala wa Serikali za Mitaa utaanza kufanya kazi katika Kambi za Wakimbizi Mishamo?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa kumekuwa na mkanganyiko wa kutoa huduma za kijamii kwenye eneo ambalo lina utawala wa aina mbili, Ofisi ya Mambo ya Ndani na Ofisi ya TAMISEMI na wanaotoa fedha ni TAMISEMI. Je, mkanganyiko huu ni lini Serikali itakwenda kuuondoa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Umoja wa Mataifa ulijitoa kuhudumia kambi za wakimbizi na kukabidhi Serikali na Serikali ikatoa uraia. Tunavyozungumza leo hii eneo la utawala kata tayari kuna madiwani ambao wanafanya shughuli za kiutawala lakini eneo la Serikali za vijiji hakuna utawala wa aina yoyote. Ni lini mtakaa na Wizara ya Mambo ya Ndani ili muondoe sintofahamu ambayo ipo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkanganyiko ambao umetokana na vijiji hivi kuwa chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Ofisi ya Rais TAMISEMI kimsingi tunaendelea kuiweka sawa; na ndiyo maana siku za nyuma hatukuwa na madiwani katika zile kata nne lakini mwaka 2020 madiwani walichaguliwa. Pia kuna watendaji wa vijiji ambao siku za nyuma hawakuwepo; na linaloendelea sasa ni utaratibu tu wa ndani ya Serikali kuongea kati ya Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ili tuweze kukubaliana mfumo mzuri zaidi wa kuendesha vijiji hivyo.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakaa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuondoa changamoto ambayo ipo kwa sasa, ahsante.