Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Mji Mdogo wa Mbalizi uliomo kwenye Halmashauri ya Mbeya ni kati ya miji inayokua kwa kasi sana lakini inakosa miundombinu muhimu na uhaba na maji pia. (a) Je, ni lini Mji huo utapewa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji? (b) Je, ni lini Serikali itatatua tatizo kubwa la maji kwenye Mji huo? (c)Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata zilizo ndani ya Mji wa Mbalizi?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.
Kwa kuwa Waziri amepotoshwa kwenye jibu (b) sehemu ya kwanza ya swali langu na hivyo kuwapotosha wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi na pia kulipotosha Bunge; je, Waziri atachukua hatua gani kwa Afisa huyo aliyempotosha?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ndani ya Mji Mdogo wa Mbalizi kuna ardhi ya zaidi ya ekari 5,000 iliyokuwa Tanganyika Packers, na haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 sasa na kwa kuwa Halmashauri ya Mbeya imetenga eneo mahsusi kwa kunenepesha mfugo na kwa ajili ya kiwanda cha nyama, je, ni lini Serikali itarudisha ardhi hiyo kwa Halmasahuri ya Mbeya kwa madhumuni ya makazi bora na huduma za jamii? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Sasa naomba nitoe msisitizo katika eneo la kwanza ni kwamba Ofisi ya Rais - TAMISEMI tunapofanya hizi kazi tunahakikisha kwamba coordination inakamilika vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kama unaona kwamba kuna mapungufu, naomba u-clarify ni eneo gani ambalo linaonekana halijakuwa sawasawa, ili mimi kama Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI nijue kwamba eneo gani ambalo halikukaa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la opotoshaji limekuwa la jumla, lakini hili tulilielekeza katika ofisi zote za mikoa, kwamba ma-RAS wote wako responsible katika majibu yote yanayojibiwa na TAMISEMI. Kwa hiyo, nilitaka angalau ungenipa ufafanuzi ni eneo gani uliona kwamba lilikuwa na mapungufu tuweze kulifanyia kazi kubwa, kwa sababu lengo kubwa ni kujenga, kwamba ni jinsi gani majibu yawe sawasawa kwa ajili ya kuboresha mahitaji ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika eneo la piliā€¦
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri amesema hivi swali lake kipengele (b) hakijajibiwa kabisa kwa maana hiyo, kwa sababu umepotoshwa majibu ya kipengele chote.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kuhusu swali la ni lini Serikali itarudisha eneo hili kwa ajili ya wananchi, mimi nilifika pale Mbeya nilipokwenda kutembelea Iyunga lakini nikafika katika Jimbo la Mheshimiwa. Mimi naipongeza Serikali kwa sababu kuna juhudi kubwa imefanyika, sasa pale kuna machinjio ya kisasa kwa ajili ya uchinjaji wa nyama tena wa kisasa katika eneo hilo la Mbeya. Lakini kwamba kuna eneo kubwa sasa eneo hili jinsi gani litafanyiwa kutwaliwa kurudishwa kwa wananchi kwa ajili ya makazi, nadhani sasa jambo hili ni jambo la mchakato, si jambo la kutoa maelekezo tu hapa, nini kifanyike haraka haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu lazima tufanye tathimini ni kitu gani kilichokuwepo hapo, kwa sababu inawezekana ukienda ndani kuna migogoro mingine ya ziada. Kwa hiyo, naomba niseme kwamba hilo ni suala zima la mchakato, naamini kwamba Baraza la Madiwani likikaa litafanya maamuzi litapeleka mapendekezo halafu vyombo husika vitakuja kufanya tathimini. Vitakaporidhika TAMISEMI - Ofisi ya Ardhi tutafanya tathimini ya kinakuona kama eneo hilo linaweza likarudishwa kwa ajili ya maslahi ya wananchi ili wananchi wapate huduma ambayo inahitajika katika maeneo yao.

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Mji Mdogo wa Mbalizi uliomo kwenye Halmashauri ya Mbeya ni kati ya miji inayokua kwa kasi sana lakini inakosa miundombinu muhimu na uhaba na maji pia. (a) Je, ni lini Mji huo utapewa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji? (b) Je, ni lini Serikali itatatua tatizo kubwa la maji kwenye Mji huo? (c)Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata zilizo ndani ya Mji wa Mbalizi?

Supplementary Question 2

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto zilizoko wenye Mji Mdogo wa Mbalizi unafanana kabisa na changamoto zinazopatika kwenye Mji Mdogo wa Namanyere ambao pia ni Makao Makuu ya Wilaya ya Nkasi. Mamlaka hii ya Mji Mdogo wa Namanyere inahudumiwa na Mamlaka Ndogo ya Mji wa Namanyere. Mamlaka hii imeshindwa kuhudumia Mji huu kutokana na kupanuka zaidi kwa Mji wenyewe. Na kwa kuliangalia hilo Halmashauri imeshapitisha katika vikao vyake maombi ya kupata mamlaka ya Mji wa Namanyere. Je, ni lini Serikali itazingatia maombi haya ili kukidhi huduma zinazohitajika sana kwenye Mji huu wa Namanyere? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia ombi hili. Mheshimiwa Mbunge alifika ofisini kwangu na walinisaidia sana kuandaa database ya kuangalia maombi yote ya Miji Midogo katika Halmashauri zote za Miji mipya na Halmashauri ya Mkoa. Tunachokifanya hivi sasa ni kwamba wataalam katika Ofisi ya Rais - TAMISEMI wataenda katika maeneo mbalimbali; na nilishasema mara kadhaa; baada ya kupata ile database, kujua nani wamefikia hatua gani, waliokidhi vigezo, na ambao hawajakidhi vigezo. Hivi tutavipata hasa baada ya wataalamu kufika site.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mipata, naomba nikuhakikishie kwamba, watu wetu watafika Namanyere, watafika maeneo ya yote Sumbawanga na maeneo yale yote ambako kuna matatizo haya ya wananchi kutaka maeneo yao aidha yawe Miji Midogo, kupata Halmashauri mpya, au kupata Wilaya mpya. Wataalam wakishakamilisha lile zoezi tutakavyoangalia, pale vigezo vitakapokuwa vimefikiwa naamini Ofisi ya Rais - TAMISEMI haitosita kuipa mamlaka hii kuwa Mji Mdogo rasmi.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Mji Mdogo wa Mbalizi uliomo kwenye Halmashauri ya Mbeya ni kati ya miji inayokua kwa kasi sana lakini inakosa miundombinu muhimu na uhaba na maji pia. (a) Je, ni lini Mji huo utapewa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji? (b) Je, ni lini Serikali itatatua tatizo kubwa la maji kwenye Mji huo? (c)Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata zilizo ndani ya Mji wa Mbalizi?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kutuangalia sisi kambi mbadala.
Mheshimiwa Naibu Spika, kituo cha afya cha Lupilo ndiyo kama Hospitali ya rufaa katika kata tano za Ilagua, Lupilo, Kichangani na Milola. Je, ni lini serikali itaifanyia ukarabati kituo hiki cha afya maana kina hali mbaya ya majengo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze kwa sababu ni kweli kwamba Mbunge amekuja amejipanga kweli katika Bunge hili na mimi naomba nikuhakikishie, naelewa wazi kwamba ukarabati unaanza pale Baraza la Madiwani linapoweka vipaumbele. Na mimi nilivyopitia katika database wakati wa mchakato wa bajeti ya mwaka huu niligundua kwamba hata eneo lako la Ulanga ni kweli kuna mahitaji, isipokuwa tatizo kubwa lilikuwa katika budget ceiling.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kikubwa zaidi naomba nikuhakikishie, ni kwamba sasa hivi ukiwasiliana na Mkurugenzi wako; kama nilivyosema siku mbili zilizopita hapa; kwamba tumewaagiza wabainishe magofu yote na maeneo yote katika eneo la afya yanayotakiwa kufanyiwa ukarabati ili Ofisi ya Rais - TAMISEMI tuangali tunapeleka wapi nguvu. Katika hilo naamini kwamba eneo lako la Ulanga katika kituo hicho cha afya ni miongoni mwa takwimu ambazo zitakuja tuweze kuzifanyia kazi. Na nikuhakikishie kwamba zitakapofika ofisini kwetu tutapanga mpango mkakati kuweza kukusaidia ili uendelee kuleta heshima katika Jimbo la Ulanga kama ilivyokuwa toka zamani.