Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Mbarali na kuwa na Halmashauri mbili ili kusogeza huduma karibu na wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu maziuri ya Mheshimiwa Waziri, na ya kueleweka nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa mchakato wa huu ni mrefu, je, Serikali itakubaliana nami kwamba kuna ulazima wa kuongeza vyombo vya usafiri katika Halmashauri ya Mbarali, hasa kwenye sekta ya elimu, afya, TASAF na kadhalika ili waweze kuwahudumia wananchi kikamilifu?

Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa TARURA ipo chini ya TAMISEMI, je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kuwa kuna ulazima wa kuhamasisha hii TARURA sasa ikarabati zote zilizoharibiwa na mvua kubwa iliyokuwa inanyesha kipindi kilichopita, ili wananchi waweze kupata huduma za kijamii kwa urahisi na pia kusafirisha mazao yao?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Leornard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza ni kuhusu usafiri. Nimhakikishie tu kwamba Ofisi ya Rais TAMISEMI tumeshaanza huo mchakato. Mwaka jana tuligawa magari, kwa maafisa elimu sekondari, na mwaka huu vilevile tumeshaagiza magari mengine 184 kwa ajili ya maafisa elimu wa shule za msingi ambayo tumeshapata awamu ya kwanza 35 na mengine yanakuja, lakini yote yameshalipiwa.

Mheshimiwa Spika, vivyo hivyo tunatoa magari kwa ajili ya wahandisi wa TARURA wa halmashauri, lakini vilevile tutapeleka ambulance katika halmashauri zote nchini ambazo zina hospitali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, jukumu hili la kusadia Halmashauri nchini ikiwemo ya Mbarali lipo katika utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, la pili, kuhusu kumalizia ukarabati wa barabara za TARURA, tumelichukua hilo katika bajeti yetu na kwamba tutahakikisha kwamba zinajengwa kulingana na mahitaji. Ahsante sana.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Mbarali na kuwa na Halmashauri mbili ili kusogeza huduma karibu na wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo tangu mwaka 2017, ilipitia taratibu na vigezo vyote vya kuweza kugawa jimbo. Lakini changamoto iliyorudishwa ni Kamba kuna idadi ndogo ya watu. Je, Serikali itakuwa tayari kuigawa hii halmashauri, baada ya sensa ya mwaka huu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Halmashauri ya Kilolo, ilikuwa imekidhi vigezo vingine isipokuwa ya idadi ya watu; na kinachosubiriwa ni kujua hiyo idadi watu. Mimi ninaamini kwamba kama vigezo vitafikiwa basi mapendekezo yatapelekwa huko mbele na mamlaka husika italiangalia. Kwa hiyo, tusubiri vigezo vikishakuwa vimekamilika, basi hatua hiyo inaweza kukubalika baadaye. Ahsante sana.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Mbarali na kuwa na Halmashauri mbili ili kusogeza huduma karibu na wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ni lini sasa Serikali italigawa Jimbo la Sumbawanga Vijijini ambalo hata Mwenyezi Mungu aliligawa kati kati, Ufipa wa Chini kata 13 na Ufipa wa Juu kata 14. Sasa ni lini Serikali italigawa jimbo hilo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Rukwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilijibu katika swali la msingi, ni kwamba wafuate tu utaratibu na sisi tutazingatia endapo hizo halmashauri zimetimiza vigezo vyao, na baada ya hapo maana yake sisi tutapeleka katika mamlaka husika kwa ajili ya maamuzi. Kwa hiyo, kikubwa tu waanze mchakato halafu mamlaka husika italiangalia hilo. Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Mbarali na kuwa na Halmashauri mbili ili kusogeza huduma karibu na wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa uamuzi wa mwisho wa Serikali kugawa halmashauri, wilaya na mikoa ulifanyika mwaka 2012, takribani miaka kumi iliyopita, na kwa kuwa maeneo mengi sasa hivi yana sifa kabisa za kugawiwa, mfano Mkoa wa Tabora, Morogoro, Tanga na mikoa mingine mikubwa na baadhi ya wilaya ambazo ni kubwa kama Sikonge na Mbeya.

Je, maamuzi mengine ya Serikali tuyategemee lini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephat Kakunda, Mbunge wa Jimbo la Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Kwamba Serikali ilifanya maamuzi ya mwisho, mwaka 2012, na muda ambao umepita mpaka sasa hivi ni miaka kumi na bado Serikali inapitia na kutathmini kuona haja ya kuongeza endapo maeneo ya utawala, ama tuendelee na sasa ili tuendelee kuyaboresha na kuwa bora. Kwa hiyo, naamini kabisa Serikali uamuzi wake mpaka sasa hivi upo sahihi na bado tunazingatia; na siyo kwamba mwaka 2012 ndiyo ilikuwa mara ya mwisho. Bado huo mchakato utaendelea baada ya kuona mahitaji ya wakati wa sasa. Ahsante.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Mbarali na kuwa na Halmashauri mbili ili kusogeza huduma karibu na wananchi?

Supplementary Question 5

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa Wilaya ya Tunduru ilianzishwa mwaka 1905 na mpaka leo bado ni kubwa kulinganisha na wilaya zingine; na kwa kuwa vikao vyote vinavyohusu kugawa halmashauri ile limefanyika mpaka ngazi ya mkoa; na kwa kuwa Tunduru Kusini ndilo jimbo ambalo linaathirika sana kwa kutokuwa na halmashauri. Je, Serikali itaanzisha lini halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Kusini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Idd Mpakate, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika jibu la msingi, kwamba halmashauri ambazo zimeshamaliza mchakato, bado Serikali inaendelea kupitia vigezo na kutathimini, ili kuona kama haja ya kutangaza kwa wakati uliopo ama tuendelee kuboresha zile halmashauri ambazo ni changa. Kwa hiyo jambo hilo lipo katika ofisi zetu na wasubiri wakati ambapo itakuwa tayari kufanya hivyo, tutafanya hivyo.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Mbarali na kuwa na Halmashauri mbili ili kusogeza huduma karibu na wananchi?

Supplementary Question 6

MHE. FURAHA MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ni kusogeza huduma kwa wananchi. Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya tarafa katika Wilaya ya Nyamagana na Ilemela kwa kuwa zina kata zaidi ya kumi na tano na zina tarafa moja moja?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuongeza maeneo ya utawala ni moja ya jukumu la Serikali ambalo tumekuwa tukilifana mahali ambapo pana vigezo vyote. Kwa hiyo, kama kunakuwa na eneo halina vigezo maana yake tunakuwa hatuna hiyo fursa ya kuongeza. Kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Furaha Matondo kwamba endapo maeneo hayo yaliyoainishwa yakifuata taratibu zote na zikafika katika Serikali Kuu, basi Serikali itazingatia kulinga na vigezo vilivyowekwa kikatiba. Ahsante.