Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITHA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja la Ugalla lililopo katika Kata ya Ugalla?

Supplementary Question 1

MHE: RITHA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, upembuzi yakinifu wa daraja hilo umeshafanyika na wananchi wa Nsimbo wanataka kujua. Je, katika bajeti hii daraja hilo litajengwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili. Barabara ya kutoka Kayenze mpaka Kaliua ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Kabati ambayo ameuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Anna Richard Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo ambaye amekuwa anafuatilia sana ujenzi wa barabara hii. Daraja la Ugalla kama nilivyosema katika jibu la msingi lina urefu wa mita 150 lakini linaunganishwa na madaraja mengine saidizi makubwa zaidi ya matano na makalavati zaidi ya tisa makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi Serikali imeanza kuyajenga madaraja hayo saidizi ili tuweze kulifikia hilo daraja kubwa. Kwa hiyo, tayari Serikali imeshaanza kujenga hayo madaraja saidizi na makalavati. Kuhusu ujenzi kwa kiwango cha lami kuanzia eneo la Kawajenzi ambapo ni Mpanda Mjini kupita hilo Daraja la Ugalla hadi Kaliua ujenzi huo utaanza baada ya kukamilisha kuifungua hiyo barabara.

Mheshimiwa Spika, hii barabara ni barabara mpya ambayo inapita katika Mbuga ya Kaliua, upande wa Mkoa wa Katavi tumeshafungua mpaka kwenye daraja lakini upande wa Tabora kwa maana ya kutoka Ugala hadi Kaliua bado tunaendelea kuifungua. Kwa hiyo, baada ya kuifungua tutatafuta fedha kuijenga barabara hiyo sasa kwa kiwango cha lami. Ahsante.