Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi 40,000 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kama ilivyopitishwa katika Bajeti wa mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa majibu ya Serikali. Swali langu la msingi liliuliza kada zote hadi sasa kada za watendaji wa kata, vijiji na mitaa hazijapata kibali. Halmashauri ya Mji wa Mbulu ina upungufu wa watendaji wa kata, vijiji na mitaa zaidi ya 70, ni miaka mitatu sasa.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuajiri watumishi hawa katika Halmashauri wa Mji wa Mbulu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa waalimu wa sayansi katika mgawo wa ajira mbili zilizopita za Serikali hawakupatikana katika Halmashauri wa Mji wa Mbulu kwa kigezo cha kuona waalimu wa sanaa ni wengi na wanafunzi wameendelea kukosa masomo ya sayansi. Je, Serikali ina mkakati gani au inakusudia kugawa walimu wangapi wa sayansi katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kada ambazo hazijatangazwa kwa maana ya watendaji wa kata wa vijiji na mitaa lakini na kada nyingine zote zitaendelea kutangazwa kwa awamu kwa sasa tumeanza na sekta ya afya na elimu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge lengo la Serikali ni kuhakikisha kada hizo nyingine pia zinaajiriwa. Lakini pamoja na hiyo bado halmashauri zimeendelea kuajiri watendaji kupitia mapato ya ndani, baadhi ya halmashauri wataendelea kufanya hivyo kwa vibali vya Serikali Kuu pia kupitia Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na walimu wa sayansi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika ajira hizi ambazo tayari zimetangazwa za walimu 9800 tutaenda kuhakikisha tunapeleka walimu wa sayansi katika maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi wa walimu wa sayansi. Kwa tathmini hiyo tumeshaifanya na tutampa kipaumbele katika Jimbo lake la Mbulu Mjini, ahsante.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwa swali hili zuri sana la nyongeza lililoulizwa na Mheshimiwa Mbunge, kwanza naomba kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, kwa kibali ambacho Mheshimiwa Rais amekitoa cha kuhakikisha tunatoa ajira 32,604 ambazo zilipangwa kwenye bajeti ya mwaka 2021/2022, baada ya kutoa ajira zile za kipaumbele kwenye sekta ya afya, sekta ya elimu na sekta zile nyingine ambatanishi. Mheshimiwa Rais kupitia ofisi yetu ameridhia sasa kada zile nyingine za watumishi zilizobakia ikiwemo hao watendaji wa vijiji na kata ziweze kufanyiwa mgao kwenye ajira 7,792 ambapo bado hizo zinasimamiwa na Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba waajiri wote nchini wahakikishe tu wanapanga majukumu sahihi kwa watumishi wote wapya watakaoajiriwa ili waweze kuongeza tija na kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi 40,000 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kama ilivyopitishwa katika Bajeti wa mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pia kuna kada kama za Maafisa Ugani wa Mifugo hawajaajiriwa kwa muda mrefu: -

Je, Serikali katika mwaka huu fedha itatoa ajira hiyo? Ahsante.

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, kama nilivyosema toka mwanzo, tunaendelea kuangalia ikama ya Utumishi kwa kuzingatia misingi ya ugawaji wa watumishi katika sekta zote ili kuondoa uhaba wa watumishi nchini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa sasa tunachokifanya, tunaendelea kupokea maombi kwa Mawaziri, kwenye sekta zao na kwa kuangalia ni kwa namna gani upungufu na uhitaji uliopo kwa zile nafasi ambazo tumeshazigawa. Kwa zile ambazo hatujazigawa mpaka sasa, hao watumishi 7,792 niliowasema, tutaendelea kuzingatia mahitaji ya watumishi nchini na kuhakikisha kwamba utendaji wa kazi Serikali kwa kupitia Utumishi wa Umma unaendelea kuwa na usawa kwa kuzingatia mahitaji halisi. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi 40,000 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kama ilivyopitishwa katika Bajeti wa mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini lina uhaba mkubwa wa Afisa Maendeleo ya Jamii pamoja na Walimu wa Sayansi: -

Je, katika mgao huu ukoje? Mtaangalia majimbo haya ya vijijini ili kuweka mgao sawa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kujibu kwenye jibu langu la msingi, kwamba katika ajira ambazo hivi sasa zinaendelea na utaratibu wa kuajiri, tumeshaainisha maeneo yenye upungufu mkubwa wa wataalamu; wataalamu wa maendeleo ya jamii na pia wataalamu kwa maana ya Walimu wa Sayansi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kufuatia tathmini ile, tutahakikisha tunatoa kipaumbele katika maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi ikiwemo katika Jimbo la Mbulu Vijijini. Ahsante.