Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. SAPUTU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Wagonjwa wa Nje, Jengo X-Ray, Jengo la Watoto na Jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya Olturumet Halmashauri ya Arusha?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. SAPUTU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza maswali mawili. Kwa kuwa ujenzi wa hospitalli hii na upanuzi wake ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa muda mrefu sasa na haikuweza kutekelezwa.

Je, nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibi ambao wanategemea hospitali hiyo kwa asilimia kubwa na haijajengwa mpaka sasa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kutembelea hospitali hiyo ili ajionee hali halisi ya wagonjwa walivyo wengi na upanuzi wa hospitali hiyo haikuweza kufanyika kwa muda mrefu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeza sana Mheshimiwa Noah Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi kwa namna ambavyo anawasemea kwa dhati wananchi wa jimbo lake. Nimhakikishie kwamba Ofisi ya Rais – TAMISEMI itaendelea kushirikiana naye kuhakikisha wananchi wanapata matunda ya Serikali yao sikivu.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na ahadi ya Mheshimiwa Rais, ni kwamba ahadi za viongozi wetu wakuu wa nchi ni maelekezo, na ndiyo nimemuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye mwaka ujao wa fedha 2022/2023 tutatafuta fedha ili tuweze kuanza utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais katika ukarabati hii ya Arumeru.

Mheshimiwa Spika, pili, nipo tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge, tutakubaliana hili baada ya Bunge twende tukaitembelee hospitali hiyo.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. SAPUTU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Wagonjwa wa Nje, Jengo X-Ray, Jengo la Watoto na Jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya Olturumet Halmashauri ya Arusha?

Supplementary Question 2

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kituo cha afya cha Mtimbila kina x-ray lakini hakina jengo la x-ray wala hakina mhudumu wa x-ray. Je, ni lini Serikali itaenda kujenga hilo jengo na hatimaye kupeleka mhudumu ili watu wapate huduma hizo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aleksia Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba vituo vyetu vya afya ambavyo havina miundombinu ya majengo yanayostahili kuwepo, ikiwemo majengo ya x-ray ni kipaumbele cha Serikali kujenga majengo yale. Kwa hiyo, tutahakikisha kwa sababu tayari kuna x-ray machine katika kituo hiki lakini hatuna jengo, tutaweka kipaumbele ili tuanze ujenzi wa jengo hilo kupitia mapato ya ndani lakini pia tutatafuta fedha Serikali Kuu.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. SAPUTU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Wagonjwa wa Nje, Jengo X-Ray, Jengo la Watoto na Jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya Olturumet Halmashauri ya Arusha?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Zahanati ya Kata ya Lumuli ambayo iko katika Jimbo la Kalenga, ziko mbili. Katika Zahanati hizi, wananchi walishapaua na wameshajenga majengo yako vizuri lakini hakuna samani, vitendanishi na vifaa tiba, ni lini Serikali itapelekea hivyo vitu ili wananchi waweze kupata huduma ya afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze sana wananchi wa Iringa kwa kujenga zahanati hizi na kuzikamilisha. sasa niseme, kwamba vifaa tiba vinavyohitajika katika ngazi ya zahanati, gharama yake siyo kubwa sana ni imani yangu kwamba mkurugenzi wa halmashauri husika, wana uwezo wa kutenga kati ya ile asilimia 40 na 60 kununua vifaa tiba hivi. Kwa hiyo, naelekeza halmashauri, wakurugenzi watenge fedha, wanunue vifaa tiba zahanati hizi zisajiliwe ziweze kutoa huduma ahsante.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NOAH L. SAPUTU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Wagonjwa wa Nje, Jengo X-Ray, Jengo la Watoto na Jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya Olturumet Halmashauri ya Arusha?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Swali langu, ni lini Serikali itatathimini upya uhitaji wa eneo la zaidi ya eka 35, 30 ili kujenga hospitali za wilaya. Ni sehemu zipi utapata eneo kubwa kiasi hicho, kwanini tusitafute namna ya kujenga hizi hospitali hata kuweka ghorofa moja moja badala ya kutafuta eneo kubwa kiasi hicho?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI katika ujenzi wa hospitali za halmashauri yako ya aina mbili. Kuna maelekezo ambayo yanaendana na halmashauri za vijijini, ambako ardhi ni kubwa wanahitaji kutenga angalau ekari 30 na kuendelea kwa sababu hospitali zile tunazojenga tunatazama miaka 50 au mia moja ijayo, haituangalii miaka mitano au kumi ijayo. Kwa hiyo, tunahitaji kuwekeza katika maeneo makubwa ili hata baada ya miaka 100 miundombinu tu itabadilika lakini eneo litaweza kutosheleza.

Mheshimiwa Spika, kwa maeneo ya mijini tunaweka eneo siyo kubwa sana, inategemeana na eneo, lakini tunapendekeza kujenga majengo ya kwenda juu kwa maana ya maghorofa. Kwa hiyo, maeneo yote mawili yametazamwa, maeneo ya mijini, tunakwenda kwa maghorofa, kama eneo halitoshi lakini maeneo ya vijijini tunataka angalau eka 30 kwa sababu tunaona miaka mingi ijayo.