Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa yasiyoambukiza?

Supplementary Question 1

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jawabu zuri la Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; Magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza kwa kweli yanaongezeka kila uchao. Kwa mfano, kuanzia mwaka 2016 kulikuwa na wagonjwa takribani milioni nne na kumi na nane elfu, lakini kufika mwaka 2020 kumekuwa na wagonjwa wasiopungua milioni nne na laki nane. Magonjwa haya yanagharimu Serikali kupitia Wizara ya Afya takribani asilimia 20 ya bajeti yake na vifo takribani asilimia 33 ya vifo vyote. Je, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba, wakati sasa umefika magonjwa haya kuyaundia Tume Maalum ambayo itayashughulikia kama vile TACAIDS?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; miongoni mwa magonjwa haya yasiyoambukiza ni saratani ambayo nayo inaua watu wengi sana na pia inagharimu pesa nyingi sana kwa kuagiza dawa kutoka nje. Je, Waziri haoni wakati sasa umefika wa kuwa na kiwanda ambacho kitazalisha mionzi tiba?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumjibu swali lake la kwanza Mheshimiwa Mbunge anashauri kwamba tuanzishe tume kama ya TACAIDS kwa sababu magonjwa haya yanaonesha kila mwaka yanaongezeka na yanakuwa ni tatizo kubwa kwenye nchi yetu. Tutalifanyia upembuzi yakinifu wazo lake, lakini kikubwa ni kwamba ni sisi kuongeza nguvu zaidi kwenye kuelimishana hasa haya magonjwa yasiyoambukiza, namna life style na mambo mengine ili kupunguza idadi ya watu ambao wanapata matatizo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuongeza bajeti na kubwa zaidi kwenye eneo hili ili elimu iwafikie watu wengi lakini watu wengi zaidi wapate huduma bila bughudha yoyote. Maana yake ukianzisha taasisi wakati mwingine tunarudi kule kule, fedha nyingi zinaishia kwenye masuala ya utawala badala ya kumfikia mgonjwa husika. Kwa hiyo nafikiri ni kuongeza nguvu katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ambalo kimsingi linaonyesha ni namna gani Serikali ilivyo serious kwenye eneo hili, ni suala alilosema kwamba kiwanda cha kutengeneza mionzi dawa. Kiwanda cha kutengeneza mionzi dawa kama tulivyosema hapa kwa Afrika ni nchi nne tu zilikuwa na uwezo na kiwanda hicho na sasa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan ndani ya mwaka mmoja amewezesha na tayari hicho kiwanda kipo na mwezi wa sita kinaenda kuanza kazi rasmi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi na ukiangalia maana yake ni nini? Sisi kwa Afrika sasa Rais wetu ametufikisha mahali, katika nchi tano ambazo zina kiwanda cha kuzalisha mionzi dawa na sisi tuko. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nafikiri eneo hilo linaenda vizuri na hatuna haja ya kutengeneza taasisi. Unajua watu wetu kwenye masuala ya utawala fedha nyingi badala ya kwenda kwa mgonjwa zinaweza zikaishia kwenye masuala ya utawala.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa yasiyoambukiza?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Nataka kufahamu nini mkakati wa Serikali wa kupeleka dawa za magonjwa yasiyoambukiza katika ngazi ya zahanati?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali moja ilikuwa ni kupatikana vile vitu ambavyo huduma hiyo inaweza ikafanyika na mmeona sasa hivi kwamba karibia kila jimbo kila mahali kuna ujenzi unaoendelea kwa ujenzi wa vituo vya afya, zahanati na mambo mengine. Kikubwa sasa hivi na kwa ajira iliyopo sasa hivi utaona sasa hivi Madaktari wenye level ya digrii sasa hivi wameshafikishwa mpaka vituo vya afya na dawa hizo zinaenda kutolewa kwa ukaribu zaidi. Kwa hiyo Serikali ina mkakati kuwa, tunapomaliza hivi vituo wakati tunaweka vifaa, tunaweka madawa, lakini wataalam watapelekwa wenye uwezo wa kuwatibu watu wenye matatizo hayo.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa yasiyoambukiza?

Supplementary Question 3

MHE. FAHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa maradhi yasiyoambukiza kama sukari na presha, ushatumia dawa kwa muda mrefu au uliugua kwa muda mrefu, lakini kila ukienda kupima inaonekana normal kwa sababu unatumia dawa kwa wakati. Je, inaweza kupunguza dawa kutumia ili niepushe kupata maradhi mengine wakati tayari maradhi haya yako normal?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge ambalo ni lizuri. Nafikiri nisingetoa ushauri wa kijumla kwa sababu kila mtu anakuwa na hali halisi anapofika kwa Daktari. Nashauri jambo lolote unalotaka kufanya inapofikia mahali una shida ya presha au sukari, usiamue kijumlajumla, amua baada ya kufika kituo cha afya, kupewa vipimo na Daktari mwenyewe kwenye eneo hilo na kukushauri.