Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za Afya kwa Wazee hasa wa Mkoa wa Arusha kwa kuwapatia dawa kupitia mfumo wa bima tofauti na iliyopo sasa?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu hayo ya Serikali lakini bado kuna changamoto kubwa sana ya wazee kupata huduma ya afya kwenye vituo vyetu vya afya, hususan hospitali zetu za rufaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niiombe Serikali kuna changamoto kubwa sana, umefika wakati wa kutoa tamko rasmi kabisa kwamba wazee hawa watibiwe bure na ikionekana kuna changamoto yoyote kwenye hiyo hospitali hatua zichukuliwe mapema.

Je, Serikali inatoa tamko gani sasa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge ameielezea vizuri na tunapokea ushauri wake, Waziri wa Afya kwa kushirikiana na Waziri wa TAMISEMI, watatoa maelekezo mahususi kwa maandishi kwa ajili ya hilo kutekelezwa kama inavyotakiwa. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za Afya kwa Wazee hasa wa Mkoa wa Arusha kwa kuwapatia dawa kupitia mfumo wa bima tofauti na iliyopo sasa?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Tatizo la huduma bure kwa wazee, akina Mama na Watoto limekuwa ni changamoto kubwa sana katika nchi yetu, na kwa kuwa wote tulioko hapa ni wazee watarajiwa leo, kesho, keshokutwa na mtondo go.

Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka wa kutoa waraka wa wazi kwa ajili ya jambo hili la huduma katika makundi niliyoyataja?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi tunapokea ushauri wa Mbunge na labda niseme tu kidogo kwamba, kwa mfano tunazungumzia tu wazee walioko kwenye mfumo ambao ni wastaafu 149,000 ukiwaangalia sasa hivi kwa mwaka tu wanatumia Bilioni 61 kwenye kupata huduma za afya ambayo ni asilimia 82 tu wao ndiyo wagonjwa. Kwa maana hiyo, ukizungumzia wazee wote kwenye nchi nzima nalo ni tatizo kubwa na nakubaliana naye kwamba inahitajika hela nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi kama ambavyo nimesema swali la kwanza la msingi tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ili kuhakikisha kwamba hayo mambo yanafuatiliwa kwa ukaribu lakini tunawaomba wenzangu Wabunge na sisi tufatilie kwa karibu kuhusu wanavyohudumiwa wazee na mkiona kwamba hawahudumiwi tupaze sauti kwa pamoja, lakini sisi tutaelekeza sheria na kusimamia na kuwaadhibu ambao wanaacha kutekeleza maelekezo ya Serikali.(Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za Afya kwa Wazee hasa wa Mkoa wa Arusha kwa kuwapatia dawa kupitia mfumo wa bima tofauti na iliyopo sasa?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wazee wa Mkoani Kagera walipewa vitambulisho ambavyo vinawaruhusu kwenda kupata matibabu bure. Lakini vitambulisho vile havitambuliki pale ambapo wanakwenda kwenye hospitali au vituo vya afya. Vilevile wakiandikiwa dawa, huwa wanaandikiwa dawa ambazo bado wanaambiwa hawawezi wakapewa pale hospitali au kituo cha afya, inabidi wakanunue nje.

Je, Serikali ina mpango gani kudhibiti hayo maeneo mawili? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisikia ni Mzee mwenye kitambulisho chake, maana yake ni mzee ambaye tayari ameshatimiza vigezo vyote ambavyo vinatakiwa apate huduma. Kwa hiyo, kimsingi anatakiwa apate huduma. Lakini kuna hilo tatizo sasa kwamba anapewa huduma lakini anapofika dirisha la dawa, dawa inayohihitajika kupata haipatikani haipo kwenye dirisha la dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mmesikia hapa nyuma tukiwa tunazungumza masuala ya MSD na upatikanaji wa madawa kwenye vituo vyetu. Nguvu nyingi sasa tunaelekeza kuhakikisha hakuna dawa inayokosekana kwenye vituo vyetu ili wazee wetu waliotimiza vigezo wakienda kwenye dirisha la dawa wapate dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Jumamosi tulikuwa na Wabunge wenzetu wa Kamati ya Huduma za Jamii, kwa ajili ya Muswada wa Bima ya Afya kwa wote. Sasa tutaenda kutoa semina kwa Wabunge wote likija Bungeni basi tulisimamie hilo kwa sababu ndiyo litakuwa suluhu la kudumu. (Makofi)

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za Afya kwa Wazee hasa wa Mkoa wa Arusha kwa kuwapatia dawa kupitia mfumo wa bima tofauti na iliyopo sasa?

Supplementary Question 4

MHE. KASSIM HASSAN HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa huduma hizi za Bima ya Afya upatikanaji wa dawa kwa upande wa Zanzibar zimekuwa za chini sana.

Je, ni lini Serikali itaenda kuboresha huduma hizo ili watu wapate dawa katika hali ambayo itakuwa ni ya kawaida?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe tu Mbunge, wakati wa sisi kupitisha Muswada wetu wa Bima ya Afya kwa watu wote, wote kwa pamoja tushirikiane kuweka input nzuri ambayo mwisho wa siku italeta suluhu ya kuduma bila tena kuona wazee wanarudi kule kule ambako hatukupenda warudi. (Makofi)