Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimshukuru sana Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Nape Nawuye na Naibu wake Mheshimiwa Kundo, kwa ushirikiano mkubwa walionipatia kuhusu hili suala la mawasiliano ya mitandao na kwa majibu mazuri haya ya Serikali sina swali la nyongeza ila niwaambie wana Igunga subiri neema ya mitandao ya simu. Ahsante sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kupokea shukrani na pongezi kwa niaba ya Serikali na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wangu kwa ushirikiano ambao tunawapatia Waheshimiwa Wabunge wote kwa sababu kazi yao ni kuwawakilisha wananchi wao, ahsante.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana kwa kunipa fursa; je, Serikali ina mpango gani kuboresha mawasiliano ya simu ya katika Kata za Urushimbwe, Kibosho Kati na Mabogini, zilizopo katika Jimbo la Moshi Vijijini?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya katika wananchi wake wa Jimbo la Moshi, lakini vilevile katika kata ambazo amezitaja Urushimbwe, Kibosho Kati pamoja na Mabogini, tayari tumeziingiza kwenye mradi wa Tanzania kidigitali. Vilevile Mheshimiwa Mbunge wiki mbili zilizopita alifika ofisini kwetu tukakaa tukaongelea kuhusu suala la kata hizi tatu na alihakikisha kabisa kwamba tayari tumeshaziweka kwenye utekelezaji wa mradi wa Tanzania kidigitali. Nakushukuru sana.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 3

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pia niipongeze Wizara na Mheshimiwa Naibu Waziri aliyetembelea Wilaya ya Misenyi na kuahidi kufunga minara katika kata kumi na mpaka sasa ameongea kata tatu zimeshafungiwa minara bado kata saba. Je, ni lini sasa kata hizo zitamaliziwa kufungiwa minara ili wananchi wapate mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kuna kata ambazo tuliziingiza katika utekelezaji wetu na tayari hatua za awali za ujenzi huo zimeshaanza. Hivyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuwa na subira wakati utekelezaji huu ukiendelea kufanyika kwa wakandarasi wetu wa ndani.

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza la nyongeza. Kata ya Suruke imeshajengwa mnara wa TTCL, lakini leo una mwaka mzima haufanyi kazi. Je, ni lini Serikali itawasha mnara ule wananchi waweze kupata huduma ya mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa minara una hatua, hatua ya kwanza ni kuhakikisha kwamba tunajenga ile passive equipment maana yake kusimamisha ule mnara. Hatua ya pili ni kuweka vile vifaa vya kurusha mawimbi maana yake active equipment. Hatua ya kwanza katika minara yote ya TTCL nchi nzima tumeshamaliza na hatua inayofuatia ni kuhakikisha kwamba sasa tunaweka zile active equipment. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira, kazi hiyo imeshaanza na vifaa vimeshaingia, nina uhakika kwamba kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha hatua zitakuwa zimeshakamilika za utekelezaji katika kusimika hizo acturial equipment. Ahsante sana.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 5

MHE. ALYOCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Wilaya ya Kakonko, zipo Kata za Nyamtukuza, Nyabiboye, Gwarama, Kasuga, Lugenge, Gwanubu, Katanga Namguzu, zina tatizo kubwa sana la mawasiliano ya simu. Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano katika kata hizo. Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kamamba, Mbunge wa Kakonko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kakonko, ni jimbo ambalo liko mpakani na tayari tumeshaliingiza katika utaratibu wa miradi ya mipakani. Tayari tumeshawasiliana na Mheshimiwa Mbunge na kata hizo ambazo amezitaja, zimeshaingizwa katika mpango huo. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge asubiri utekelezaji kulingana na taratibu za kimanunuzi ukamilike na baada ya hapo changamoto ya mawasiliano katika Jimbo la Kakonko itakuwa imepungua kama sio kwisha kabisa.

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 6

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, changamoto ya mawasiliano kwa maeneo ya Kwekivu, Kimbe, Namkindi katika Jimbo la Kilindi ni kubwa na usikivu ni mdogo sana. Je, ni lini mtakwenda kutujengea minara kwa ajili ya kupata mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kilindi, tumeshaliweka katika utekelezaji wa Tanzania ya Kidigitali, kwa hiyo, nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana ili kuhakikisha kwamba wataalam wetu watakapofika katika maeneo yao, watoe ushirikiano na kutoa maeneo kwa ajili ya kusimika miradi hii ya minara.

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha mawasiliano ya simu katika Kata ya Kinungu, Isakamaliwa, Mtungulu, Kining’inila na Itumba?

Supplementary Question 7

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Maeneo mengi ya Wilaya ya Nyang’hwale, hayana mawasiliano kabisa ya simu kama Nyamtukuza, Nyalubele, Ligembe na sehemu zote ambazo ziko maeneo yale ambayo yako karibu na Nyang’hwale. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka mawasiliano ili wananchi wale waweze kupata mawasiliano mazuri?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kujibu hili. Kwa mujibu wa matakwa ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ukurasa wa 97 Ibara ya 61(j) inatutaka Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wote wa Tanzania wanapata huduma ya mawasiliano. Hivyo basi, namwomba Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu najua Mheshimiwa Mbunge wa jimbo tayari tunaendelea kuwasiliana kuhusu changamoto hizo, naamini kabisa mpango wa mwaka mmoja utakapokamilika na mpango wa miaka mitano tunaamini kwamba maeneo mengi yatakuwa yameshapata mawasiliano nchi nzima. Nakushukuru sana.