Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je lini Serikali itaigawa Halmashauri ya Wilaya Uyui, ili itoe Halmashauri nyingine ya Igalula kwa kuwa inakidhi vigezo?

Supplementary Question 1

MHE. DAUD P. VENANT: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri yametia moyo kwa wana Igalula. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza, tulishafanya mchakato mara kwanza tukapitia mchakato wote kama alivyoutaja, tulivyofika kwenye hatua ya mwisho kwenye kikao cha RCC, walisema mchakato huo bado. Lakini sasa unavyosema tumepita kwenye mchakato huo huo na tayari document zimetayarishwa kwa ajili ya vikao hivyo, sasa Serikali kupitia kwako Waziri hauoni haja ya kutoa maelekezo kwenye RCC wao sio hatua ya mwisho kutoa maamuzi waziachie document zije Wizara ili ziendelee na machakato mwingine?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, ni kubwa sana na jiografia yake ni kila unapokwenda unaikuta Uyui. Sasa hamuoni kama Serikali kutoa maelekezo ya kina kwa zile halmashauri ambazo ni zenye competition ili kuweza kuzigawa ili kurahisisha huduma bora kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daud Protas Venant, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema katika swali lake, kwamba walifanya mchakato wa awali, lakini kwa namna moja ama nyingine haukukidhi vigezo lakini wamefanya mchakato wa pili ambao uko ngazi ya mkoa, kwa maana ya kufanya RCC. Sasa tunaelekeza, Mkoa wa Tabora kutekeleza wajibu wao kutimiza sheria hii, kwa maana ya kufanya vikao vya RCC, ili kupitia maombi hayo na baadaye kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa kadri ya mwongozo.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, kuhusiana na maelekezo ya kugawa halmashauri hii kwa sababu ni kubwa itakuja kulingana na tathmini ambayo itafanyika baada ya RCC kuwasilisha maombi hayo ofisi ya Rais TAMISEMI. Ahsante.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je lini Serikali itaigawa Halmashauri ya Wilaya Uyui, ili itoe Halmashauri nyingine ya Igalula kwa kuwa inakidhi vigezo?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Mimi ningependa kujua; kwa vile mchakato wa kupandisha hadhi ya Mji Mdogo wa Mbalizi, ambao ni mamlaka kuwa halmashauri ya mji ilishapitishwa kiwilaya na mchakato vilevile ulishapitishwa kimkoa. Je, ni lini sasa Serikali itaipandisha hadhi hii Mamlaka ya Mji kuwa Halmashauri ya Mji wa Mbalizi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante saa. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijiji kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge amesema katika swali lake taratibu za awali za Mbalizi kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Mji zilishafanyika, naomba tulichukue hilo tufuatilie kama lilishawasilishwa Ofisi ya Rais TAMISEMI, na baada ya hapo tutafanya tathmini kwa mujibu wa sheria na tutawapa mrejesho hatua ambayo itafuata. Ahsante.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je lini Serikali itaigawa Halmashauri ya Wilaya Uyui, ili itoe Halmashauri nyingine ya Igalula kwa kuwa inakidhi vigezo?

Supplementary Question 3

MHE. OMAR M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, ina vijiji 102, vitongoji 611, kata 21 na tarafa nne.

Je, ni lini Serikali italigawa Jimbo hili la Kilindi? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge twende tukajiridhishe na takwimu ambazo amezisema, tuone vigezo na baadaye tuweze kufanya maamuzi, baada ya tathmini hizo tutawapa mrejesho nini hatua inaweza kufuata baada ya tathmini hiyo, ahsante.