Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli utakamilika pamoja na kuhakikisha Kituo hiki kinafanya kazi kama kilivyokusudiwa?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri na ya kuridhisha ya Serikali ningeomba kuuliza haya maswali mawili. Moja, stendi yetu ya Magufuli inaruhusu kuingiza mabasi yote yanayotoka mikoani bila kwenda kokote na kushusha pale abiria, lakini pamekuwepo bado na mabasi mengi kwenda Urafiki na maeneo ya pale kwa Wachina na Maghorofani. Pamoja na maelekezo mengi yanayotolewa na viongozi wa mkoa na wilaya. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya kushindwa kwa muda mrefu kusimamia maelekezo yake?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni ukweli stendi ile pamoja inaenda kukamilika kwa wachache walioingia kupitia mnada wanalipa square mita au mita za mraba Sh.40,000 tofauti na maeneo mengine ya Jiji la Dar es Salaam ikiwepo hata maeneo ya pale Mlimani City, kati ya shilingi 15,000 hadi shilingi 25,000, lakini hawa wanalipa shilingi 40,000.

Je, Serikali haioni sasa ni sababu ya kupunguza kufikia hiyo kati ya shilingi 15,000 hadi shilingi 25,000 ili matumizi yaende kama yalivyokusudiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mtemvu kwa kazi kubwa anayoifanya kuwasemea wananchi wa Jimbo la Kibamba na nimwakikishie Serikali itaendelea kumpa ushirikiano ili aweze kutekeleza miradi mbalimbali ya wananchi wa Kibamba. Kuhusu mabasi ambayo hayaingii kwenye stendi ya Magufuli, ni kweli kumekuwa na baadhi ya makampuni ambayo hayatumii ipasavyo stendi kadri ya maelekezo na malengo ya ujenzi wa stendi ile. Kwa hivyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunalichukua hili tunalifanyia kazi na tutatoa maelekezo mahususi kuhusiana na utaratibu wa mabasi kutumia stendi ile ya Magufuli.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na gharama ya upangishaji kwa square mita kufika hadi Sh.40,000 mapendekezo yake ni Sh.15,000 hadi Sh.25,000 naomba niseme tunalichukua hilo kama Serikali tutalitazama na tuweze kuona mazingira kama yanaruhusu basi tuweze ku- review bei hizo ili wananchi wapate unafuu katika upangishaji.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli utakamilika pamoja na kuhakikisha Kituo hiki kinafanya kazi kama kilivyokusudiwa?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Mkoa wa Songwe ni miongoni mwa mikoa mipya na mpaka sasa hatuna stendi ya mkoa, tayari fedha zilishatengwa. Naomba kufahamu nini mkakati wa Serikali katika kutupatia hizo fedha bilioni 29 ili tuweze kujenga stendi ya mkoa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mkoa wa Songwe kwa sababu ni mpya hauna stendi ya mabasi ya mkoa na kama alivyosema Mbunge Serikali tayari imeshaweka mpango wa kujenga stendi ya mabasi ya Mkoa wa Songwe na imeshatenga fedha. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba kazi iliyopo sasa tunatafuta fedha ili twende kujenga stendi ya kisasa ya Mkoa wa Songwe.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli utakamilika pamoja na kuhakikisha Kituo hiki kinafanya kazi kama kilivyokusudiwa?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa stendi ya Mbezi ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayosimamiwa na TAMISEMI. Je, ni lini mradi wa kimkakati wa Soko la Mlandizi utajengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya maeneo yote ambayo yanahitaji kujengewa stendi za kimkakati ikiwepo Halmashauri ya Kibaha. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tushaelekeza halmashauri walete andiko walishaleta na najua kulikuwa kuna mazungumzo ya eneo wapi tujenge ile stendi. Nikuhakikishie kwamba TAMISEMI tunaendelea na kufanya tathmini ya mapendekezo ya halmashauri ili twende kujenga stendi ile na tutafanya hivyo mapema iwezekanavyo. Ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli utakamilika pamoja na kuhakikisha Kituo hiki kinafanya kazi kama kilivyokusudiwa?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Naomba kuuliza kwa kuwa akinamama wa Mkoa wa Dar es Salaam wengi ni akinamama lishe na wanafanya shughuli ndogondogo, lakini katika eneo hilo hilo la stendi ya Mbezi bado kuna eneo kubwa ambalo Serikali inaweza ikawajengea vibanda vidogo vidogo. Je, Serikali haioni haja hata kwa kutumia Mfuko wa Akinamama ile asilimia yao kuwajengea mabanda rahisi ya kuweza kufanya kazi zao, akinamama wote wa Mkoa wa Dar es Salaam? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tunahitaji kuboresha maeneo ya wafanyabiashara wadogowadogo na ndio maana Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan ameelekeza kuboresha maeneo ya wafanyabiashara wadogo wadogo wakiwemo akinamama ntilie lakini pia machinga na wafanyabiashara wengine. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba eneo la Mbezi ambalo anasema lina nafasi ya kujenga tutakwenda kulitazama ili tuone uwezekano wa kuwekeza hapo. Wazo lake la kutumia asilimia 10 pia tutalifanyia tathmini kuona au kutafuta chanzo kingine kwa ajili ya ujenzi huo. Ahsante.