Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini uchimbaji wa madini ya dhahabu utaanza katika eneo la Utegi, Tarafa ya Girango?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Waziri kwa majibu mazuri pamoja na kwamba hayajaleta sana matumaini kwa wananchi. Pamoja na majibu haya nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza nataka nijue tu kwamba pale utafiti utakapokamilika nini nafasi ya wachimbaji wadogo kupewa nafasi kuchimba madini kwenye eneo lile?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nataka nijue maeneo yanayozunguka eneo la Utegi kama Kowak, Mika na maeneo mengine nini nafasi ya kuanza utafiti kwenye maeneo yale ili eneo litakapokamilika utafiti wa awali kwenye eneo la kwanza iendane sambamba na eneo la pili na haya maeneo mengine?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Jimbo la Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala zima la upatikanaji wa maeneo ya machimbo ya madini kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi hutegemea kukamilika kwa utafiti. Utafiti unapokuwa umekamilika na kwa jinsi ambavyo utafiti huo huchukua gharama kubwa na kampuni zinazofanya utafiti huu ni kampuni kubwa zenye uwezo wa uchimbaji mkubwa, sisi kama Wizara tuna mamlaka ya kumegua eneo ambalo wachimbaji wadogo wanaweza wakakatiwa, waweze nao kupata maeneo yao ya kuchimba kama ambavyo sera yetu inasema kwamba lazima tuwape wachimbaji wadogo maeneo ya kuchimba.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, swali lake hilo la kwanza la wachimbaji wadogo kupatiwa maeneo ya kuchimba linachukuliwa kwa uzito mkubwa na tutawahakikishia kwamba watapewa maeneo.

Mheshimiwa Spika, maeneo ambayo anayazungumzia kwamba ni lini utafiti huo utakamilika na kuweza kuanza uchimbaji, ni wazi kwamba utafiti ndio utakaotupa jibu kwamba ni lini uchimbaji utaanza katika maeneo hayo.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini uchimbaji wa madini ya dhahabu utaanza katika eneo la Utegi, Tarafa ya Girango?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na ripoti ya GST, Wilaya ya Liwale imeonekana kuwa na madini mengi sana ya dhahabu, kito na sapphire. Tayari wawekezaji wako kule na wachimbaji wadogo wameshaanza kazi, lakini Wilaya ya Liwale haina Ofisi ya Madini pale, matokeo yake wale wachimbaji wadogo na wawekezaji wengine wanakwenda Tunduru kuuzia madini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka ofisi pale Liwale ili kuwarahisishia wachimbaji wadogo kupeleka madini yao Tunduru badala ya kuuzia Liwale?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi Wizara ya Madini tumeendelea kujenga masoko ya madini na kuanzisha vituo vya kuuza na kununua madini katika maeneo yote yenye madini nchini. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba ni suala la muda tu katika mzunguko wetu kadiri mapato yanavyoruhusu, tutafika huko Liwale na tutajenga soko na tutahakikisha kwamba wachimbaji wake walioko huko wana masoko ya kuuzia madini yao kwa bei iliyo sahihi na bila kupunjwa na mtu yeyote.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini uchimbaji wa madini ya dhahabu utaanza katika eneo la Utegi, Tarafa ya Girango?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nataka kumuuliza Naibu Waziri kumekuwa na RL nyingi kwa maana ya leseni zilizoshikiliwa na Serikali katika Halmashauri ya Msalala Kata ya Ntobo. Sasa ni lini Serikali itaachia maeneo haya ili wachimbaji wadogo wadogo wa Jimbo la Msalala waweze kutumia haki yao ya msingi kuchimba katika maeneo yale?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo yote yaliyoshikiliwa na Serikali au maeneo yote ambayo yameshikiliwa na kampuni kubwa za utafiti wa madini ambayo anaomba au anadai ni lini watarudishiwa wananchi. Watarudishiwa wananchi pale ambapo utafiti utakamilika au sisi tumebaini kama Wizara kwamba watumiaji wake hawana mpango wa kuyatumia na hivyo tutaweza kukaa nao na kuyarejesha Serikalini tuweze kuwekea utaratibu wa kupewa wadau au wawekezaji ambao wako tayari kuwekeza.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini uchimbaji wa madini ya dhahabu utaanza katika eneo la Utegi, Tarafa ya Girango?

Supplementary Question 4

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ili niulize swali moja dogo la nyongeza. Jiwe la rubi lenye uzito wa kilo 2.8 lipo kwenye maonyesho kwa sasa Dubai na jiwe hili linasadikika linatoka Tanzania na kwamba siku chache zijazo kutakuwa na mnada wa kuuza jiwe hili. Je, kama nchi tunanufaika vipi na mnada huo? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kitandula, Mbunge wa Mkuranga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mnamo tarehe 13 Aprili, 2022 Wizara ya Madini ilipata taarifa kupitia mitandao ya kijamii kwamba kuna jiwe la madini ya rubi lenye uzito wa kilo 2.8 na ambalo linadaiwa kuwa na thamani ya dola za Marekani milioni 120, sawa na zaidi ya bilioni 240 za Kitanzania ambalo limepewa jina la Bad All Hamal na ambalo linakwenda kuwekwa mnadani ndani ya siku 30 baada ya mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan na jiwe hilo kudaiwa kwamba limetoka Tanzania.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya kupata habari hizi Wizara ya Maliasili imechukua hatua za haraka kutafuta kama habari hizi ni za kweli na kama kweli jiwe hili kweli limetoka Tanzania na kwa sababu jiwe hili limeshavuka mipaka liko kwenye nchi nyingine, taarifa hizi sasa tunazozikusanya ili tuweze kutoa taarifa sahihi katika Bunge lako Tukufu zinahusisha Nchi ya Dubai na tayari Ubalozi wetu uliopo Dubai na sisi tunafanya mawasiliano kufuatilia ukweli na uhalisia wa thamani ya jiwe hili. Pia baada ya ufuatiliaji wa awali tumebaini kwamba mmiliki halali au tuseme sasa wa jiwe hilo yuko nchini Marekani katika Jimbo la California na mawasiliano naye pia tumeshafanya tangu jana. Hivyo sasa suala hili linazidi kupanua wigo wake kidiplomasia kwamba linahusisha nchi tatu; Nchi ya Tanzania, Dubai na Marekani.

Mheshimiwa Spika, nikuhakikishie tu kwamba tutakapokuwa tumepata nyaraka za usafirishaji wa jiwe hili kama kweli limetoka Tanzania tukapata nyaraka zinazoonyesha thamani na asili ya hili jiwe kwamba limetoka wapi. Tutakapokuwa tumepata na nyaraka za mauzo kati ya mmiliki wa sasa na wa hapo awali, sisi tutaleta taarifa katika Bunge lako Tukufu za uwepo wa jiwe hili na kama ni la kwetu, niwahakikishie Watanzania kwamba haki yao haitapotea sheria, kanuni na taratibu zetu zitatumika kuhakikisha kwamba rasilimali hii inakwenda kunufaisha Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho, sisi Wizara ya Madini tunaendelea kuwahakikishia Watanzania kwamba tumesimama imara kudhibiti na kusimamia rasilimali madini kwa manufaa ya nchi yetu. (Makofi)

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini uchimbaji wa madini ya dhahabu utaanza katika eneo la Utegi, Tarafa ya Girango?

Supplementary Question 5

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Nina swali linalofanana na hilo. Kule Lupaso kwenye Kijiji cha Matemwe, kunafanyika uchimbaji: Je, Serikali inafahamu kwamba kuna uchimbaji unaendelea pale?

Je, uchimbaji ule unanufaisha vipi Halmashauri na Serikali kwa ujumla?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba nikiri kwamba sina hakika na tuko tayari baada ya Bunge hili nikutane na Mheshimiwa Mbunge na watendaji wetu tuweze kujua na kufuatilia kuhusu machimbo hayo. (Makofi)