Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa, hili zoezi ambalo linaendelea sasa hivi la kuweka mipaka ndiyo limeenda kuchochea kabisa mgogoro uliopo kati ya vijiji hivi 24 na Hifadhi ya Wamembiki. Na kwa kuwa Mheshimiwa Rais anazamira ya dhati kabisa kumaliza huu mgogoro uliopo pale. Je, Serikali haioni kuna haja ya kwenda kuhakiki upya hii mipaka kwa kufuata mipaka ile waliyokubaliana wananchi mwaka 97 kati ya wananchi na Hifadhi ya Wamembiki? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili Mheshimiwa Waziri kwa kuwa wananchi wanayozunguka Hifadhi ya Wamembiki wana changamoto nyingi sana. Uko tayari kuongozana nami baada ya Bunge hili la Bajeti kwenda kuzungumza na hawa wananchi? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jonas Zeeland, Mbunge wa Mvomero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Mvomero kwa kukubali kuruhusu pori hili ambalo lilikuwa ni Hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori (WMA) kuwa Pori la Akiba ambalo kwa kusema ukweli Serikali inawashukuru sana wananchi hawa. Kwa sababu umuhimu wa eneo hili kwanza ni mapito ya wananyama wengi wakiwemo wanyama wakali na ni ushoroba ambao unapita katika maeneo ya Hifadhi ya Selou, Mikumi, Tarangile na Saadan. Lakini pia katika maeneo haya kuna umuhimu wa utunzaji wa vyanzo vya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivyo nimhakikishie tu Mbunge kwamba wananchi hawakukosea kukubali kupandisha eneo hili kuwa Pori la Akiba. Sasa ile changamoto ambayo inaonekana kwamba tumeenda kuibua migogoro mipya niwahakikishie tu wananchi wa Mvomero kwamba tutaenda kuishughulikia na kwa kuwa wataalam wako uwandani basi tutahakikisha hii migogoro inakoma na wananchi waendelee kuishi maisha yao vizuri na wakati huo huo pori hili tunalihifadhi kwa faida ya wananchi wanayozunguka maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili niko tayari tu kuambatana na Mheshimiwa Mbunge pia kwenda kuwaona wananchi, kutatua na kuelezeana namna ya umuhimu wa kutunza maeneo haya kwa ajili ya vizazi vinavyokuja. (Makofi)

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa hii nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, matatizo yaliyoko kwenye hili Pori la Wamembiki yanafanana na matatizo yaliyoko katika Wilaya yangu ya Mbozi kwenye Pori la Isalalo kati ya wananchi wa Kata ya Isalalo na Mbinzo na Itaka na TFS.

Je, ni lini Serikali itatatua huu mgogoro wa Pori la Isalalo? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George, Mbunge wa Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote niwaombe wananchi wafahamu kwamba migogoro mingi ambayo inasemekana kuwa ni migogoro ni migogoro ambayo ni nani amemkuta mwenzie? Pori analoliongea Mheshimiwa George ni eneo ambalo lina GN ambayo GN ni ya miaka ya nyuma na wananchi wamesogea katika maeneo hayo. Kwa bahati mbaya kabisa Kamati ya Mawaziri Nane haikuweza kupita katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimuombe kwa kuwa huu ni mgogoro mpya, Serikali itaenda kuhakiki yale maeneo na kuyaangalia umuhimu, kwanza tunaangalia umuhimu wa eneo lile kama ni vyanzo vya maji na kuna wanyamapori na mazalia ya wanyamapori yako katika maeneo hayo, tunaendelea kuwashauri wananchi kuyaachia yale maeneo pamoja na kuwa tunawaita sisi ni wavamizi. Linapoonekana eneo halina umuhimu sana basi Serikali inapitia na kumega yale maeneo nakuwaachia wananchi.

Mheshimiwa Spika, hivyo nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaenda kuyahakiki hayo maeneo na kama yanaendelea kuwa yanafaa katika uhifadhi basi tutawashauri wananchi lakini kama yatakuwa yaruhusu kumegwa basi tutayaachia. Ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, vijiji vya Ngomalusambo na kijiji cha Vikonge ni miongoni mwa vijiji ambavyo Serikali ilitoa maelekezo kupitia kwa Mheshimiwa Rais Hayati Dokta John Pombe Magufuli viachiwe vibaki kuwa kwa matumizi ya wananchi, lakini mpaka sasa bado vijiji hivyo vina mgogoro kati ya TFS na vijiji hivyo.

Ni lini Serikali itakuja kutatua mgogoro huu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimuahidi tuu Mheshimiwa Kakoso kwamba tutafika katika maeneo hayo nakuyaangalia kama yana umuhimu wa kuyaachia tutaendelea kuyaachia. Ahsante.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nishawahi kuuliza swalli hapa Bungeni la Msitu wa Kazimzumbwi na Mheshimiwa Waziri aliniahidi kwamba Kamati ya Mawaziri Nane itafika kwenda kutatua mgogoro baina ya Msitu wa Kazimzumbwi na wananchi wa Kata ya Zingiziwa, Chanika, Buyuni na Pugu, lakini mpaka ninapozungumza hapa Mawaziri Nane hawajafika.

Naomba kujua, Je, ni lini Mawaziri hawa nane watafika kwenda kutatua mgogoro huo? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ziara ya Mawaziri wa Kisekta hivi sasa ninavyoongea wako safarini kuelekea Arusha na nimuahidi tu Mheshimiwa Jerry kwamba, kwa kuwa oparesheni hii imeshaanza na tunaendelea na zoezi hili tutafika katika msitu huo na tutatatua changamoto hiyo. Ahsante.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.

Vijiji vya Ntwigu, kijiji cha Ng’wandwe, kijiji cha Mwanduti na Kipendamoyo ni miongoni mwa vijiji ambavyo vilikuwa kwenye orodha ya kupatiwa usajili kipindi cha usuluhishi wa migogoro ya Mawaziri nane, lakini baada ya lile zoezi vijiji hivi havijapatiwa usajili.

Mheshimiwa Spika, je hivi vijiji baada ya kuwa vimekosa hadhi ya kuwa kwenye Hifadhi kwa sababu hakuna wanyama na wale wananchi wameshakuwa wengi wamevamia hilo eneo. Ni lini sasa hivi vijiji vitapewa usajili wa kudumu ili wananchi wajue mipaka yao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rehema Migilla kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, usajili wa vijiji unafanywa na Serikali za Mitaa. Hivyo nimuombe Mheshimiwa Rehema kwamba atawasiliana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuangalia kama kuna umuhimu wa vijiji hivi kusajiliwa. Na niombe vijiji hivi vinavyosajiliwa viwe na hadhi inayolingana. Kwa sababu kuna vijiji vingine vinapelekwa kwenda kusajiliwa kumbe viko ndani ya hifadhi. Nitoe tahadhari hiyo kwa wananchi kwamba wanapopeleka vijiji hivi kwenda kusajiliwa wajiridhishe kwamba je, wako ndani ya vibali vinavyoruhusiwa kusajiliwa? Ahsante.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 6

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, naomba nimuulize Waziri wa Maliasili na Utalii ni lini itafika katika Jimbo langu la Nanyumbu kutatua mgogoro wa mipaka katika vitongoji vya Wanika na Malomba na kijiji cha Mbangala Mbuyuni? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa
Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahya, Mbunge wa Nanyumbu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, kabla ya bajeti hii kuisha basi nimuombe tutafute hata weekend moja tuende tukatatue mgogoro huu. Ahsante. (Makofi)