Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya Singida Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, ninaipongeza sana Serikali kwa majibu mazuri haya ambayo yanaleta matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Singida Mjini. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa, uwepo wa hospitali ya Wilaya unaenda sambamba na ujenzi wa vituo vya afya. Wananchi wa Kata ya Kisaki wamejenga kituo chao cha afya na Serikali ilileta Shilingi Milioni 50 na kituo hakijakamilika.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha kituo hicho cha afya?

Swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri utakuwa tayari kuambatana nami kwa ajili ya kwenda kutembelea maeneo yote hayo ambayo tumeyataja hapo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima kwa namna ambavyo anawatendea haki wananchi wa Jimbo la Singida Mjini, nimhakikishie kwamba katika zahanati ile ambayo tayari Serikali ilipeleka shilingi milioni 50 kwa ajili ya ukamilishaji katika Kata ya Kisaki, natoa maelekezo ambayo tayari Ofisi ya Rais TAMISEMI tulikwishayatoa kwamba zahanati zote ambazo zilipokea shilingi milioni 50 kama hazijakamilika ni lazima Halmashauri kupitia mapato yao ya ndani watenge fedha na kukamilisha. Kwa hivyo, natoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida kuhakikisha zahanati hiyo inakamilishwa.

Mheshimiwa Spika, pili, niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge tutakubaliana baada ya kikao hiki tupange ili twende kufanya ziara katika Jimbo lake. (Makofi)

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya Singida Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, sasa Hospitali ya Wilaya ya Ngorongoro imeanza kutoa huduma; Je ni lini sasa Serikali itapeleka Wauguzi pamoja na vifaa tiba ambayo ni changamoto kubwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Ngorongoro inafanya kazi lakini tunafahamu kwamba bado kuna upungufu wa vifaa tiba na kuna upungufu wa watumishi. Ndiyo maana katika ajira za mwaka huu wa fedha, Serikali inakwenda kuajiri watumishi wa afya 7,600 ambao watapelekwa katika maeneo mbalimbali ikiwepo Hospitali ya Halmashauri ya Ngorongoro lakini pia imetenga fedha kwenye mwaka ujao Shilingi Bilioni 69 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hospitali hii pia itapewa kipaumbele.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya Singida Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika Hospitali yetu ya Mkoa wa Manyara tuna jengo moja tu lililokamilika ambayo ni maternity ward. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo yote ya hospitali ikiwemo word na jengo la upasuaji na jengo la radiology ili kurahisisha utoaji wa huduma?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu la nyongeza la Mheshimiwa Regina Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie kwamba mpango wa Serikali ni kuhakikisha hospitali za Rufaa za Mikoa zote zinakuwa na majengo yote muhimu kwa ajili ya kutoa huduma za afya. Kwa hivyo, hospitali hii ya Mkoa wa Manyara nayo ambayo ina upungufu wa wodi, majengo ya upasuaji na majengo ya radiology tutahakikisha tunaendelea kutafuta fedha ili majengo hayo yajengwe kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya Singida Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pale kwenye hospitali ya Wilaya ya Makandana tunaishukuru sana Serikali imepeleka vyombo muhimu sana kwa maana ya X-Ray na Ultrasound, lakini pale kuna Mtaalam mmoja kiasi kwamba akiugua au akipata dharura huduma hiyo inasitishwa kwa muda pale.

Je, ni lini Serikali itatuongezea Mtaalam mwingine kwa ajili ya Ultrasound na X-Ray?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Suma Fyandomo Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Rungwe maarufu Makandana ni muhimu sana inaendelea kutoa huduma za jamii kwa wananchi wa Rungwe, Serikali imetambua uhitaji wa vifaatiba kama X-Ray na Ultrasound imepeleka inafanya kazi. Ni kweli kwamba tuna mtumishi mmoja lakini mpango wa Serikali ni kuhakikisha tunaendelea kuajiri watumishi hao na hivi sasa tumeweka mpango mkakati wa kuwasomesha wataalamu wa usingizi na Radiology ili wawe wa kutosha katika halmashauri zetu. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatafuta watumishi ili kuongeza watumishi katika hospitali ile.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya Singida Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Ningependa kuuliza Serikali, Je, ni lini itapeleka fedha za kukamilisha ujenzi na kununua vifaatiba kwa ajili ya hospitali za Wilaya za Biharamulo, Bukoba DC, Karagwe na Kyerwa ili ziweze kukidhi viwango vya kuwa hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba hospitali zetu za Halmashauri zikiwemo hizi za Biharamulo, Bukoba, Kyerwa na maeneo mengine lakini nchini kote tuna upungufu wa baadhi ya vifaatiba na ndiyo maana katika bajeti zetu zote tumeendelea kutenga fedha na bajeti ijayo tumetenga Shilingi Bilioni 69. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutahakikisha tunazipa vipaumbele hospitali hizo.