Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, nini hatma ya madai ya maslahi ya waliokuwa wafanyakazi wa mgodi wa TanzaniteOne?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwanza majibu ya Serikali yamenishangaza kidogo, kwa sababu hapa wanazungumzia TanzaniteOne lakini ukiangalia TanzaniteOne tayari walishauza hisa kwa Sky Associate Group Limited.

Swali langu, kwa sababu hawa Sky Associate inaonekana kwamba walikuwa hawajasajiliwa na BRELA hapa Tanzania, je, mmiliki wa iliyokuwa TanzaniteOne ni TanzaniteOne wenyewe au hao Sky Associate Group Limited? Hilo ni swali langu la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, wafanyakazi wa iliyokuwa TanzaniteOne hawajawahi kufukuzwa au kuondolewa kazini; je, hadi sasa wanazungumzia mahakamani miezi 11 lakini wanadai zaidi ya miezi 60 mpaka sasa.

Je, na hii miezi mingine iliyobaki watalipwa lini na kwa utaratibu gani na nini msimamo wa Serikali kwenye jambo hili? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa wamiliki wa mgodi kwamba kulikuwa na ubia ya mwingine zaidi ya TanzaniteOne pamoja na mwenzake aliyemtaja ni kwamba mgodi huu uliingiwa ubia kati ya TanzaniteOne na kampuni yetu ya Madini ya STAMICO. Kwa mujibu wa mikataba iliyokuwepo hakukua na mwingine na ndiye ambaye aliingia huu ubia na ndiye ambaye alikuwa mwendashaji wa mgodi na mwenye dhamana ya kuajiri na kufukuza wafanyakazi.

Mheshimiwa Spika, kwa swali la pili, malipo au madai wanaodai hawa wanaodai haki zao ambayo ipo kwenye kumbukumbu na ndio ambayo malalamiko haya yamefikia Wizarani ni hiyo shilingi bilioni 2.5 na sio bilioni 60 anayotamka na kama kuna madai ya nyongeza. Kwa kuwa suala hili tayari lipo bado kwenye mifumo ya kisheria, vyombo vyetu vya kisheria vitaendelea kulifuatilia na kufanyia kazi kwa mujibu wa taratibu na kanuni za Wizara husika.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, nini hatma ya madai ya maslahi ya waliokuwa wafanyakazi wa mgodi wa TanzaniteOne?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa wafanyakazi hawa waliokuwa TanzaniteOne wamekuwa wanasumbuka muda mrefu sana.

Je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka wa kukaa na mwekezaji mpya waangalie wafanyakazi wenye sifa, waweze kupewa ajira katika hii kampuni mpya ambayo imekuja badala ya TanzaniteOne? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wafanyakazi hawa 540 wanashauri lililoko mahakamani na shauri lao ni la muda mrefu na wanamalalamiko ambayo hayajafanyiwa kazi, siamini kama mwendeshaji mpya wa mgodi huu wa TanzaniteOne atakuwa tayari kuwachukua watu ambao tayari wana mgogoro na eneo lile ambalo wanalifanyia kazi. Kwa hiyo, mimi ningeshauri tu kwamba shauri lao lifuatiliwe hadi mwisho, ila kama kuna wenye sifa na mwenye mgodi mpya anaona kwamba anaweza kaujiri bila kujali mtafaruko au kesi waliyonayo, sisi kama Wizara hatutoingilia hilo.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, nini hatma ya madai ya maslahi ya waliokuwa wafanyakazi wa mgodi wa TanzaniteOne?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nilikuwa nataka kufahamu ni lini Serikali itaweza kusimamia malipo ya wahanga wa kesi ya mwaka 1994 katika kata ya Bulyanhlu?Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Madini, siku zote iko tayari kusikiliza kero za wadau wake wa sekta ya madini na kama malalamiko haya yakifikia Wizarani, sisi tutalifanyia kazi bila kusita.