Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni chombo gani kinadhibiti vyuo binafsi vinavyodahili walimu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa kumekuwa na matatizo mengi yanayoikabili elimu nchini Tanzania tumeona watoto wengi wanamaliza darasa la saba hawajui kusoma na kuandika, lakini pia idara nyingi za udhibiti wa elimu nchini Tanzania hazina vitendea kazi.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwanunulia vitendea kazi hususani magari Idara ya Udhibiti Ubora wa Elimu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, kuna mwongozo wowote ambao umetolewa na Wizara ya Elimu katika kudhibiti hivi vyuo vya watu binafsi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbogo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza anazungumzia suala la vitendea kazi; kwanza nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeshafanya mambo makubwa sana kwenye udhibiti wa ubora wa elimu nchini hasa kwenye upande wa vitendea kazi.

Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali imeshajenga ofisi karibu katika halmashauri zote za wilaya nchini kwa ajili ya maeneo ya ndugu zetu hawa au watumishi wetu kuweza kupata mazingira mazuri na salama ya kutendea kazi zao. Lakini vilevile mwaka uliopita wa fedha Serikali ilinunua magari zaidi ya 184 na kuyasambaza kwenye halmashauri au kwenye ofisi hizi za wadhibiti ubora katika halmashauri zote nchini, lakini juzi juzi hapa baada ya zoezi la Sensa kukamilika tumepeleka vishikwambi katika ofisi hizi kwa ajili ya watumishi hawa katika ngazi hii ya udhibiti ubora.

Kwa hiyo, kwa msingi wa vitendea kazi tayari Serikali tumeshafanya kazi kubwa sana na hivi sasa tupo katika programu za kuwaongezea uwezo kwa maana ya kuweza kuweka programu mbalimbali za mafunzo kwa watumishi hawa ili kuweza kutenda kazi yao sawasawa. Niwaondoe wasiwasi Waheshimiwa Wabunge kwamba tayari Serikali imefanya kazi kubwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la miongozo katika utendaji kazi kwenye udhibiti ubora tunakwenda na kanuni pamoja na miongozo mbalimbali ya elimu, ndio wanayozingatia katika utendaji wao wa kazi wa kila siku. Kwa hiyo miongozo kimsingi ipo kuhakikisha kwamba kazi hizi zinakwenda sawasawa, nakushukuru sana.