Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa barabara za Wilaya ya Same baada ya kutengewa 9.5% tu ya fedha za TARURA kwa mwaka 2018/2019?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu haya ambayo yanaleta faraja kwa watu wa Same, kati ya mtandao wote wa barabara hizi za Same za kilometa 874 asilimia 80 ya barabara hizo zina-connect watu wa milimani ambao wao ndio wakulima wengi na kule ndiko kwenye mvua kubwa ambazo hizi barabara huharibika mara kwa mara.

Je, Serikali itakubaliana na mimi kwamba wakati umefika sasa barabara hizo zitengenezwe kwa kutumia aidha mawe au zitumie zege hasa zile sehemu mbaya ili wananchi waweze kupeleka mazao sokoni kwa wakati wote? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri maeneo ambayo ameyaainisha ya milimani katika Halmashauri ya Same na mimi nimefika na ninatambua hali ngumu ambayo wanapata wananchi wa maeneo hayo na Serikali tumepokea ushauri na tutashauriana katika ngazi za chini ili waweze kutekeleza sehemu ya mawazo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyatoa, ahsante sana.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa barabara za Wilaya ya Same baada ya kutengewa 9.5% tu ya fedha za TARURA kwa mwaka 2018/2019?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga haina kabisa mtandao wa barabara ya lami; je, nini kauli ya Serikali kuhusu kuipatia halmashauri hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ndio maana moja ya mkakati wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI katika bajeti zilizopita ilikuwa ni kutoa shilingi milioni 500 katika kila jimbo ili waanze sasa kujenga mtandao wa lami.

Kwa hiyo, kwa sababu hiyo ahadi inaendelea kutekelezeka nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi tutafanya hivyo, lakini mapendekezo makubwa mnayatoa ninyi wenyewe, lakini wazo la Serikali ni kuweka mitandao ya lami katika maeneo yote, ahsante sana.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa barabara za Wilaya ya Same baada ya kutengewa 9.5% tu ya fedha za TARURA kwa mwaka 2018/2019?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa mafuriko au maporomoko yale ya milimani kipindi cha mvua yanaleta maji yote tambarare na barabara inayotoka Same mpaka Bendera inakuwa haipitiki, wakati mwingine hasa kuanzia Ndungu mpaka Bendera kwenyewe.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuifanya na kuipasisha barabara hiyo ijengwe kwa lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua adha ambayo Mheshimiwa Mbunge ameieleza na ndio maana katika mkakati wa Serikali tumeongeza fedha ili tuhakikishe kwamba hizi changamoto ambazo Wabunge wamekuwa wakizieleza humu ndani tunazitatua. Kwa hiyo, na hilo tumelipokea tutaliweka katika mipango yetu, ahsante sana.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa barabara za Wilaya ya Same baada ya kutengewa 9.5% tu ya fedha za TARURA kwa mwaka 2018/2019?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza nampongeza mlezi wetu Mheshimiwa Zuberi Ali Mauridi, Spika Baraza la Wawakilishi kule Zanzibar kwa kufanya ziara katika Mkoa wetu wa Lindi na Jimbo la Mchinga. (Makofi)

Sambamba na hilo wakati anaelekea kwenye ile shule maalum ya wasichana ambayo Mama Samia Suluhu Hassan ametoa pesa shilingi bilioni nne. Mheshimiwa hakuweza kufika kule kutokana na ubovu wa barabara; barabara ile ni ya matope; na kwa kuwa mwezi wa saba shule ile itaanza, imeshapewa kibali cha usajili.

Je, je ni lini barabara ile itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Mchinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba moja ya jitihada kubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni kwamba ni kujenga shule maalum za wasichana katika kila mkoa zenye wastani wa thamani ya shilingi bilioni nne na katika maeneo hayo tunatambua tunahitaji mtandao ya barabara. Kwa hiyo, kwa hatua ya awali tutawaelekeza TARURA Mkoa wa Lindi, kwanza waijenge kwa kiwango cha changarawe ili iweze kupitika wakati wote wakati sisi tunatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa barabara za Wilaya ya Same baada ya kutengewa 9.5% tu ya fedha za TARURA kwa mwaka 2018/2019?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, changamoto zilizoko kule Same zinafanana sana na changamoto za Meru ambako barabara nyingi zinakwenda mlimani na barabara ni za vumbi.

Je, Serikali haioni kwamba ni wakati muafaka sasa wa kuongeza bajeti ya matengenezo ya barabara ili tuweze kuwa na barabara ambazo ni za hard surface?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaona haja hiyo ya kuongeza fedha kwa ajili ya bajeti za matengenezo na ujenzi mpya na ndio maana kila mwaka imekuwa ikiongeza bajeti. Kwa hiyo, sisi tulishukuru Bunge kwa kutuongezea na tutafanya hivyo kuhakikisha barabara za jimboni kwako na Tanzania nzima kwa ujumla zinapitika wakati wote, ahsante sana.