Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Hospitali ya Kanda ya Kusini iliyopo Mtwara itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwanza nishukuru na niipongeze Serikali kwa jitihada inayofanyika kwa ajili ya kuendeleza hospitali hii.

Mheshimiwa Spika, hospitali hii ni tegemeo kubwa sana kwa watu wa Kanda ya Kusini ambao wanalazimika kutembea umbali wa kilometa 1,200 kwa mfano kutokea Mbamba Bay mpaka Dar es Salaam kufuata hizi huduma kutokana na pale kutokuwa na huduma kamilifu. Hospitali hii haina ambulance, haina gari ya Mkurugenzi, haina chumba cha kuhifadhia maiti, hospitali hii OC yake ni ndogo sana lakini ndiyo Hospitali ya Kanda.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka jicho la kipekee katika hospitali hii? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili; sambamba na hilo watumishi pia wako wachache, lakini tayari kumeshakuwa na msongamano na pia kupunguza msongamano ambao pia unaelekea katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Je, ni lini Serikali itaongeza idadi wa watumishi ili kuondoa hadha hii ambayo imeendelea huko? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza Mbunge kwa namna ambavyo anafatilia masuala ya huduma kwenye kanda yake, lakini pia tumepokea barua yake kuhusu vifaa vinavyohitajika na Wilaya yake, pamoja na mambo mengine.

Mheshimiwa Spika, lakinio niseme kwamba moja kwanza ieleweke kwamba hospitali hii ya kanda ni hospitali ambayo sasa ndiyo inaenda kufikisha miaka miwili toka izinduliwe na Makamu wa Rais na kwa kibali cha mwaka huu tumepeleka kuomba kuajiri watumishi 111; lakini kwa sasa wako watumishi 166.

Mheshimiwa Spika, lakini pia amezungumzia suala la ambulance; kwa hospitali hii ya kwenu katika ambulance 727 ambazo Rais wetu ametoa fedha kwa ajili ya kununua ambulance iko kwa ajili ya hospitali hii ya kwenu.

Mheshimiwa Spika, lakini amezungumzia suala la mortuary na mengine; shilingi bilioni 4.4 ambazo ninazungumzia hapa tayari manunuzi yameanza kufanyika kwa ajili ya ujenzi wa mortuary, ujenzi wa nyumba za wanyafakazi, umaliziaji wa maabara lakini umaliziaji wa jengo la mama na mtoto.

Kwa hiyo, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hospitali hii itaenda kuwa ni nzuri na unajua we mwenyewe kwamba katika hospitali zote za kanda nchini hospitali hiyo ndiyo ina majengo mazuri kuliko hospitali yoyote, ahsante sana.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Hospitali ya Kanda ya Kusini iliyopo Mtwara itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; kwa kuwa Singida Mjini hatuna Hospitali ya Wilaya na kwakuwa Wizara ya Afya ilikuwa tayari kutukabidhi Hospitali ya Mkoa kwa maana ya yale majengo ya Mkoa ili tuanzishe Hospitali ya Wilaya. Sasa nataka kujua ni lini mtatukabidhi hayo majengo ya Mkoa tuweze kuanzisha Hospitali ya Wilaya? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli anaposema Mheshimiwa Mbunge Hospitali ya Mkoa iko sasa hivi kwenye eneo ambalo Hospitali ya Wilaya ndiyo inatakiwa iwepo na sasa kuna majengo mengine ambayo yanaendelea kujengwa kwenye eneo lingine. Lakini Mheshimiwa Mbunge ni kweli tuna majengo yanamaliziwa siyo muda mrefu ili Hospitali ya Mkoa iweze kuhama lakini nikuhakikishie tuna shida hiyo kule Geita, pale kwako tutahama polepole kwa sababu ukiama ghafla haraka haraka unaweza ukavuruga shughuli za tiba kwenye eneo lako, ili tusikuharibie siasa yako kabla ya mwaka 2025 tunamalizia majengo, tutahama polepole, lakini tutahakikisha kwamba hatutavuruga shughuli zako, cha msingi wape ushirikiano lile lile eneo na mshirikiane kwa pamoja kuweza kutoa huduma. (Makofi)

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Hospitali ya Kanda ya Kusini iliyopo Mtwara itakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwanza tunaishukuru sana Serikali kwa hatua iliyofikia katika hospitali yetu ya Kanda ya Kusini, lakini tumekuwa na changamoto kubwa sana ya Madaktari Bingwa. Je, ni lini sasa Serikali itatuletea Madaktari Bingwa katika hospitali yetu hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba hospitali ile inahitaji Madaktari Bingwa. Kuna Madaktari Bingwa, lakini Madaktari Bingwa kwa kiwango kinachohitajika kwa Hospitali ya Kanda bado hawajafikia hicho kiwango. Sasa upembuzi yakinifu unafanyika kuweza kuainisha maeneo mengine ili kuamisha na kupeleka kwenye eneo hilo.

Mheshimiwa Spika hivyo hata hivyo cha kwanza tulikuwa tunangojea kukamilisha baadhi ya miundombinu hapa karibuni ndiyo CT-scan imekwenda na MRI mashine, sasa hata ukiwahamisha wataalam wa kibingwa wanaweza wakapata vifaa vya kufanyia kazi ndiyo maana hawajaweza kupelekwa mapema katika eneo hilo.