Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kyatema – Kanazi – Ibwela – Katoro – Kyaka kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, inaonesha kwamba Serikali huenda haifahamu vizuri barabara hii.

Mheshimiwa Spika, barabara hii inahudumia kata 18 za Bukoba, inahudumia wilaya mbili; Wilaya ya Bukoba na Wilaya ya Misenyi, inahudumia nchi mbili; inaziunganisha Tanzania na Uganda na vita ya mwaka 1978 ya Iddi Amini ilipiganwa kwa kutumia barabara hii.

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili kwenda Bukoba kuangalia barabara hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika barabara hiyo kuna Daraja la Kalebe, daraja kubwa ambalo ni la zamani sana, ni bovu, linaruhusiwa uzito wa tani saba, lakini kwa vile hakuna ulinzi wala kizuizi wanapita magari ya tani 15 mpaka 20.

Je, tunasubiri watu wafe pale ndio mtengeneze daraja hilo na barabara hiyo?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Jasson Samson Rwekiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri Mheshimiwa Mbunge amekuja mara kadhaa Wizarani akifatilia ujenzi wa barabara hii pamoja na daraja lake. Kwa niaba ya Serikali napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge ya kwamba nipo tayari kuongozana naye kwenda jimboni Bukoba Vijijini ili nikashuhudie na kuona barabara hii pamoja na daraja hili mara baada ya vikao hivi vya Bunge.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili suala la Daraja la Kalebe ni sehemu ya barabara hii ya kutoka Kyatema- Kanazi, Bwela, Katoro – Kyaka; na kwa maana hiyo kwa kuwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekwishakamilika na mwaka ujao wa fedha tumeweka mapendekezo kwamba barabara hii na daraja hili vijengwe.

Kwa hiyo, nitamwomba Mheshimiwa Mbunge bajeti yetu ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ikifika aipitishe ili pia daraja tuweze kulijenga, ahsante.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kyatema – Kanazi – Ibwela – Katoro – Kyaka kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, naomba kuiuliza Wizara, wananchi wa Mkoa wa Mbeya wanataka kujua ni lini barabara ya njia nne itaanza kujengwa ambayo ilisaidiwa kwamba kuanzia Uyole mpaka Mbalizi? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natambua umuhimu wa barabara hii ya Mbeya mpaka Tunduma na tayari Serikali ilikwishaitangaza na mkandarasi amepatikana na tunachosubiri na hata kwa maelekezo yako ni kwamba hivi karibuni hususan ndani ya mwezi huu wa pili tutasaini mkataba ili barabara hii ianze kujengwa kwa njia nne kama ambavyo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan alivyoahidi alivyotembelea Mkoa wa Mbeya, ahsante.