Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itauboresha uwanja wa mpira wa Boma uliopo Masasi Mjini kwa kiwango kinachofaa kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana wa Masasi?

Supplementary Question 1

MHE. GEOFREY I. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwa kuwa tunashida kubwa ya ajira kwa vijana, lakini pia kwa kuwa tunajua kuna vipaji vingi vya vijana kwenye nchi yetu, lakini pia kwa kuwa tunafahamu ziko nchi zimewekeza vya kutosha kwenye vijana kama vile Brazil, Congo DRC, Senegal, Nigeria, Ghana, naomba sasa niulize maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, ningependa kujua kwamba kutokana na umuhimu huu ambao nimeusema, Wizara inaweza ikatengeneza utaratibu kwa kuanza kuweka bajeti kidogo ya kuweza kusaidia Halmashauri za Miji Midogo ambayo haina uwezo wa kibajeti kuweza kuendeleza viwanja ambavyo tayari vipo kwenye maeneo yale? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tunafahamu kwamba kuna juhudi kubwa zinafanywa na watu binafsi kwenye kuendeleza vijana kupitia shule mbalimbali za soka. Je, Serikali inaona ni muhimu sasa kuweza kusaidia vituo vya kulelea vijana na hasa ukuzaji wa vipaji vya soka na michezo mingine ili tuweze kupata vijana ambao wameandaliwa vizuri kwa ajili ya timu ya Taifa na kuweza kupata ajira nje ya nchi? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwambe, Mbunge wa Masasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza alipenda kufahamu kama Serikali tupo tayari ku-support halmashauri ambazo bajeti zao ni chache na wasingeweza kufanya kazi hii.

Mheshimiwa Spika, katika majibu yangu ya msingi nimesema kwamba jukumu hili ni la Serikali Kuu, lakini pia Serikali za mitaa. Naomba nipongeze Halmashauri ya Masasi wao wameshaanza kuzungusha uzio katika uwanja ule, lakini pia sisi kwa upande wa Wizara pia tumeanza kujenga baadhi ya viwanja na katika mwaka huu wa bajeti, tulitenga viwanja zaidi ya saba. Pale bajeti ambapo itaruhusu sisi tutaendelea ku-support.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili alitaka kufahamu ni kwa kiasi gani tunaweza tuka-support vituo vya kukuza vipaji (academies).

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara tunaandaa mazingira wezeshi kuhakikisha hizi academy zinafanya vizuri na mpaka sasa tuna academies binafsi zaidi ya 84. Kwa hiyo, sisi Wizara tutaendelea ku-support. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itauboresha uwanja wa mpira wa Boma uliopo Masasi Mjini kwa kiwango kinachofaa kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana wa Masasi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la msingi.

Kwa kuwa shule nyingi sana za sekondari, za msingi na vyuo zina viwanja vibovu sana na Mheshimiwa Waziri amesema kwamba kuna baadhi ya halmashauri tayari zimeanza kutenga hizo fedha. Je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na jambo hilo kwa sababu watoto wetu wanakosa haki yao ya msingi ya kutengeneza vipaji vyao?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara na kama Serikali tulishatoa kauli kwamba katika shule zetu tuhakikishe tuna miundombinu ya michezo. Hivyo nitoe rai kwa halmashauri zetu, vyuo na maeneo ambako vijana wetu wanahitaji miundombinu hiyo waendelee kutenga, lakini wavitunze na waviendeleze.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itauboresha uwanja wa mpira wa Boma uliopo Masasi Mjini kwa kiwango kinachofaa kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana wa Masasi?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, wakati Naibu Waziri anajibu maswali yake anaonesha jukumu kuu la Serikali pamoja na Serikali za Mitaa ni kujenga, kuhakikisha kwamba viwanja vinajengwa, lakini kuna halmashauri ambazo kwa mwaka mapato ya ndani hayafiki hata shilingi bilioni moja. Hapo ametutajia mfano Halmashauri ya Geita ambayo inapata mrabaha tu shilingi bilioni sita, hao wana uwezo wa kujenga.

Ninataka nijue, ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha zile halmashauri ambazo hazina uwezo zinajengewa viwanja walau vyenye hadhi ya kuhodhi ligi ya mkoa?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru, naomba nijibu swali moja la Mheshimiwa Esther, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kwamba suala la michezo ni hitaji la wananchi wetu na tunafahamu kwamba vipaumbele vyetu katika nchi ni pamoja na kuhakikisha magonjwa yasiyoambukiza yanaweza kupigwa vita na wananchi wanakuwa salama. Pamoja na kwamba bajeti zetu hazitoshi katika halmashauri, nitoe rai kwa halmashauri zote kutenga fedha hizi kwa kuwa tusipotenga fedha hizi maana yake hatutekelezi sera hii ya maendeleo ya michezo.

Kwa hiyo, hata kama bajeti zetu ni ndogo tutenge, kwa mfano Halmashauri hii ya Masasi, Mheshimiwa Mbunge pia ametenga sehemu ya Mfuko wa Jimbo kuhakikisha ana- support jitihada za halmashauri, kwa hiyo, tuendelee kutenga fedha.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itauboresha uwanja wa mpira wa Boma uliopo Masasi Mjini kwa kiwango kinachofaa kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana wa Masasi?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi ni moja kati ya viwanja kongwe nchini ambacho kiko katika Mkoa wa Tabora.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha uwanja huo ili na wenyewe uweze kutumika katika michezo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Mwaifunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara yetu pia tunapojenga viwanja hivi tunaangalia na ukanda, lakini pia katika jitihada za Serikali tumehakikisha kwenye vile vipaumbele vyetu kwa upande wa academies tulizozianza, Tabora tulianza nao.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Hawa naomba nipokee ombi hili kwamba tutaendelea kutenga fedha kama ambavyo tumetenga kwenye viwanja saba vya mwaka huu, zaidi ya shilingi bilioni 10 tumeanza kazi, kwa hiyo tutawafikia.