Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza magari ya kisasa ya zimamoto?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru saba kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa mikoa ambayo inategemea sana uchumi wa misitu; mikoa ya nyanda za juu Kusini na hasa Mkoa wa Njombe, wananchi wamepata umasikini mkubwa sana kutokana na moto ambao unatokea mwaka baada ya mwaka. Serikali ina mpango gani wa kuwa na mkakati wa kusaidia kwa kuleta vifaa vya kisasa kwenye maeneo hayo ambayo yanashambuliwa sana na moto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli anayoyasema hutokea kwenye mikoa na wilaya nyingi zenye misitu. Kwa kutambua hilo ndiyo maana Mkoa wa Njombe hadi sasa wanayo magari mawili, moja liko Njombe Mjini na lingine liko Makambako. Ni dhamira ya Serikali kadiri uwezo wetu utakavyoongezeka wa kununua magari ya kuzimia moto, Mkoa wa Njombe pia utazingatiwa.