Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuanzisha mfuko wa mabadiliko ya tabianchi kusaidia kupambana na athari za mabadiliko ya Tabianchi?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali namba moja; kwa kuwa tayari kuna jitihada ambazo zilishafanyika toka mwaka 2014 za kuanzisha mfumo wa fedha wa mabdiliko ya tabianchi (Tanzania Climate Financing Mechanism), pamoja na tafiti nyingi pia zilifanyika, ili kuanzisha mfuko wa mabadiliko ya tabia ya nchi.

Je, kwa nini Serikali haioni haja ya kutumia taarifa na tafiti mbalimbali ambazo zilifanyika huko kabla ili kuweza kuharakisha utaratibu huu wa kuanzisha mfuko wa mabadiliko ya tabianchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali namba mbili; kama ninavyokumbuka kwamba dunia inalichukulia suala la mabadiliko ya tabianchi ni janga kubwa kuliko athari nyingine za kimazingira;

Je kwa nini Serikali haioni haja ya kutengeneza mfuko wa mabadiliko ya tabia ya nchi unaojitegemea ili kuweza kuchochea ufadhili na kuweza kuhamasisha wafadhili na wahisani kuweza kuchangia mfuko wa mabadiliko ya tabianchi sambamba na zile jitihada za Serikali kuweza kuji- commit fedha zaidi katika huu mfuko? Ahsnate sana.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Jimbo la Donge, maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo alilolishauri Mheshimiwa Mbunge, tayari ni jambo ambalo tumeshaanza kulifanyia kazi. Hivi ninavyokwambia tumeshaanza mchakato wa mapitio ya Sheria hii ya Mazingira ambayo imo katika Sura ya 191. Tumeanza mchakato huu lengo na madhumuni ili kuona, kwanza namna gani mfuko huu utaundwa, lakini vipi unaweza ukapokea fedha, namna utakavyozitoa hizo fecha, ni fursa na faida gani na ni athari zipi ambazo zinanweza zikapatiwa msaada ama zikasaidiwa kupitia mfuko huu, baada ya mfuko huu kwa sasa unaanza kutoa hizo. Kwa hiyo kikubwa nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato umeanza na muda wowote unaweza ukakamilika na hiyo hali ikaanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kingine nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba lengo na adhma ya Serikali katika kuunda mfuko huu kwanza ni kuhakikisha kwamba mfuko huu unajitegemea, lakini la pili ni kuhakikisha kwamba mfuko huu unapata fedha ya kutosha, tatu ni kuhakikisha kwamba mfuko huu unapata misaada kutoka kwa wafadhili mbalimbali, ili lengo na madhumuni mfuko huu uweze kusaidia wananchi katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na utunzaji na uhifadhi wa mazingira. Hivyo nimwambie tu Mhehsimiwa Mbunge kuwa adhma ya Serikali inaendanana na mawazo yake.

Mheshimiwa Mwenyekti, nakushukuru.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuanzisha mfuko wa mabadiliko ya tabianchi kusaidia kupambana na athari za mabadiliko ya Tabianchi?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafsi. Kwa kuwa mabadiliko ya tabianchi yana madhara makubwa na huweza kusababisha majanga.

Je Serikali inaimarishaje kuwapa taaluma kisasa zaidi ya uokozi na uhifadhi watu wengi zaidi badala ya kutegemea JWTZ na Zima Moto pekee?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO
NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Zanzibar, najibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, athari za mabadiliko ya tabianchi siku zote zinasababishwa na zinachangiwa kiasi kikubwa na shughuli za kibinandamu ambazo binadamu wanafanya katika maisha yao ya kila siku. Zikiwemo shughuli za ukataji wa miti, shughuli za uharibifu wa vyanzo vya maji, shughuli za uchomaji wa misitu, shughuli za ufanyaji wa shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya hifadhi na shughuli nyingine. Kwa hiyo hatua moja ambayo tumeichukua kwanza ni kuwaelemisha wananchi, kuwaeleza athari ambazo zinapatikana baada ya wao kufanya hizo shughuli za kiubinadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili amabalo tunalifanya ni kusimamia sheria. Kwa sababu mbali na kuwaelimisha lakini kwa vile sheria zipo ni kuzisimamia sheria. Tatu ni kuchukua hatua za kisheria kwa wale wote wanaochafua ili lengo na madhumnuni tusiwape mzigo wengine wakina Zima Moto na watu wanaoshirikiana maafa na watu wengine.

Mhehsimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuanzisha mfuko wa mabadiliko ya tabianchi kusaidia kupambana na athari za mabadiliko ya Tabianchi?

Supplementary Question 3

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa masuala ya badiliko ya tabianchi si masuala ya ki-Muungano lakini masuala ya mikataba ya kimataifa na masuala ya mikataba ya kikanda ni masuala ambayo yanahusika moja kwa moja na masuala ya kimuungano je mtaishirikisha vipi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika matayarisho ya mfuko huo wa mazingira?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimia Mwenyekiti, kwanza pamoja na majibu mazuri sana aliyoyatoa Comrade Chillo, Naibu Waziri wangu naomba kujibu swali la nyongeza la ndugu yangu Simai, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli suala la mazingira si suala la Muungano. Hata hivyo, katika kipindi chote, kwa sababu mazingira hayajali mipaka, tumehakikisha kutekeleza miradi mbalimbali upande wa Tanzania Bara na upande wa Visiwani. Ndiyo maana leo hii tuna mradi mkubwa wa ujenzi wa ukuta kule Wete Pemba, hali kadharika Kaskazini A kuna mradi unaendelea. Hata hivyo katika mradi wetu, na juzi mmeona tulikuwa na tukio kubwa sana la kupokea Mwana Mfalme katika nchi yetu katika mradi wa carbon credit, na kwenye jambo hili tumeshirikiana kwa kizuri zaidi. Kwa hiyo huku tunakokwenda sasa ushirikiano wetu unakuwa mkubwa zaidi; na hata katika vikao hivi vya awali ambavyo tumeendelea kuvifanya vyote tunashiriki kwa umoja na Ofisi ya Makamu wa Kwanza Zanzibar kule, kwa lengo la kuhakikisha kwamba mazingira tunayashughulikia wote kwa upana wake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuanzisha mfuko wa mabadiliko ya tabianchi kusaidia kupambana na athari za mabadiliko ya Tabianchi?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na jitihada nzuri za Serikali ambazo wiki iliyopita tuliona imetoa kanuni na miongozo ya namna gani Taifa litanufaika na namna ya kuuza ile hewa ya ukaa, kwa maana ya Carbon emission.

Je, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira iko tayari kutoa mafunzo kwenye Halmashauri ambazo zimekuwa mstari wa mbele katika kupanda miti kama ilivyo Halmashauri ya Mafinga, Mufindi, Kilolo na Halmashauri katika Mkoa wa Njombe?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chungahela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefika wakati tumeona kwamba jambo hili la biashara hii ya hewa ukaa ni jambo ambalo pamoja na kwamba lina umaarufu lakini bado lina ugeni kwa baadhi ya maeneo katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa ambacho tumekifanya kwanza tumeandaa kanuni. Tayari kanuni zipo na katika kanuni zile tayari imeelezwa namna ambavyo tutapita kila kijiji na kila eneo. Hivi tunavyokwambia tayari tumeshashirikiana na Wizara nyingine za kisekta wakiwemo watu wa Halmashauri na Wizara nyingine ili lengo na madhumuni kupitia maeneo yote ya Tanzania hasa kwa upande huo; ili lengo na madhumuni kuwaeleza wananchi fursa na faida zinazopatikana katika biashara ile ikiwa ina mnasaba wa kutunza na kuhifadhi mazingira. Kwa hiyo nimuhakikishie
Mheshimiwa Mbunge katika maeneo aliyoyataja yote tutapita, tutatoa elimu, tutawaelimisha wananchi ili waweze kujua fursa na faida zinazopatikana katika biashara hii ya carbon credit.