Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha Taasisi ya TAKUKURU katika uwajibikaji wake?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nishukuru majibu mazuri ya Serikali. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali bado tuna changamoto nyingi hasa kwenye upande wa magari katika taasisi hii ili waweze kufanya kazi zao vizuri na kurahishisha kazi zao;

Je, Serikali ina mpango gani kuhusiana na masuala mazima ya magari ya usafiri kwa Taasisi hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu la pili;

Je, Seriikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Taasisi hii, ambao bado maeneo mengi tuna changamoto kubwa ya watumishi kwenye taasisi hii, ili waweze kufanya kazi vizuri na tukiangalia Taasisi hii ina - deal na masuala ya rushwa na bado tuna changamoto nyingi sana katika nchi hii kuhusu suala la rushwa?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu changamoto ya usafiri, hili linachukuliwa umuhimu wa pekee, na hata kwenye bajeti ijayo tunaomba nafasi ya kuongeza vyombo vya usafiri, ili kuwasaidia maafisa wetu wa TAKUKURU kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile suala la kuongeza watumishi tunaendelea nalo ni zoezi endelevu. Kwa ushahidi Waheshimiwa Wabunge wote mnajua hata mwaka huu TAKUKURU ilipata nafasi na mpaka sasa kwenye kipindi hiki, bado wanaendelea na mchakato. Tangazo lao la mwisho lina kama wiki mbili hivi bado wanaendelea kufanya mchakato wa kupata watumishi zaidi. Kwa hiyo hili zoezi la kuongeza watumishi ni zoezi endelevu kulinganna na upatikanaji wa fedha na namna Serikali itakavyopata nafasi ya kuongeza nafasi zaidi.