Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ukerewe kitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Nampongeza Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa hatua kubwa iliyofikiwa ya ujenzi wa chuo hiki cha VETA.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa dhamira ya Serikali kujenga vyuo vya VETA ni kusaidia vijana wetu kupata taaluma itakayowasaidia kujiajiri au kuajiriwa kulingana na mazingira yao, nataka kujua, ni kozi zipi au aina ipi ya mafunzo itakayotolewa kwenye chuo hiki cha VETA ukerewe?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyozungumza kwenye majibu ya msingi kwamba mafunzo tutaanza mwezi wa Nne na tutaanza kwa kozi fupi; na tuliwaelekeza Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya, katika Mabaraza yetu ya Madiwani waweze kuamua au ku-detect na aina ya kozi ambazo tunatarajia kuanza nazo; ziko zile kozi za jumla ambazo tunatarajia kuanza nazo kama za ufundi umeme wa majumbani, uchomeleaji na ufundi wa mabomba; hizo ni kozi muhimu ambazo tunatarajia kuanza nazo katika kipindi hicho kifupi.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ukerewe kitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi. Serikali imeahidi kujenga Chuo cha VETA Jimbo la Mbulu Vijijini na tumeandaa ekari 50, na umetuma wawakilishi wako; je, lini mnaanza kujenga Chuo cha VETA Mbulu Vijijini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Flatei, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika swali la mwanzo kwamba ujenzi wa vyuo 63 unatarajia kuanza hivi karibuni, kwa hivi sasa tunaandaa michoro pamoja na kufanya geotechnical survey, topographical survey, pamoja na kufanya estimate kwa ajili ya kuanza ujenzi kwenye maeneo mbalimbali, ikiwemo na Wilaya ya Mbulu. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ukerewe kitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Wilaya ya Tarime haina Chuo cha VETA. Mwaka 2022 niliuliza swali hili hili kwa Mheshimiwa Naibu Waziri na akaahidi kwamba wataiweka kwa upande wa Rorya na Tarime. Nataka nijue, katika hivyo vyuo 63 ambavyo mnatarajia kujenga, Wilaya ya Tarime nayo imo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika kipindi kilichopita Mheshimiwa Mbunge aliuliza hoja hii. Naomba tu Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi hiki cha maswali uje kuangalia orodha iwapo kama Wilaya walioiyoitaja ipo au haipo.