Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Ushetu?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza niwapongeze Wizara niwapongeze Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri wanazofanya. Kwa kuwa Manispaa ya Kahama ina chuo cha FDC ambacho kinafanya kazi kama ile ile ya Chuo cha VETA: Kwa nini sasa chuo hiki cha VETA kisijengwe katika Halmashauri ya Ushetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili: Kwa kuwa uhitaji wa Chuo cha VETA kwa wananchi wa Ushetu mkubwa sana kulingana na ongezeko kubwa la vijana ambao wanamaliza vyuo vikuu lakini hawaendelei na masomo ya juu: Kwa nini sasa Serikali isione hili kwa umuhimu kulingana na umbali wa kilometea zaidi ya 113 kutoka Ushetu kuja Manispaa ya Kahama?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kuwa Wizara haipangi maeneo ya kujenga vyuo hivi vya VETA, ni jukumu la Serikali za Mikoa pamoja na Wilaya kupanga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa vyuo hivi vya VETA. Naomba nitoe wito kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakuu wa Mikoa washirikishe Waheshimiwa Wabunge wa maeneo mbalimbali kuhakikisha kwamba wanakwenda kupanga maeneo sahihi ya kuweza kufanya ujenzi wa vyuo hivi vya VETA.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lakwe la pili, tunajua umuhimu wa vyuo hivi na hivi sasa tumeanza katika ngazi ya Wilaya pamoja na Mikoa; baada ya kukamilika zoezi hili katika ngazi za wilaya pamoja na mikoa, tutafanya tathmini ya kina ili kuweza kuona namna gani tunaweza kuzifikia zile Halmashauri ambazo labda ziko mbali na maeneo ambayo yamejengwa katika VETA zile za Wilaya pamoja na Mikoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Ushetu?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakwenda kujenga VETA katika Jimbo la Arumeru Magharibi katika Wilaya ya Arumeru?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyozungumza katika majibu ya msingi, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba inajenga vyuo vya VETA katika kila Mkoa na Wilaya nchini na tumeweza kufikia Mikoa yote na hivi sasa tunakamilisha Mkoa wa mwisho ule Mkoa wa Songwe. Katika mwaka huu wa fedha tunakwenda kujenga katika Wilaya 63 ambazo zilikuwa hazina vyuo hivi. Iwapo kama Arumeru ni miongoni mwa Wilaya zile 63 bila shaka tutaifikia wilaya hii na kuhakikisha kwamba tunakwenda kujenga katika Wilaya ya Arumeru.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Ushetu?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Wilaya ya Kishapu ni moja kati ya wilaya ambazo zinatekeleza ujenzi wa miradi hii ya VETA; na mpaka sasa hivi mradi huu una zaidi ya miaka mitatu uko katika ujenzi, lakini bado kuna upungufu wa ukamilishaji wa umeme, furniture, maji, na baadhi ya miundombinu katika maeneo hayo. Ni zaidi ya Shilingi milioni 400 zinahitajika kwa ajili ya kukamilisha mradi huu. Ni lini Serikali itakamilisha suala la kuleta fedha kwa ajili ya kukamlisha mradi huu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge wa Kishapu na Waheshimiwa Wabunge wengine ambao maeneo yao tayari tumeweza kujenga vile vyuo 25. Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mwaka huu tayari ameshatoa jumla ya Shilingi bilioni 10.3 kwa ajili ya kukamilisha maeneo yale katika vile vyuo vyote 25. Katika zile kazi ambazo bado hatujakamilisha, na tayari tumeshaanza kuzipeleka kwenye maeneo yale kwa lengo la kukamilisha kazi hizo. Kwa hiyo, muda mfupi ujao tutakuwa tumekamilisha. (Makofi)

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Ushetu?

Supplementary Question 4

MHE. NG'WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ilitenga eneo la ekari 50 kuipa Wizara ya Elimu bure kabisa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA: Sasa ni lini chuo hiki kitaanza kujengwa rasmi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ng’wasi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Ilemela ni miongoni mwa Wilaya 63 ambazo tunaanza ujenzi katika mwaka huu wa fedha.