Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudisha Shamba la Kijiji cha Ng’ang’ange kwa wananchi kufuatia mauziano kati ya EFATHA na Kijiji kutofuata sheria?

Supplementary Question 1

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Kwa kuwa mgogoro huu umekuwa ni wa muda mrefu na ni kero kubwa kwa wananchi wa Ng’ang’ange; je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kufanya ziara katika kijiji hicho ili kuweza kutatua hiyo kero kwa wananchi? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza linaloulizwa kwa niaba ya Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kumhakikishia Mbunge kwamba kwa kuwa tumepanga ziara ya Mkoa wa Iringa, ambayo tutataka tutembelee majimbo yote na Halmashauri zote za Iringa, niko tayari pia kufika Halmashauri ya Kilolo ili kwenda kukutana na wananchi tuzungumze na kumaliza mgogoro huu. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudisha Shamba la Kijiji cha Ng’ang’ange kwa wananchi kufuatia mauziano kati ya EFATHA na Kijiji kutofuata sheria?

Supplementary Question 2

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Serikali ina mpango gani wa kuwarudishia mashamba wananchi waliodhulimiwa na taasisi ya EFATHA Kijiji cha Moro, Msandamungano na Mpwapwa, vilivyopo Wilaya ya Sumbawanga Vijijini? Ahsante.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mgogoro uliopo baina ya vijiji hivo vilivyotajwa na Shirika la Efatha Ministry ambapo katika kuhangaika nalo, tunatambua kwamba zipo kesi zinazoendelea na nyingine ambazo zimeshaamuliwa. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakapokuwa tunafanya ziara ya Nyanda za Juu Kusini, tutafika na eneo la Rukwa ili kuzungumza na wananchi na kutatua mgogoro uliopo.