Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka wahudumu wa afya na madaktari kwenye Vituo vya Afya na Hospitali ya Wilaya ya Tanganyika?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kwanza niipongeze Serikali kwa kujenga vituo vya afya na hospitali ya Wilaya. Kwa bahati mbaya sana idadi ya watumishi ambao ndio wanaokuja kufanya kazi kwenye maeneo husika kwenye vituo vya afya na hospitali ya wilaya bado ni wachache, Halmashauri yangu ya Wilaya kwenye hospitali ya wilaya mahitaji ya watumishi ni 608 waliopo ni 40 tu, kitu ambacho wanashindwa kufanya kazi na wanashindwa kutoa huduma ile iliyokusudiwa.

Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itapeleka wahudumu hasa kada ya wauguzi ili waweze kufanya kazi na hospitali ya wilaya ianze kufanya kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Serikali imeleta X- ray kwenye eneo la Wilaya ya Tanganyika, kinachokwamisha sasa hivi ni Bodi ile ya Mionzi kutokwenda kuthibitisha. Je, ni lini watawapeleka wataalam hao na hiyo X-ray ilishafungwa kama miezi minne iliyopita? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imejenga Hospitali ya Halmashauri ya Tanganyika na hospitali ile imeanza kutoa huduma za afya kwa awamu ya kwanza na watumishi waliopo 40 kwa sasa ni wale ambao wanatoa huduma za awali. Serikali imeweka utaratibu mzuri kuhakikisha kwamba majengo mengine yanapoanza kutoa huduma, watumishi pia wanapelekwa, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hawa watumishi 608 wanahitajika pale hospitali itakapoanza kutoa huduma katika majengo yote, lakini kwa sasa watumishi 40 wanatoa huduma zile za awali na Serikali itaendelea kupeleka watumishi ili waweze kutoa huduma zote katika wodi ambazo zinaendelea na ukamilishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la x-ray ni kweli Serikali imepeleka digital x-ray katika Halmashauri ya Tanganyika kama ambavyo imepeleka katika Hospitali za Halmashauri nyingi kote nchini na wataalam wa mionzi kutoka Arusha tutawasiliana nao wafike Tanganyika ili waweze kufanya ukaguzi na kutupa kibali cha kuendelea na huduma za x-ray, ahsante.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka wahudumu wa afya na madaktari kwenye Vituo vya Afya na Hospitali ya Wilaya ya Tanganyika?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Serikali imejenga vituo vingi ikiwepo katika Jimbo la Makambako, Kituo cha Ikelu, Kitangililo na Lyamkena.

Je, ni lini sasa Serikali itatupelekea waganga ili kusudi wananchi waendelee kupata matibabu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Deo Kasinyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imejenga Vituo vya Afya vya Ikelu, Kitandililo na Lyamkena na nimpongeze sana Mheshimimiwa Deo Sanga, kwa namna ambavyo anawapigania wananchi wa Jimbo la Makambako na huduma za afya zimeendelea kuboreshwa. Nimhakikishie kwamba Waganga watapelekwa katika vituo hivi ili waanze kutoa huduma za awali za msingi wakati Serikali inaendelea kuajiri watumishi wengine kwa ajili ya kuwapeleka katika vituo hivi, ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka wahudumu wa afya na madaktari kwenye Vituo vya Afya na Hospitali ya Wilaya ya Tanganyika?

Supplementary Question 3

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kata ya Sunya katika Kituo cha Afya tulipata ajali mbaya sana mwezi Novemba na tulipoteza watumishi karibu sita, sasa kituo kinataka kufungwa. Je, ni nini commitment ya Serikali kuweza kutuletea watumishi hao kwa haraka sana ili kituo kisifungwe? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Jimbo la Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ilitokea ajali na kupoteza watumishi wetu takribani sita katika Kituo cha Afya hiki cha Sunya. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, lakini shughuli za Serikali lazima ziendelee katika kituo kile cha afya na tulikubaliana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, kuhakikisha anafanya mgawanyo wa ndani wa watumishi waende kwenye kile kituo cha afya waanze kutoa huduma. Kwa hiyo, naomba nitumie fursa hii kumkumbusha Katibu Tawala wa Mkoa haraka iwezekanavyo apeleke watumishi kwenye kituo hiki cha afya ili wananchi waendelee kupata huduma za afya, ahsante.