Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa Shilingi Milioni 100 kumalizia Kituo cha Afya Mchomoro zilizoahidiwa na Rais wa Awamu ya Tano?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niishukuru Serikali, kwa kuamua kwamba itatenga shilingi Milioni 400 katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 ili kukimalizia kituo cha afya cha Mchomoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, sisi pia tuna vituo vitatu, Kituo cha Mkongo, kituo cha Rusewa na kituo cha Mputa vya afya, ambavyo ni vya siku nyingi sana. Tuliahidiwa katika Bunge lako tukufu hapa kwamba vitafanyiwa ukarabati.

Je, Serikali ni lini itafanyia ukarabati vituo vya afya vya Mkongo, Rusewa na Mputa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa Mbunge wa Jimbo la Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Halmashauri ya Namtumbo ina vituo hivi vitatu vya afya, amabvyo ni vya siku nyingi vimekuwa chakavu, Serikali imeweka mpango wa kuainisha vituo vyote chakavu lakini kutenga fedha kwa awamu, kwa ajili ya kuvikarabati. Kwa hiyo, ninakuhakikishia Mheshimiwa Mbunge wakati tunatekeleza utaratibu huo, vituo hivi vya afya pia vitaingia kwenye mpango na kukarabatiwa kwa awamu. Ahsante.