Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, Serikali ina kauli gani juu ya maeneo ya ardhi yanayotumika na Serikali au Taasisi zaidi ya miaka 12 yakiwa hayana hatimiliki?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, napenda kupata ufafanuzi, mwaka 1974 mpaka 1980 kulikuwa na program ya Serikali kupitia Wizara ya Mifugo ya kuwasaidia wanakijiji wa Kijiji cha Mekomariro kunenepesha mifugo yao, na baada ya miaka hiyo Serikali ikaacha maeneo hayo. Ni miaka 43 sasa maeneo hayo yanatumiwa na wanakijiji, na eneo lililokuwa linatumiwa na Wizara ya Mifugo halina hati wala halina GN. Ni kwa nini sasa wananchi wenye maeneo hayo bado wanasumbuliwa na Serikali kwamba eneo hilo ni la Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuna maeneo ya migogoro ya Mekomariro, Sirorisimba na Lemololi Mahanga, Ng’oroli na Mahanga, ni lini Serikali itaenda kuwasaidia maeneo hayo kuyapima na kuyapa hati za kimila? Ahsante. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili yaliyoulizwa na Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la shamba la kule Mekomariro ambalo linaonekana halina hati, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo halina ukweli wowote kwa sababu shamba lile tunavyofahamu Serikali, linayo hati. Ila tunatambua ukweli kwamba upo mgogoro baina ya shamba hilo na wananchi katika maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali la pili juu ya lini sasa Serikali itaenda kumaliza jambo hilo? Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kumaliza kujibu maswali hapa, tutakaa mimi na yeye sasa tukubaliane ni lini twende katika eneo hilo ili kumaliza yale ambayo yanaendelea kuleta mgogoro katika eneo hilo.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, Serikali ina kauli gani juu ya maeneo ya ardhi yanayotumika na Serikali au Taasisi zaidi ya miaka 12 yakiwa hayana hatimiliki?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwulize Naibu Waziri wa Ardhi, Serikali inapeleka lini fedha za upimaji wa ardhi katika Halmashauri ya Ushetu hasa katika kata zinazokua kwa kasi; Kata ya Igwamanoni, Kata ya Idahina, Nyankende pamoja na Burungwa?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali lililoulizwa na Mheshimiwa Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maombi ya wananchi wa Ushetu juu ya kupimiwa eneo lao yalishawalishwa kupitia Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa, tutakapokuwa tumeshapata fedha hizo, tutaleta fedha Ushetu ili sasa maeneo yale yaweze kupimwa, kupangwa na kumilikisha wananchi wetu ili maendeleo yaweze kupatikana kama ambavyo Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza napenda nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo ameyatoa kwa Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka pengine nitoe ufafanuzi kuhusiana na hizi pesa ambazo halmashauri zinaomba kwa ajili ya kupanga, kupima na kumilikisha. Naomba watambue, fedha aliyotoa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ile Shilingi bilioni 50 inakwenda kwenye Halmashauri kulingana na maandiko wanayotoa. Fedha ile inakwenda kusaidia kwenye Halmashauri ambazo ndiyo zenye mamlaka ya Upangaji. Kwa hiyo, tunategemea ile pesa isihesabike kama ndiyo fedha inayokwenda kukamilisha kazi, isipokuwa Halmashauri zinatakiwa kutenga fedha ya ndani kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya ardhi. Kwa hiyo ile isihesabiwe kama ndiyo fedha ambayo inategemewa sana katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mamlaka za Upangaji, sisi tuna-support kuongeza kile ambacho ninyi mmetenga kwa ajili ya maendeleo ya Ardhi na siyo kwamba tunatoa bajeti kwa ajili ya ku-fulfill mpango mzima wa kupanga katika maeneo yenu.