Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Wizara inafahamu kwamba baadhi ya maeneo mtandao wa maji haujafika; je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi hawa kwa dharaura?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Naibu Waziri yupo tayari kuongozana nami kwenda kuona adha kubwa wananchi wa kata hizi wanazopata katika kukosa maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali yake mawili, Mheshimiwa Abdallah Chaurembo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa dharura, mara zote DAWASA imekuwa ikijitahidi kuona inafanya kila linalowezekana wananchi wasikose maji kabisa, lakini nawaomba uvumilivu kwa sababu visima tisa ambavyo tunatarajia kuja kuvichimba katika maeneo yale ya Kimbiji; na tutajenga tenki kubwa maeneo ya Lugwadu la Shilingi milioni 15. Haya matatizo yatakoma kabisa.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa hivi jitihada ndogo ndogo zinazoendelea kufanywa na DAWASA, naomba tuendelee kuwavumilia. Kuongozana nawe ni sehemu ya majukumu yangu, hakuna neno, tutakwenda kufanya kazi. (Makofi)

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jiji la Mwanza hususan Manispaa ya Ilemela inakabiliwa na tatizo la maji. Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua visima virefu vya maji ambavyo havifanyi kazi kwa muda mrefu; mfano, Nsumba Kata ya Kiseke, Mtongo Kata ya Kayenze, Lugeye Kata ya Sangabuye na Kisami Kata ya Bugogwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge Viti Maalum Mwanza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli maeneo haya aliyoyataja hususani eneo hili la Jimbo la Ilemela kwa Mheshimiwa dada yangu Angelina Mabula tayari tumeanza kazi ya ufufuaji wa visima. Tayari visima viwili vimeweza kufufuliwa na kazi zinaendelea kuhakikisha visima vyote ambavyo bado vina maji ya kutosha tunakwenda kuvifufua.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 3

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii, katika mradi mkubwa wa maji wa shilingi bilioni 520 wa Mkoa wa Arusha kuna baadhi ya kata ya wilaya ambazo mradi huu unapita lakini maji hayajasambazwa katika Wilaya ya Arumeru na Arusha Mjini.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kusambaza maji kwenye maeneo haya?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu ni mkubwa na umetumia fedha nyingi na tunatarajia tija iwe ni kubwa maeneo yote ambayo mradi unapita lazima maji yatawafikia. Naomba niwe nimelipokea na kuhakikisha nalifuatilia kwa karibu maji yaweze kuwafikia kwa haraka.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, siko mbali sana na swali alilouliza mtu wa Mbagala kwa sababu kata ulizozitaja ndiyo mtandao huo huo wa Kata ya Buza, Makangarawe, Sandali na Vituka. Tunaomba na sisi maji haya yaweze kusambazwa kule kwetu.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba niseme nimepopkea, maji yatafika.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 5

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona. Mradi wa maji wa Matwiga phase one ni wa muda mrefu na unakwenda kwa kusuasua. Je, ni lini Serikali sasa itaukamilisha mradi huu ili wananchi wa Kipembawe waweze kunufaika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu unafanyiwa kazi kwa jitihada kubwa sana, Mheshimiwa Mbunge naomba uendelee kuwa na subira kidogo, mambo mazuri yanafika pale.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 6

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, Wilaya ya Makete mlitupatia shilingi bilioni 1.7 za mradi wa maji kutoka Lumage kwenda Madihani na kutoka Usalimwani kwenda Mfumbi, mkandarasi hajafika hadi leo.

Ni ipi kauli ya Serikali dhidi ya mkandarasi huyu ambaye anaigharimu Serikali hadi sasa kwenye suala la maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara tulishatoa tamko kwa wakandarasi wote ambao watataka kuturudisha nyuma watarudi wao. Mheshimiwa Mbunge nafuatilia mkandarasi huyu sababu zilizompelekea kutofika, mimi na wewe naomba tukutane baada ya Bunge hili tuweze kufanyia kazi.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 7

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Katika maeneo yenye changamoto kubwa sana ya maji ikiwemo ni Jimbo la Mtwara Vijijini, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inaondoa kero hii ya maji katika Jimbo la Mtwara Vijijini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Shamsia, Mbunge wa Mtwara Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge naamini unafahamu jitihada ambazo zinafanywa na Wizara katika eneo lako na tumeshaongea mara nyingi, Mheshimiwa Mbunge naomba tuendelee kuwasiliana kama unavyofanya tutakuja kuhakikisha maji yanafika maeneo yote ambayo tayari miradi inaendelea.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 8

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, kuna utekelezaji wa maji katika miji 28, ningependa kufahamu ni jambo gani linakwamisha uwezeshaji wa utekelezaji wa mradi huu hadi hivi sasa haujaanza katika miji 28?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahya Mhata kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi wa miji 28 kimacho unaweza ukaona haujaanza lakini tayari wakandarasi walifika maeneo yote na tayari wanaendelea kufanya kazi ambazo siyo za site lakini kuanzia Februari hii tunatarajia wakandarasi wengi kuja kuanza kuwaona huko kwenye site na kufanya kazi zile zinazoonekana kwa macho moja kwa moja.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 9

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Jimbo la Kigoma Kusini vipo vijiji vilivyopakana kabisa na Ziwa Tanganyika lakini vijiji hivyo havijapatiwa maji. Ni mpango upi wa Serikali kuvipatia vijiji hivyo vinavyopakana na Ziwa Tanganyika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo haya anayoyatamka Mheshimiwa Mbunge tayari jitihada zinafanyika na sisi kama Wizara tunatamani kuona tunatumia vyanzo vya uhakika kwa miradi yetu kwa hiyo vijiji hivi ambavyo viko pembezoni mwa Ziwa Tanganyika navyo ni sehemu ya maeneo ambayo tunaendelea kuyawekea mkakati wa kupata maji.

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 10

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Kata ya Mkundi, Nanyanga pamoja na Mchichira, Wizara ilileta mitambo ya kuchimba maji na maji yakapatikana lakini mpaka leo wananchi wale hawajaanza kuyatumia maji yale. Je, ni upi mpango wa Serikali kuhakikisha inaleta vitu ili wananchi waweze kutumia maji.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Katani Katani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuchimba kisima ni hatua moja, baada ya hapo tunakuja sasa kwenye usambazaji. Hivi punde tutajitahidi kuhakikisha visima hivi vilivyochimbwa siyo tu kwenye eneo lako hata pale Mtwara mjini tuna visima tulishachimba na sasa tunaelekea sasa kwenye utekelezaji wa usambazaji Mheshimiwa Mbunge.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Supplementary Question 11

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na jitihada kubwa ambayo Serikali imefanya ya kutupa mkandarasi Palemon kwa ajili ya maji katika Kijiji cha Puulu, Songambele na Ngee. Mkandarasi huyu ana zaidi ya miezi mitano toka alipoonyeshwa mradi hajaonekana kabisa, wananchi wanalalamika, nini kauli ya Serikali kuhusu mkandarasi huyu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya, Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia Bunge lako Tukufu kusema wakandarasi wote ambao hawajafika kwenye maeneo ya kazi wafike mara moja kadiri ya mikataba yao inavyowataka. Nje ya hapo sisi kama Wizara tutachukua nafasi yetu na wasije wakatulaumu.