Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini adha ya Walimu kukaa chini kwa kukosa Ofisi Shule za Msingi za Maendeleo, Bonyokwa na Kinyerezi JICA itatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kuna pesa ambazo zinakuja sasa hivi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa. Swali la kwanza; je, ni kwa nini Serikali wakati inaleta hizo pesa ilete pamoja na hizo pesa za kujenga ofisi za walimu kwa sababu kumekuwa kuna tofauti kubwa kati ya madarasa ambayo yanakuja kujengwa lakini Walimu wanakuwaqa hawana ofisi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je ni lini Serikali itanunua furniture za ofisi ambazo zimejengwa na manispaa zipo tu na hazina furniture za walimu? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Jimbo la Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa sasa wa Serikali ni kujenga na kuongeza madarasa katika maeneo ambayo yana uhitaji na ndio maana katika miradi mikubwa ambayo tunayo sasa kwa maana Mradi wa SEQUIP pamoja na BOOST yote miwili kwa pamoja ina thamani karibU trilioni 2.35.

Mheshimiwa Spika, katika yale madarasa maeneo mengine wanajiongeza, ukipeleka madarasa mawili wanajenga na ofisi katikati ambalo ni jambo jema. Tumekuwa tukipeleka fedha kwa ajili ya majengo ya utawala. Kwa hiyo sisi tutaendelea tu kuziagiza halmashauri kutenga fedha kujenga maeneo ya utawala, lakini ofisi nyingine waendelee kujiongeza kwa kuweka ofisi katikati ya madarasa ambayo tumekuwa tukiyapeleka huko. Kuhusu fanicha nafikiri ni maelekezo yetu pia kwa halmashauri zote nchini kuwapatia furniture kwenye staff rooms zote za shule katika maeneo yao, ahsante sana.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini adha ya Walimu kukaa chini kwa kukosa Ofisi Shule za Msingi za Maendeleo, Bonyokwa na Kinyerezi JICA itatatuliwa?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kuishukuru Serikali kwamba katika Mkoa wa Simiyu tuna madarasa mengi sana, lakini kuna upungufu wa Ofisi za Walimu. Walimu wetu hawafanyi kazi kwa furaha kwa sababu hawana ofisi wengi wanakaa kwenye miti. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu ujenzi wa Ofisi za Walimu? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Minza Mjika, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa wa Simiyu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeziagiza halmashauri kujenga ofisi kwa kila halmashauri kutenga mapato yao ya ndani kwa sababu moja ya jukumu letu sasa ni kujenga madarasa, mabweni, mabwalo ya chakula ambayo ndio kazi kubwa tunayoifanya sasa ikiwemo na majengo ya utawala kwa baadhi ya shule. Kwa hiyo kwa kadri tutakavyokuwa tunatafuta fedha tutakuwa tunapeleka, lakini tumeziagiza halmashauri kutumia mapato yao ya ndani kufanya hivyo. Kwa hiyo tunafanya hivyo kwa Mkoa wa Simiyu na mikoa yote nchini, ahsante sana. (Makofi)

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni lini adha ya Walimu kukaa chini kwa kukosa Ofisi Shule za Msingi za Maendeleo, Bonyokwa na Kinyerezi JICA itatatuliwa?

Supplementary Question 3

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Walimu wengi wanakosa viti na meza nzuri za kukaa na kuweza kufanya kazi zao vizuri. je, Serikali inalijua hilo na ina mkakati gani wa kulitatua? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mtwara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunatambua changamoto hizo katika baadhi ya shule na tunazifanyia kazi. Ahsante.