Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza: - Chaguzi za Madiwani zilifanyika katika kambi ya wakimbizi Katumba wa 2015:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha chaguzi za Serikali za Vijiji na Mtaa?

Supplementary Question 1

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nifanye masahihisho kidogo ni Kata ya Katumba siyo Mtumba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya maeneo ambayo ilikuwa ni makazi ya wakimbizi yalikuwa yanapata ufadhili wa Shirika la Wakimbizi Duniani (UNHCR) katika huduma mbalimbali za jamii ikiwemo elimu, maji na barabara. Ningependa kujua Serikali ina mpango gani wa kuhusisha UNHCR kwa kuwa makambi yanaenda kuvunjwa, msaada gani ambao watautoa ili kuboresha miundombinu mbalimbali ambayo sasa hivi imekuwa ni hafifu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema pale awali kwamba maeneo haya uchaguzi bado haujafanyika, japo uchaguzi haujafanyika jukumu kubwa la Serikali ni kuhakikisha katika maeneo hayo, wanaendelea kupata huduma za kijamii kwa ufanisi kama kawaida. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI jambo hilo tunaliangalia kwa karibu zaidi na kwa kuanza changamoto yetu kubwa ni kuisukuma bajeti hii ambayo sasa hivi imepitishwa kuhakikisha kwamba Halmashauri hii inafanya uchaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo ni kuhakikisha kwamba, kwanza tunajua katika maeneo hayo huduma za kijamii nyingi zilikuwa zinatolewa na Shirika la Wakimbizi Duniani, sasa hivi ni jukumu la Serikali. Hili ni jukumu letu kubwa na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutapeana ushirikiano wa kutosha ili wananchi wa pale waweze kupata huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo miundombinu ya barabara, huduma ya elimu, huduma ya afya na ifike muda na wao wajione kwamba ni wananchi kama wananchi wengine wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza: - Chaguzi za Madiwani zilifanyika katika kambi ya wakimbizi Katumba wa 2015:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha chaguzi za Serikali za Vijiji na Mtaa?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. NCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naitwa Mwanne Ismail Nchemba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, tatizo la Wakimbizi wa Katumba linafanana na tatizo la Wakimbizi wa Ulyankulu na kwa kuwa hawakufanya uchaguzi wa Madiwani. Je, Serikali inasema nini, ni lini utafanyika uchaguzi wa Madiwani katika Jimbo la Ulyankulu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu hao ni wananchi wake, akiwa Mbunge wa Viti Maalum ana kila sababu ya kuona maeneo hayo yanafanyika uchaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka swali hili nilijibu katika Mkutano wetu wa Bunge uliopita, nilisema pale kuna takribani Kata tatu uchaguzi haujafanyika kwa sababu za msingi, bado suala zima la utengamano linaendelea na pale sasa hivi bado Jeshi na Wizara ya Mambo ya Ndani wanaendelea kumiliki eneo lile. Utararibu utakapokamilika jukumu letu kubwa watu wa TAMISEMI baada ya ule mtangamano kuwa vizuri zaidi na eneo lile sasa rasmi likishakuwa chini ya TAMISEMI, mchakato wa uchaguzi sasa utaendelea ili watu wa pale wajikute nao wana Serikali yao halali iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Namba 292