Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Vituo vya Polisi vya Tarafa ya Mang'ula na Kidatu vitakarabatiwa?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Kwa kuwa jana Katibu Mkuu wa CCM, Comrade Daniel Chongolo alipita kwenye ziara katika Jimbo la Kilombero na aliviona vituo hivi na akanielekeza Mheshimiwa Mbunge nije niongee na Waziri wa Mambo ya Ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; je, nikileta nakala ya hati ya ardhi hizo ambazo Mheshimiwa Naibu Waziri amesema, Serikali itakuwa tayari kuanza ujenzi wa vituo hivyo vya Tarafa ya Mang’ula na Tafara ya Kidatu?

Swali la pili; kwa kuwa tayari Tarafa ya Ifakara lipo eneo linalomilikiwa na Jeshi la Polisi na Wizara ya Mambo ya Ndani; je, Serikali iko tayari kuanza kwa haraka kujenga Kituo cha Polisi cha Ifakara?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Meshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge Asenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba maeneo hayo mawili ni ngazi ya Tarafa yanahitaji Vituo vya Polisi, lakini majengo yaliyopo yamechakaa sana, lakini mojawapo ya jengo la JWTZ liko kwenye hifadhi ya barabara, na barabara inayojengwa italiondoa.

Kwa hiyo, ni ahadi yetu kwamba tunaweka katika bajeti ya mwaka 2023/2024 tutakayoipitisha mwezi Juni ili tuweze kuanza mipango ya ujenzi, la msingi tupate hizo hati miliki ili kuhakikisha kiwanja kiko ndani ya mikono ya Jeshi letu la Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kituo cha Ifakara naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, nilitembelea eneo lile kwa kweli wanachangamoto ya kituo, wanahitaji kujengewa kituo kipya cha Polisi ngazi ya Mji wa Ifakara.

Kwa hiyo, ni ahadi yetu pia kwamba tutakipa kipaumbele katika bajeti inayokuja, nashukuru sana.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Vituo vya Polisi vya Tarafa ya Mang'ula na Kidatu vitakarabatiwa?

Supplementary Question 2

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi cha Tarafa ya Nyalonga kilichopo katika Kijiji cha Nyadibuye majengo yake yamechoka sana, na hivi wakati wa mvua yanavuja tena sana.

Swali; lini Serikali itafanya ukarabati wa kituo hicho cha polisi? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce Kamamba, Mbunge wa Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulishazungumza na Mbunge na moja ya ziara yangu ilikuwa nifike, lakini sikuweza kufika kwamba kuna changamoto kwenye kituo hiki na ukanda ule ni ukanda wa mvua kubwa, ni kweli changamoto tunaiona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpe ahadi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutawasiliana na OCD na RPC wa Mkoa wa Kigoma ili katika vipaumbele vyake vya ukarabati wa majengo chakavu ya polisi hiki kipewe kipaumbele, ili hatimaye fedha zitakapotoka kiweze kukarabatiwa, nashukuru.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Vituo vya Polisi vya Tarafa ya Mang'ula na Kidatu vitakarabatiwa?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Msalala hasa Kata ya Ngaya na kata ya Isaka tayari wana eneo na tayari tumeshajenga vituo vya polisi viko kwenye hatua ya renta; sasa ni lini Serikali itatenga fedha ili ije imalizie vituo hivi viwili ili wananchi waweze kupata huduma hiyo haraka? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi anazofanya za kuhamasisha wananchi wake kuchangia ujenzi wa vituo hivi ikiwa ni pamoja na Halmashauri ya Msalala. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri hali ya fedha itakavyoruhusu vituo hivi vya kata mbili ambavyo vimeshajengwa kiwango cha renta tutaviunga mkono kwa kumalizia baadhi ya vifaa vinavyopatikana madukani/viwandani sorry ili ujenzi wake uweze kukamilishwa, nakushukuru.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Vituo vya Polisi vya Tarafa ya Mang'ula na Kidatu vitakarabatiwa?

Supplementary Question 4

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo la uchakavu wa vituo vya polisi ni la nchi nzima; swali langu je, Serikali haioni umuhimu wa kuandaa mpango kabambe wa miaka mitatu kwa ajili ya maboresho ya vituo hivi kwa maana ya kurahishisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mbunge Mheshimiwa Lambert, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpe uhakikisho kwamba kwa kutambua umuhimu wa kuwa na mpango mkakati wa utekelezaji Wizara ya Mambo ya Ndani kushirikiana na vyombo vyake imeandaa mpango wa miaka kumi wa ujenzi na ukarabati wa vituo vya polisi. Kwa hiyo, ulilolisema tumeshalifanyia kazi, mpango ule tunaugawa katika vipindi vya miaka mitano/mitano na miaka mitatu mitatu kwa maana ya Medium Term Expenditure Framework (MTF) ili kuvigharamia, ndio maana tunaposema hapa kwamba tunaingiza, tunatoa kwenye ule mpango mkuu wa miaka kumi tulionao. Nashukuru.