Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itashughulikia suala la mtambo wa kielektroniki ulioharibika kwa zaidi ya mwaka sasa na kusababisha mlundikano mkubwa wa hati za ukaazi katika Idara ya Uhamiaji Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa ruhusa yako nina maswali mawili ya nyongeza: -

Swali la kwanza, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yupo katika jitihada za kuwaita wawekezaji nchini kwetu Tanzania kwa ajili ya kuja kuwekeza nchini mwetu, wakati huo huo pia kuna kuwa na idadi kubwa ya wageni ambao wanakuja Tanzania kwa ajili ya kuja kujifunza.

Je, kwanini vibali vinachelewa?

Swali la pili, ninamuomba Mheshimiwa Waziri kama ataridhia kwake tukaongozana mimi na yeye kufanya ziara ya maksudi kwenda kuangalia mtambo ule ambao ulikuwepo Zanzibar na kuangalia vile vibali walau 100 vilivyochapishwa kwa mwaka huu 2022. Naomba sana hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haji Mbunge wa Pangawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya kuchelewa, kwanza nikiri hii changamoto ipo, lakini changamoto hii inasababishwa zaidi na wananchi wenyewe au wale ambao wanaotaka kuomba vile vibali vyewewe. Sababu moja ni za kimtandao unajua tumeingia katika e-permit kwa hiyo time nyingine inawezekana mtandao ukawa unasumbua ukachelewesha kidogo, lakini sababu nyingine ni kwamba wananchi wenyewe au wale ambao wanaomba zile permit huwa wanafika wakati wanakuwa wanashindwa kukamilisha vigezo na masharti hivi vinapelekea sasa kuchelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa ni kwamba kuna baadhi ya watu huwa wanawapitisha hawa wageni katika njia ambazo siyo rasmi wala siyo sahihi hii inapelekea vilevile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine kwa upande wa kwenda kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi tupo tayari kwa ajili ya kwenda huko kukagua huo mtambo huko Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itashughulikia suala la mtambo wa kielektroniki ulioharibika kwa zaidi ya mwaka sasa na kusababisha mlundikano mkubwa wa hati za ukaazi katika Idara ya Uhamiaji Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la kuwapatia Watanzania vitambulisho vya Taifa limechukua muda mrefu sana na imekuwa na sintofahamu. Kuna Watanzania ambao takribani miaka mitatu mpaka minne wana namba tu hawana kadi.

Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na jambo hili? Kama mmeshindwa muwaambie Watanzania kwamba mmeshindwa na haiwezekani zoezi hili. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hili jambo lilikuwa limekwama kidogo, lakini tulikuwa tuna changamoto na sababu ya kwamba hivi vitambulisho vichelewe kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa nimwambie Mheshimiwa kwamba bado Serikali haijashindwa kuwapatia wananchi vitambulisho, hivi ninavyokuambia vitambulisho vimeshazalishwa na tayari huko Wilayani vimeshasambazwa. Kikubwa ni kwamba kama Wilaya ambavyo vitambulisho havijafika basi tuelezane tujue namna ya kufanya lakini vitambulisho tayari vimeshapelekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, even if vinazalishwa kwa speed siyo ile ya kawaida lakini kwa ufupi ni kwamba vitambulisho vinazalishwa na vitawafikia wananchi ili waweze kupata hiyo huduma ya vitambulisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. (Makofi)