Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K. n. y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Shule nyingine ya Msingi katika Kata ya Ng’ambo Tabora Mjini kwani Kata hiyo ni kubwa?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyopo kwenye shule ya msingi Ng’ambo Tabora ni sawa na changamoto iliyopo kwenye shule ya msingi Igurubi ambayo ni Makao Makuu ya Tarafa ya Igurubi Jimbo la Igunga. Tunayo shule ya msingi ambayo kwa sasa ina wanafunzi wengi mpaka imezidiwa, kwa hiyo tunaomba pia Serikali katika utatuzi wa changamoto hizi iweze kuangalia pia shule ya msingi Igurubi ili iweze kulipatia ufumbuzi wa tatizo hili na changamoto hii ili wanafunzi wetu wasome kwa uhuru? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nicholaus Ngassa Mbunge wa Igunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nae ameeleza tu kwamba katika Jimbo lake la Igunga Tarafa ya Igurubi kuna Shule ya Msingi Igurubi ambayo na yenyewe ina wanafunzi wengi. Nimhakikishie tu kwamba moja ya mpango wa Serikali sasa hivi ni kutapisha shule zote zenye wanafunzi zaidi ya 2000 na ndio maana tuko katika mkakati wa kutafuta fedha na tumezitambua shule zote ambazo zina changamoto hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo mpango huu utakapokamilika maana yake tutawafikia na wao. ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K. n. y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Shule nyingine ya Msingi katika Kata ya Ng’ambo Tabora Mjini kwani Kata hiyo ni kubwa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami ningependa niongeze hapo swali la nyongeza, kwa kuwa Serikali imekiri hapa kwamba shule nyingi zimezidiwa na wanafunzi kwa nini Serikali sasa isitangaze kwamba hapa Tanzania tuna upungufu wa shule badala ya kuendelea kutangaza kwamba tuna upungufu wa madarasa peke yake?(Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Kakunda Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la Mheshimiwa Mbunge tu ni kwamba anataka kufahamu tutangaze kwamba tuna uhaba wa shule na siyo madarasa. Nimhakikishie tu kwamba Serikali inatambua changamoto zote, katika baadhi ya maeneo tuna changamoto ya madarasa na kuna baadhi ya maeneo tuna changamoto ya shule, ndiyo maana katika maeneo ambayo yana changamoto ya shule Serikali tunapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya, kwa hiyo hatuwezi kutangaza kama janga kwa sababu Serikali ipo kazini na inafanya kazi kutatua hizi changamoto ambazo Mheshimiwa Mbunge ameainisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)