Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa magari na nyumba za Askari Polisi Kituo cha Polisi Nungwi?

Supplementary Question 1

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa sasa Nungwi imebadilika hadhi kutoka kijiji kuelekea mji na kwa kuwa sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la watu pamoja na wawekezaji katika sekta ya utalii wa Kimataifa.

Je, Serikali haioni haja ya kuongeza majengo na watendaji ili kukiongezea daraja Kituo cha Polisi Nungwi kutoka daraja C kwenda B?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Nungwi kumekuwa na changamoto kubwa mno ya upatikanaji wa maji jambo ambalo limewapelekea maaskari wengi kuondoka kituoni kwenda sehemu za mbali kutafuta maji hayo.Je, Serikali haioni haja ya kuwachimbia kisima au kutafuta njia mbadala ili kuhakikisha kuna upatikanaji wa maji ya kudumu katika eneo lile? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Simai, Mbunge wa Nungwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja tunatambua kweli maeneo mengi ya vijijini ikiwemo Kijiji cha Nungwi kimekua na kuwa Mji Mdogo na watu wameongezeka, lakini kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, eneo hili ni dogo, kama tuna dhamira ya kupanua, basi Mheshimiwa Mbunge atusaidie kushirikiana na Mamlaka ya Wilaya pale ili tupate eneo la kutosha kuweza kujenga kituo kinachokidhi mahitaji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la upatikanaji wa maji, naomba nishauri kwamba, kazi ya Jeshi la Polisi sio kuchimba visima, lakini kule kuliko na polisi kama walivyo wananchi wengine mamlaka za ugawaji wa maji ziwafikie kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa kuwachimbia kisima. Tutawasiliana na wenzetu wa upande wa Zanzibar ili kuona uwezekano wa kuwapatia kisima wenzetu hawa ili wasiende umbali mrefu kutafuta maji. (Makofi)

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa magari na nyumba za Askari Polisi Kituo cha Polisi Nungwi?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Mwaka, 2013 Kituo cha Polisi cha Mkokotoni kilipata majanga ya kuungua kwa moto na hadi kufikia tarehe 29 Machi, kituo hicho tayari kimekamilika kwa asilimia 95. Je, ni ipi kauli ya Serikali ili kukamilisha asilimia hizi tano ili kituo kile cha polisi kiweze kufanya kazi vizuri kama inavyotakiwa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Usonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ikiwa wananchi wamejitahidi kukamilisha kituo kwa kiwango cha asilimia 95, nachukua dhima ya kuwasiliana na wenzetu wa Jeshi la Polisi kupitia Mfuko wao wa Tunzo na Tozo kukamilisha asilimia tano zilizobaki ili kituo hicho kiweze kukamilishwa. (Makofi)

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa magari na nyumba za Askari Polisi Kituo cha Polisi Nungwi?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Licha ya juhudi kubwa anazofanya Mbunge wa Jimbo la Peramiho, je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi pale Peramiho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Thea Ntara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hitaji la kuwepo Kituo cha Polisi katika eneo la Peramiho ni kubwa kutokana na kukua kwa kasi ya shughuli za kibinadamu kwenye eneo hilo la Peramiho. Namwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa wa Ruvuma, tutaona uwezekano wa kuingiza eneo la Peramiho katika mpango wa ujenzi wa kituo cha polisi. (Makofi)