Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea wahudumu wa kada mbalimbali za afya nyumba bora ili kuboresha makazi yao?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa majibu haya, dah, hadi maswali ya nyongeza yanakuwa na utata. Kwa ruksa yako nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri wakati Serikali inaendelea na mchakato wa kuboresha huduma za afya nchini; katika Jimbo la Kilombero chini ya Kanisa Katoliki imejengwa Hospitali kubwa sana ya Kansa. Hospitali hiyo mpaka leo haijafunguliwa. Baba Askofu anaomba Viongozi Wakuu wa nchi yetu wakafungue Hospitali hiyo. Mheshimiwa Waziri ana majibu gani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. St. Francis Hospital ni hospitali ya kanda, inatibu zaidi ya mikoa 10. Gharama zimekuwa kubwa na wananchi wanalalamikia kwa sababu Serikali imeondoa ruzuku iliyokuwa inatoa zamani: -

Je, Waziri anaweza kusema chochote kwamba wanaweza kukaa na Uongozi wa St. Francis Hospitali ya Ifakara ili kuzungumza namna ya kurejesha ruzuku ya awali?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza amezungumzia hospitali ambayo imefunguliwa, mimi na yeye tutakwenda Kilombero kuiangalia hospitali hiyo na kukagua halafu tuje tushauri mamlaka husika ili taratibu anazozisema ziweze kuchukuliwa hatua.

Mheshimiwa Spika, pili, suala la ile ruzuku ambayo alikuwa anaipata, nafikiri hata juzi tulikuwa tunazungumza hapa na Mheshimiwa Jenista Mhagama kuhusu hata masuala ya watumishi na mambo mengi. Nalo hili tunaenda kulifikiria kwenye bajeti hii na wakati wa bajeti tutawajibu.

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea wahudumu wa kada mbalimbali za afya nyumba bora ili kuboresha makazi yao?

Supplementary Question 2

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi kuuliza swali la nyongeza. Serikali ilianzisha ujenzi wa hosteli kwenye Chuo cha Uuguzi pale Tukuyu mwaka 2008. Ujenzi umekamilika, umefikia hatua ya kufanya finishing tu yaani kuweka madirisha na milango, wanafunzi 150 wanakaa nje ya chuo. Je, ni mpango gani wa Serikali kuhakikisha kwamba majengo yale yanakamilika na wanafunzi wale 150 wanaingia kukaa chuoni? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantona kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo amesema Mheshimiwa Mbunge labda nimwambie tu kwa mwaka huu kwa ajili ya umaliziaji vyuo kama hivi ambavyo vimekaribia kufanyiwa finishing ili watoto waingie ndani, zimetengwa around bilioni 2.7 kumalizia vyuo ambavyo viko 17 vinavyotakiwa kumaliziwa nchi nzima. Kwa hiyo kitamaliziwa kabla ya mwezi wa 12 kila kitu kitakuwa kimekaa vizuri.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea wahudumu wa kada mbalimbali za afya nyumba bora ili kuboresha makazi yao?

Supplementary Question 3

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Jimbo la Lushoto wananchi pamoja na Serikali yao wamejenga vituo vya afya pamoja na zahanati, lakini kumekuwa na changamoto kubwa sana za nyumba za watumishi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za watumishi katika Wilaya ya Lushoto?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo swali la msingi lilieleza kwamba kwa mwaka huu wa fedha zinaenda kujengwa nyumba 300. Naomba tukae na Mheshimiwa Mbunge tuangalie katika hizi 300 kama Lushoto eneo analolizungumzia limeguswa kama halijaguswa, tuone mapema tunaweza tukafanya nini ili hilo litekelezeke.