Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Lengo la barabara hii ni kufungua mawasiliano kati ya Burundi na Tanzania. Kufuatia hili, katika kikao cha ushauri cha Bodi ya Barabara iliamuliwa barabara hii ihamishwe, kipande hiki cha Gwarama – Muhange, kitoke TARURA kwenda TANROADS . Nini kauli ya Serikali kuhusiana na suala hili?

Mheshimiwa Spika, la pili, kwa kuwa barabara hii ni muhimu, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana nami, aweze kuiona hii barabara? Nina hakika akishaiona atakuwa tayari kuchukua hatua za muhimu kujenga barabara hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Kigoma imeipendekeza kupandishwa hadhi; na kwa kuwa Serikali tunafanya kazi kwa pamoja, basi jambo hili tumelipokea na ninaamini wenzetu wa TANROADS na wenyewe wanalo. Kwa hiyo, endapo hii barabara itakuwa inakidhi vigezo vyote, basi Serikali italifanyia kazi na itekeleze kama ambavyo Bodi ya Barabara ya Mkoa imependekeza.

Mheshimiwa Spika, suala la mimi kuongozana naye, nipo tayari mara baada ya Bunge lako Tukufu tutakapomaliza. Ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Barabara ya kutoka Irula katika Jimbo la Kilolo kwenda Image mpaka Kata ya Ibumu ni barabara mbaya sana, haijawahi kuchimbwa hata siku moja: Ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango hata cha changarawe tu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Tendega ameainisha hii barabara ya kutoka Irula mpaka Ibumu kwamba ni bararaba ambayo haijajengwa, basi tutakwenda kufuatilia ili tuone kama imeanishwa kwenye bajeti ili tuweze kuifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Napenda kujua ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara inayounganisha Wilaya ya Shinyanga Mjini na Shinganya Vijijini kutoka Old Shinyanga kwenda Solo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Dkt. Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba kila kitu kipo katika mipango na Serikali tumeainisha maeneo yote yenye vipaumbele. Kwa hiyo, kadri tutakavyoyafikia, maana yake yote yataainishwa. Umuhimu wa hii barabara unafahamika na ndiyo maana mara zote tumekuwa tukifanyia matengenezo. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii na yenyewe itafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Barabara ya kutoka Chala kwenda Mpalamao imekuwa ni ahadi ya viongozi wengi na iliwekwa kwenye ilani lakini mpaka sasa hatuoni kinachoondelea. Ni lini mtatekeleza ahadi hiyo ya barabara ya Chala - Mpalamao?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya kutoka Chala mpaka Mpalamao ni kweli tumekuwa tukiizungumza mara kwa mara, na nimemwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ipo katika vipaumbele ambavyo tumeviweka. Kwa hiyo, tunatafuta fedha ili ianze kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 5

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri kuwa Kata ya Kidatu kuelekea Kata Msola Stesheni katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara, barabara haipitiki kwa sasa: -

Je, Serikali ina mpango gani wa dharura wa kutengeneza barabara ile angalau kwa kiwango cha changarawe ili iweze kupitika?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoanisha Mheshimiwa Mbunge ipo katika mipango ya Serikali ya kuhakikisha kwamba inajengwa. Kwa hiyo, tusubiri tu muda utakapofika na barabara hiyo itafanyiwa kazi.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 6

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Barabara ya Tabora - Mwambali imeshafanyiwa usanifu tangu mwaka 2020, lakini mpaka leo haijaanza kujengwa. Ni lini barabara hii itaanza kujengwa? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu baadhi ya maswali, barabara zote ambazo tayari zimefanyiwa usanifu na ambazo zipo katika mpango wa Serikali ni kwamba sasa hivi kitu kimoja ambacho tunakitafuta ni fedha ili tuanze kuzitekeleza. Kwa hiyo, ninaamini kwamba mara fedha itakapopatikana, basi na hii barabara itaanza kujengwa. Ahsante sana.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 7

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba Serikali barabara yetu Bigwa na barabara yetu Ngerengere, Matuli, Matulazi:-

Je, lini Serikali itatuangalia?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamisi Taletale, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Ngerengere kwenda Matulazi ni moja ya barabara muhimu na ya kipaumbele. Moja ya kazi kubwa ambayo tunaifanya sasa hivi, ni kufanya usanifu ili sasa tuiweke katika mipango yetu ya kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo. Ahsante sana.

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 8

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya Kisesa, Bujola kwenye Makumbusho ya Machief wa Kisukuma imebaki kilometa 1.3.

Je, ni lini itakamilishwa na Serikali kwa kiwango cha lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya ambayo ameianisha ni kwamba mpaka sasa Serikali imeshafanya kazi sehemu kubwa. Kwa hiyo, sehemu ndogo ya kilomita 1.3 iliyobakia na yenyewe ipo katika mpango ili iweze kukamilika. Ahsante sana.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Supplementary Question 9

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nilitaka kujua kuna barabara yetu ya Chemba - Soya ambayo kwa muda mrefu imekuwa na shida kubwa na mara kadhaa viongozi walipokuja waliahidi kuijenga walau kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, naomba kujua commitment ya Serikali katika hili.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ahadi zote ambazo viongozi wamezianisha zipo katika mpango. Kwa hiyo, hata hii ambayo barabara ameiainisha Mheshimiwa Mbunge ya kutoka Chemba mpaka Soya ni miongoni mwa barabara zetu, zipo katika mipango yetu. Ahsante sana.